zwangandaba
JF-Expert Member
- Jan 31, 2023
- 750
- 1,426
Swalama wakuu!
Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika SADC inajiandaa kuondoa kikosi chake lilichoko Msumbiji kusaidia serikali kupambana na magaidi wa kiislaam ifikapo July 15 2024 baada ya kuwa huko tangu 2018 mwishoni.
Kikosi hicho kijulikanacho kama SAMIM chenye jumla ya wapiganaji 1900 kimekuwa huko kwa lengo la kupambana na magaidi, kujenga uwezo kwa majeshi ya serikali lakini pia kuongeza wigo wa misaada ya kiutu kwa raia.
Wakati SADC wakijikusanya mdogomdogo kukusanya vikosi, rais wa Msumbiji Phelipe Nyusi mwaka 2020 alifanya ziara Rwanda na kukutana na rais Kagame na kuomba msaada wa kijeshi.
Mwaka 2021 Rwanda ilipeleka askari 1000 na ndani ya miezi 3 walifaniliwa kuiteka moja ya ngome ya waasi na kukomboa miji kadhaa kutoka milononi mwa magaidi.
Jambo la kushangaza wakati SADC wanaondoa majeshi yake kutokana na ukata, Rwanda mpaka sasa imeendelea kuongeza askari kifikia 2500 nchini Msumbiji kulinganisha na 1900 wa SADC wanaotarajiwa kuondoka ili hali bado hali ya usalama haijatengemaa kwenye maeneo wanayo yaacha kwa vikosi vya serilali
Ajabu nyingine:
Wakati SADC wakitegemea michango ya AU, China na wafadhili mbalimbali, mpaka muda huu hakuna ajuaye ni nani anagharamia oparesheni za majeshi ya Rwanda yanayo onekena kuwa na vifaa bora na vya kisasa kulinganisha na kikosi cha SAMIM kinachoundwa na askari 1900, askari 1400 wakitoka Afrika ya kusini na wengine kutoka nchi za Botwana, Angola, Malawi, Tanzania na Namibia.
Majeshi ya Rwnda yamejikita maeneo ya Acube, Montepuez na pemba kutokana na maeneo hayo kuwa shuguli za madini ya graphite na gemstones pamoja na Carbo delgado eneo lenye shughuli za uchimbaji wa mafuta pamoja na mkoa wa Palma wenye utajiri wa madini mbalimbali.
Wadadisi wanadai huenda Wanyarwanda wameahidiwa kupewa mafuta na madini kama malipo ya kazi.Raisi Nyusi ametembelea Rwanda mara nyingi kuliko nchi yeyote ya SADC. Na katika moja ya ziara Nyusi alipewa na Kagame zawadi ya shamba pamoja na ng'gombe wenye pembe kubwa.
Ukaribu usio wa kawaida kati ya maraisi hawa na operation za kijeshi zinazotekelezwa bila ya kuwapo uwazi anaegharamia oparesheni za kijeshi kwa vikosi vya Rwanda nchini Msumbiji
Pia hali ya Rwanda kujikita kimkakati na kiufanisi maeneo yenye utajiri wa madini unaleta jibu kuwa huenda wanapigania kwa moyo kile walicho kubaliana kati ya Nyusi na Kagame
Wachambuzi wa masuala ya kiusalama barani Afrika pia wanafananisha hali ya DR Congo ambako SAMDRC ina pambana na waassi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda.
Ni katika hali kama hiyo, majeshi ya waasi wa m23 yameonekana kutumia silaha bora kuliko za SADC na hata mafanikio ya kikosi cha SADC nchini DRC bado ni madogo kulingana na maadui wao.
Wakati kikosi cha SADC kinagharamiwa na UN, M23 na Rwanda haijulikani nani anawafadhili kwa kiwango kikubwa kiasi hiki kuwa na uwezo wa kukabiliana na kuwapa changamoto majeshi ya SADC.
Kwa mantiki hiyo, utaona kuwa Rwanda huwa hana masihala na eneo lolote barani Afrika ilimradi pawe na raslimali.
Pia kwa kuangalia tu mifano ya nyendo za oparesheni za kijeshi za nchi ya Rwanda nchini Msumbiji na DRC , mwenye akili anapata jibu kuwa kuna wenye nguvu wako nyuma ya nchi hii ndogo ya Afrika Mashariki.
Kwa mantiki hii, huenda amani DRC isipatikane kwa njia ya vita bali mazungumzio juu ya meza.
Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika SADC inajiandaa kuondoa kikosi chake lilichoko Msumbiji kusaidia serikali kupambana na magaidi wa kiislaam ifikapo July 15 2024 baada ya kuwa huko tangu 2018 mwishoni.
Kikosi hicho kijulikanacho kama SAMIM chenye jumla ya wapiganaji 1900 kimekuwa huko kwa lengo la kupambana na magaidi, kujenga uwezo kwa majeshi ya serikali lakini pia kuongeza wigo wa misaada ya kiutu kwa raia.
Wakati SADC wakijikusanya mdogomdogo kukusanya vikosi, rais wa Msumbiji Phelipe Nyusi mwaka 2020 alifanya ziara Rwanda na kukutana na rais Kagame na kuomba msaada wa kijeshi.
Mwaka 2021 Rwanda ilipeleka askari 1000 na ndani ya miezi 3 walifaniliwa kuiteka moja ya ngome ya waasi na kukomboa miji kadhaa kutoka milononi mwa magaidi.
Jambo la kushangaza wakati SADC wanaondoa majeshi yake kutokana na ukata, Rwanda mpaka sasa imeendelea kuongeza askari kifikia 2500 nchini Msumbiji kulinganisha na 1900 wa SADC wanaotarajiwa kuondoka ili hali bado hali ya usalama haijatengemaa kwenye maeneo wanayo yaacha kwa vikosi vya serilali
Ajabu nyingine:
Wakati SADC wakitegemea michango ya AU, China na wafadhili mbalimbali, mpaka muda huu hakuna ajuaye ni nani anagharamia oparesheni za majeshi ya Rwanda yanayo onekena kuwa na vifaa bora na vya kisasa kulinganisha na kikosi cha SAMIM kinachoundwa na askari 1900, askari 1400 wakitoka Afrika ya kusini na wengine kutoka nchi za Botwana, Angola, Malawi, Tanzania na Namibia.
Majeshi ya Rwnda yamejikita maeneo ya Acube, Montepuez na pemba kutokana na maeneo hayo kuwa shuguli za madini ya graphite na gemstones pamoja na Carbo delgado eneo lenye shughuli za uchimbaji wa mafuta pamoja na mkoa wa Palma wenye utajiri wa madini mbalimbali.
Wadadisi wanadai huenda Wanyarwanda wameahidiwa kupewa mafuta na madini kama malipo ya kazi.Raisi Nyusi ametembelea Rwanda mara nyingi kuliko nchi yeyote ya SADC. Na katika moja ya ziara Nyusi alipewa na Kagame zawadi ya shamba pamoja na ng'gombe wenye pembe kubwa.
Ukaribu usio wa kawaida kati ya maraisi hawa na operation za kijeshi zinazotekelezwa bila ya kuwapo uwazi anaegharamia oparesheni za kijeshi kwa vikosi vya Rwanda nchini Msumbiji
Pia hali ya Rwanda kujikita kimkakati na kiufanisi maeneo yenye utajiri wa madini unaleta jibu kuwa huenda wanapigania kwa moyo kile walicho kubaliana kati ya Nyusi na Kagame
Wachambuzi wa masuala ya kiusalama barani Afrika pia wanafananisha hali ya DR Congo ambako SAMDRC ina pambana na waassi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda.
Ni katika hali kama hiyo, majeshi ya waasi wa m23 yameonekana kutumia silaha bora kuliko za SADC na hata mafanikio ya kikosi cha SADC nchini DRC bado ni madogo kulingana na maadui wao.
Wakati kikosi cha SADC kinagharamiwa na UN, M23 na Rwanda haijulikani nani anawafadhili kwa kiwango kikubwa kiasi hiki kuwa na uwezo wa kukabiliana na kuwapa changamoto majeshi ya SADC.
Kwa mantiki hiyo, utaona kuwa Rwanda huwa hana masihala na eneo lolote barani Afrika ilimradi pawe na raslimali.
Pia kwa kuangalia tu mifano ya nyendo za oparesheni za kijeshi za nchi ya Rwanda nchini Msumbiji na DRC , mwenye akili anapata jibu kuwa kuna wenye nguvu wako nyuma ya nchi hii ndogo ya Afrika Mashariki.
Kwa mantiki hii, huenda amani DRC isipatikane kwa njia ya vita bali mazungumzio juu ya meza.
warfare. Ndio maana hata kimajukumu Tanzania ndio inayo hold zaidi jungle to jungle battle, pia hapo hapo ktk SAMIDRC hawapigani pamoja Kila mtu anapewa majukumu yake hivyo ukinzani wanao kutana nao M23 Kwa Tanzania hata wewe unapokea habari zake pia najua unajua south hawafanyi operation za aina hiyo wao haswa ni air attack. Halipingwi hili.