Msumbiji hakuna ISIS, ni usanii na dhulma. Ukifuatana nami utajua

Kwa kifupi tu, hali si nzuri.. Jeshi liko on patrol 24 hours.. Kuna kambi kambi ndogo nyingi tu alongside Ruvuma River kuulinda mpaka..

Wapo Makanali ambao ndio wanacoordinate hiyo kazi chini ya brigade kubwa ya Songea na Kambi nyingine ndogo za Nachingwea na Naliendele Mtwara.

Hao watu wanaweza wasiwe ISS lakini ni magaidi waliojificha kwenye dini ya kiislamu. Muda mfupi badala ya shambulio la Kwanza la Kitaya walikamatwa watu makazi yao yakiwa Msikitini kijiji cha Msimbati na wengine Kijiji cha Madimba ilipo Plant ya kuchakata gesi.

Vifaa vingi tu vya kisasa vishapelekwa huko mpakani na msitu mkubwa ulioko Msumbiji wanakodhaniwa hao watu wanajificha unafyekwa kidogo kidogo kusaidia operation. Hali huku si nzuri, watu saa 1 jioni wako ndani
Umetoa tamko kuonesha uelewa halafu umeturudisha kule kule.Kwanini kama ni magaidi wajifiche ndani ya dini ya kiislalmu.Kwani nani kasema dini ya kiislamu ni dini ya magaidi.
Wapiganaji gani ambao wanaweza kupigana kuuwa na hata kukimbizana na jeshi halafu wakajifiche msikitini.Misikiti inakuwa kwenye mitaa watu wanaoswali wanajuwana.Kama walikutwa watu misikitini hii ni kwa vile watu wakipatwa na hofu mara nyingi wanakimbilia nyumba za ibada kudhani watapata amani kama ilivyokuwa misikiti ya Rwanda miaka ile.Na hata watu waovu nao wakiona usalama wao uko hatarini hukimbilia huko.Lakini huwezi kusema ukikuta mtu muovu yumo humo ukasema ndio kambi yake ya kufanyia uovu.Ukiwa na mawazo hayo wewe mwenyewe itakuwa una chuki na hiyo nyumba.
 
Basi utuambie hao wauao wananchi,basi ni akina nani?
Yako majina mengi yanayofanana nao na pengine ndio majina yao yanayowafaa. Wahuni,wananchi waliofukuzwa kwenye ardhi zao kwa njama,Watoto na wajukuu wa waliouliwa watu wao,Majina mengine mengi yapo yanayowafaa lalkini ISIS ni kutudanganya na kututilia fitna katika jamii,
Katika hilo kundi wanaweza kuwepo waislamu basi isiwe ndiyo kisingizio tena cha kusema kundi zima ni la waislamu wenye msimamo mkali tena ni tawi la wale wa Iraq na Afghanistan.Hapo ni kutudanganya na kuachiwa uendelee kusema hivyo unakaribisha madhara kwa wasiokuwa na hatia huko mbeleni.
 
Si kweli.. suala la ardhi sio sababu. Kwahiyo unataka kusema wamakonde ndio wanamiliki mpaka bandari huko ambayo hao magaidi walishawahi kuiteka na ikawa chini yao?

Kama ni ardhi mbona wengine wengi tu wanauliwa ambao sio wa Tanzania? Kama tatizo ardhi ambayo ipo Msumbiji kwanini waje kuua mpaka huku kwetu na kusema wanataka kusimamisha dola yao??
Unao ushahidi wa haya unayo yaandika ?
 
Umeona viashiria vya fitna hivyo.Wengi wanashindwa kuving'amua na wanaacha watu wanaumizwa kwa visingizio mbali mbali.Hasa jamii ya kiislamu inaathirika sana na uzushi wa aina hiyo kutoka kwa majirani zao na kutoka vyombo vya dola.
Jamii ya kiislam inaathirika vipi wakati wanaofanya matukio hayo ni wao wenyewe?
 
Jamii ya kiislam inaathirika vipi wakati wanaofanya matukio hayo ni wao wenyewe?
Si imesemwa wanaofanya ni waislamu.Kama ni hivyo basi waislamu wanauwana wenyewe kwa wenyewe si ndio kuathirika kwenyewe huko. Kwa upande mwengine fikiria vizuri ikiwa eneo hilo la Msumbiji linatajwa lina waislamu wengi kuliko maeneo yote ya nchi hiyo.

Sasa inakuwaje waislamu wajikusanye hapo halafu iwe inauwa wenzao tena kwa kuwasimamisha njiani tu na kuwaswaga kwenye uwanja wa mpira si inawezekana katika hao kuna ndugu au mjomba wake.

Sasa hao ni waislamu au ni viumbe gani kwani hata wanyama wana huruma na wenzao wa karibu.Kwanini wasiende kwenye vijiji vyenye watu wa dini nyengine na mbali na watu wa karibu yao.

Ukizingatia mantiki hii utapata dalili kuwa ama taarifa hizo si za kweli na au watendaji si waislamu wachilia mbali majina yenye utata kama hayo ya ISIS.
 
Umetoa tamko kuonesha uelewa halafu umeturudisha kule kule.Kwanini kama ni magaidi wajifiche ndani ya dini ya kiislalmu.Kwani nani kasema dini ya kiislamu ni dini ya magaidi.
Wapiganaji gani ambao wanaweza kupigana kuuwa na hata kukimbizana na jeshi halafu wakajifiche msikitini.Misikiti inakuwa kwenye mitaa watu wanaoswali wanajuwana.Kama walikutwa watu misikitini hii ni kwa vile watu wakipatwa na hofu mara nyingi wanakimbilia nyumba za ibada kudhani watapata amani kama ilivyokuwa misikiti ya Rwanda miaka ile.Na hata watu waovu nao wakiona usalama wao uko hatarini hukimbilia huko.Lakini huwezi kusema ukikuta mtu muovu yumo humo ukasema ndio kambi yake ya kufanyia uovu.Ukiwa na mawazo hayo wewe mwenyewe itakuwa una chuki na hiyo nyumba.
Unawezaje kuutofautisha Uislam na ugaidi??
 
Hivi mtoa mada unawatetea ISIS au waislam au hao magaidi wa mozambique?
maana wote ni kitu kimoja.
 
Nilidhani umekuja na data kuonyesha kwamba hakuna ISIS huko, kumbe umekuja na maswali ili kwamba wengine wakuhakikishie kuwa ni vinginevyo
Mimi ni mkristo lakini siamini kama hawa wahuni wana imani za dini ya kiisalamu...hawa wamekua infiltrated na CIA na washirika wao wafaransa kwakua kuna gesi hapo wanajaribu kutoiacha amani..waibe kiurahisi...ila dawa yao magufuri atawanyoosha
 
mimi ni mkristo lakini siamini kama hawa wahuni wana imani za dini ya kiisalamu...hawa wamekua infiltrated na CIA na washirika wao wafaransa kwakua kuna gesi hapo wanajaribu kutoiacha amani..waibe kiurahisi...ila dawa yao magufuri atawanyoosha
Hakuna lolote, kila kitu tunasingizia mabeberu wakati wapiganaji tunawaona ni weusi kabisa
 
Habari za ISIS na mauwaji nchini Msumbiji zimesambaa sana na zimeanza kujadiliwa mpaka Umoja wa Mataifa.Bila kujali ukubwa wa taarifa hizo na umbali zilikofika tujaribu kuwa watulivu ili tujadiliane na tufikie pazuri kuepusha madhara zaidi.

Waislamu tuna maelekezo tunapofikiwa na taarifa ya jambo kabla hatujaanza kuchukua hatua za kushughulikia taarifa hizo
{ {يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنْ جَاءَكُمْ فَاسِقٌ بِنَبَإٍ فَتَبَيَّنُوا أَنْ تُصِيبُوا قَوْمًا بِجَهَالَةٍ فَتُصْبِحُوا عَلَى مَا فَعَلْتُمْ نَادِمِينَ} } [الحجرات 6]
Enyi mlioamini, kama fasiki akikujieni na habari yoyote msimkubalie tu, bali pelelezeni kwanza, msije mkawadhuru watu kwa ujahili na mkawa wenye kujuta juu ya yale mliyoyatenda}

Kutokana na ukubwa wa habari,madhara yanayotokea na zaidi yale yatakayofuatia ni muhimu kujadiliana kwa undani kuona kasoro ya hoja ya kuwepo kikundi cha ISIS nchini Msumbiji kinachosemekana kinauwa watu hovyo na kuwazidi nguvu majeshi ya nchi hiyo na pia wamewahi hata kuvuka mpaka na kuingia Tanzania kuuwa watu.

Hoja zangu za kufanya upembuzi zinaweza kuwa nyingi na ndefu lakini kwa ufupi tu ni kuwa kikundi hicho kinasemekana ni cha waislamu wenye msimamo mkali na kimekula kiapo kuwa chini ya ISIS wale tuliowahi kuwasikia nchini Iraq na maeneo mengi ya Mashariki ya kati na kaskazini mwa Afrika.

Kwa hivyo hawa ISIS wa Msumbiji ni kama tawi la ISIS ya kimataifa. Na kwa huku kusini mwa Afrika walianzia kuwa Alshabab halafu wakwa karibu na Aboud Rogo halafu wakavuka mpaka wakafika Kibiti na baadae kufika Cabo del Gado nchini Msumbiji ambako wamekuwa wengi na kupata nguvu pengine kuliko Alshabaab na Alqaeda.

1.Ikiwa picha ni hiyo,kiongozi wao ni nani na wapi ndio makao yao makuu wanakopeleka taarifa za utiifu na mafanikio ya mashambulio yao?

2.Wapi wanapata silaha na gharama za kuendesha harakati zao?

3.Eneo la Cabo ni misitu minene kama ya Kongo na mapango kama Afghanistan au ni tambarare na vichaka vya mikorosho vinavyofanana na maeneo ya Mtwara nchini Tanzania ?

4.Jeshi la Msumbiji limepata mafunzo wapi na silaha zao wanauziwa na nani kiasi kwamba hawafui dafu kwa vijana hao wa ISIS ambao baadhi ya watoa taarifa husema ni wahuni wanaotokana na vijana waliokosa ajira na wenye njaa.

5.Kwanini hao ISIS wanapouwa huwa hawapati upinzani kutoka kwa wanavijiji ambao kama hawana silaha za kijeshi basi wana silaha za jadi na watu wa makabila ya kimakonde ni maarufu kwa matumizi ya silaha za jadi wanapovamiwa.

6.Hao ISIS wa Msumbiji kama wapo hawaoni kwamba wanapoteza muda bure hilo lengo wanalohusishwa nalo eti kuanzisha dola ya kiislamu itakayokuwa na bendera ya rangi nyeusi,kwa sababu wenzao wote kuanzia Iraq,Ufaransa,Mali mpaka Somalia hakuna walipofanikiwa.Ni wapambanaji gani wajinga hao watakaokuwa kila siku hawabadili mbinu za kivita hata wanaposhindwa.

7. Kama ni kikundi cha waislamu kweli mbona wanafanya kinyume na Uislamu na tofauti sana na wale wanaodaiwa ni wenzao wa nchi nyengine. Mbona wao wamekuwa ovyo sana katika mapambano yao wanauwa tu hata hawajachokozwa.Wana tatizo gani na ndugu zao na majirani zao.

Maswali yote hayo hapo juu majibu yake yanaweza kutoa majibu kuwa kikundi cha ISIS cha Msumbiji na yale yanayotajwa kutendwa nao ni vitu hewa na haviingii akilini kwa watu wenye nia thabiti ya kujua ukiondoa wale wanaoshabikia kwa ujinga na chuki zao.

View attachment 1624211
POROJO TAKATAKA
 
Hivi mtoa mada unawatetea ISIS au waislam au hao magaidi wa mozambique?
maana wote ni kitu kimoja

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi nakataa kuwepo ISIS Msumbiji na natetea Uislamu kutohusika na ukatili wa aina yoyote kwa sababu mafunzo ya kiislamu daima ni amani na napinga magaidi wa aina zote wawe wa kikristo au namna nyengine.
 
na napinga magaidi wa aina zote wawe wa kikristo au namna nyingine.
Cha muhimu nii hiki tu zingine ni propaganda.....maana watu wanajiita waislam na wanafata mafundisho ya kiislam wewe unakataa sio waislam siyo mbaya...ni vizuri kuwapinga lakini pia kupotosha sio dili labda useme ni waislam waliokengeuka
 
Cha muhimu nii hiki tu zingine ni propaganda.....maana watu wanajiita waislam na wanafata mafundisho ya kiislam wewe unakataa sio waislam siyo mbaya...ni vizuri kuwapinga lakini pia kupotosha sio dili labda useme ni waislam waliokengeuka



Sent using Jamii Forums mobile app

The full extent of US co-operation with Turkey, Saudi Arabia and Qatar in assisting the rebel opposition in Syria has yet to come to light. The Obama administration has never publicly admitted to its role in creating what the CIA calls a ‘rat line’, a back channel highway into Syria. The rat line, authorised in early 2012, was used to funnel weapons and ammunition from Libya via southern Turkey and across the Syrian border to the opposition. Many of those in Syria who ultimately received the weapons were jihadists, some of them affiliated with al-Qaida.

By the terms of the agreement, funding came from Turkey, as well as Saudi Arabia and Qatar; the CIA, with the support of MI6, was responsible for getting arms from Gaddafi’s arsenals into Syria. A number of front companies were set up in Libya, some under the cover of Australian entities. Retired American soldiers, who didn’t always know who was really employing them, were hired to manage procurement and shipping. The operation was run by David Petraeus, the CIA director who would soon resign when it became known he was having an affair with his biographer. (A spokesperson for Petraeus denied the operation ever took place.)
 
The full extent of US co-operation with Turkey, Saudi Arabia and Qatar in assisting the rebel opposition in Syria has yet to come to light. The Obama administration has never publicly admitted to its role in creating what the CIA calls a ‘rat line’, a back channel highway into Syria. The rat line, authorised in early 2012, was used to funnel weapons and ammunition from Libya via southern Turkey and across the Syrian border to the opposition. Many of those in Syria who ultimately received the weapons were jihadists, some of them affiliated with al-Qaida. By the terms of the agreement, funding came from Turkey, as well as Saudi Arabia and Qatar; the CIA, with the support of MI6, was responsible for getting arms from Gaddafi’s arsenals into Syria. A number of front companies were set up in Libya, some under the cover of Australian entities. Retired American soldiers, who didn’t always know who was really employing them, were hired to manage procurement and shipping. The operation was run by David Petraeus, the CIA director who would soon resign when it became known he was having an affair with his biographer. (A spokesperson for Petraeus denied the operation ever took place.)
umeandika nini hiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
 
Back
Top Bottom