Msukuma: Serikali ihalalishe Bangi na Mirungi

Msukuma: Serikali ihalalishe Bangi na Mirungi

Nafikir msukuma, hajafaham jambo moja kuwa uchizi si lazima uvue nguo hata kuongea mambo yasiyostaili kwa watu wenye akili nao ni uchizi, msukuma umeitia aibu geita na wasukuma, hivi unataka kutuambia kuwa watu wanapolima wanavuta bangi??

Kiukwel najisikia aib kujitambulisha maana umelitia doa bunge, et nawe ni mbunge, aseee kapimwe akili huenda nawe ulipitia huko..
 
mi namuunga mkono msukuma. kigwangala arudi shule, hata pombe inasababisha alcohol induced psychosis, kansa ya koo, tumbo na ini kuharibika. bangi inababisha ukichaa kwa watu susceptible tu. tatizo huwa kwa watu na siyo ganja.
 
msukuma anatafuta kik kwenye media kwel umaarufu mtaji
 
Baada ya mjadala wa juzi juzi bungeni juu ya matumizi ya "Bangi na mirungi" ulioibuliwa na Mbunge wa Geita Vijiini Joseph Kasheku Musukuma, nilimtafuta daktari Chriss Cyrilo (MD) aeleze kama bangi ina faida kama alivyosema Msukuma au ina hasara. Na haya ndio maelezo ya daktari.
____________________________________

FAIDA 11 ZA KIAFYA ZA MATUMIZI YA BANGI (MARIJUANA).

Na Dr.Christopher Cyrilo (MD)

UTANGULIZI;

Katika baadhi ya nchi Duniani, matumizi ya bangi yamehalalishwa kuzingatia utashi wa mamlaka za nchi husika. Uruguy na Marekani (katika majimbo 20) ni mifano ya nchi hizo. Tafiti mbalimbali za kiafya zimefanyika na kupelekea ugunduzi kuwa bangi huweza kutumika kama tiba kwa baadhi ya magonjwa, isipokuwa haipaswi kutumika ovyo kama ilivyo kwa dawa zingine.

Zifuatazo ni faida 11 za kiafya za bangi. Kisha tutaeleza na athari hasi za bangi hapo baadae.

1. Inaweza kutumika kukinga na kutibu presha ya jicho (glaucoma), bangi inapunguza presha ya jicho (intraocular pressure) kwa watu wenye presha ya kawaida na hata wale ambao presha ya jicho iko juu( glaucoma).

2. Inaweza kuboresha afya ya mapafu na kupunguza athari za tumbaku katika mapafu. Januari 2012, tafiti zilionesha bangi haiathiri kazi za mapafu badala yake huongeza ufanisi wa mapafu.

3. Huweza kuzuia kifafa. Kemikali aina ya "Tetrahydrocannabinol" au "THC" iliyopo katika bangi huambatana na seli za ubongo zinazochochea umeme katika mfumo wa fahamu. Muambatano huo hupunguza msisimko (excitability) wa mfumo wa fahamu na kuzuia kutokea kwa kifafa.

4. Kuzuia kuenea kwa baadhi ya kansa, "Cannabidiol au CBD" ni kemikali iliyopo kwenye bangi ambayo hupunguza kuenea kwa kansa mwilini. Mfano, kansa ya matiti.

5. Inapunguza wasiwasi, maumivu na kichefuchefu, hata hivyo ikitumiwa kwa kiasi kikubwa huweza kuongeza wasiwasi.

6. Hupunguza na kutibu matatizo ya kutetemeka kwa misuli, (Parkinsonism)

7. Bangi huweza kutibu magonjwa ya utumbo (Inflammatory bowel diseases). Mwaka 2010 katika chuo cha Nottingham, tafiti ziligundua kuwa kemikali zilizopo kwenye bangi husaidiana na seli za mwilini kuongeza kinga za mwili na ufanisi wa utumbo.

8. Kupunguza maumivu ya viungo. Bangi hupunguza maumivu, hupunguza miwasho na kuleta usingizi.

9. Huboresha ngozi na kuchangamsha kazi za mwilini, Pia huongeza matumizi ya sukari mwilini.

10. Huongeza uwezo wa kubuni vitu (creativity), uwezo wa kukumbuka na uwezo wa kuzungumza.

11. Huweza kusaidia watu wanaopata matatizo ya mfadhaiko kutokana na kumbukumbu za mambo ya kutisha (post traumatic stress disorder) Mfano, Kwa wahanga wa majanga ya asili na yale yasio ya asili kama vita, moto, tsunami nk. Watu hao hupata kuona upya matukio ya kutisha walioshuhudia zamani na huweza pia kuyaona katika ndoto. Bangi huweza kuwasaidia kuepuka tatizo hilo. Maveterani wa vita ni mfano mzuri kabisa.

ANGALIZO. Matumizi ya kiafya ya bangi yanapaswa kuwa chini ya maelekezo ya daktari au mtaalamu wa afya, kwa sababu athari zake hutegemea kiasi cha matumizi na hali ya afya ya mtumiaji. Inaaminika kuwa Bangi ina athari chache kulinganisha na pombe.

Dr.Chriss Cyrilo (MD).
Asante.
 
Jamani inategemea mtu na mtu na kijiti na kijiti kinyonga(chameleon)alizoea ya kamp kaja kukutana na gampera ya A town akajihisi anaweza kuwa kama mike air Jordan acha atoke penye balcony mpaka chini wakazuga alikuwa anaota.
 
Bangi haina tatizo, matatizo wanayo watu wenyewe. Maana kuna wengine hata wakinywa bia mbili huwa ni kituko balaa, hapa malimbe kuna mzee aliniambia alianza kuvuta bangi mwaka 1986 mpka leo anaendelea na yuko sawa kabsa na home kwake maendeleo yapo.
 
hao ndio maadui wa lowasa na akili zao
 
BANGI! BANGI! Ngoja namimi niseme kitu. Mwaka 2008 nlivyo kuwa form three nlijaribu kuvuta bangi ya kutoka Malawi, hiyo bangi nilipewa na mzee mmoja maarufu sana mitaa ya Itunge, Kyela Mjini.
Alisema 'mimi tangu nianze kuvuta bangi sijaona madhara yake ni miaka zaidi ya 25 sasa navuta na nafanya kazi zangu vyema kabsa'. Alivyosokota moja alivuta kisha akanipasia na mimi, nikaivuta akanambia endelea kuvuta.
Baada ya dakika chache nikawa kama nina kizunguzungu kizito sana. Akanichukua na kunilaza nlilala mpaka kesho yake mchana (kutoka saa 11jion-8mchana). Nlivyo amka nikamuliza mzee kimetokea nin? ......alicheka sana, na kunambia 'wewe kichwa chako kibovu, usivute tena bangi anaweza kuchanganikiwa'. Na akaongeza kuwa BANGI inawatu wake na vichwa vyake...huku akinipa vijana ambao wameweuka kwa kuvuta BANGIQ
Pia, alisema 'ukiwa unawaza mawazo hatari/mabaya usivute bangi maana ambacho utatenda baada ya kupata stimu ni kile ambacho ulikiwa unafikir wakat ukivuta.
 
Herb heals the nation alcohol destroy it - Bob Marley
Nimeshangaa waziri anakataa bangi haina faida.... It induces appetite hasa kwa wagonjwa wa Kansa who are on chemotherapy which causes severe nausea and loss of appetite, inasaidia in epilepsy in some researches done though we still need more.... Wenzetu wanapambana Na kuifanya medical marijuana isaidie ye anapanda.... At least he could have said we need more research.... Nina my friend whom she had a parent with cancer Na hakuwa Na appetite nilimshauri atafute bangi wampikie Na mboga she had a good appetite after that...
 
Ila Kiukweli bange Ina madhara na inaleta ht uchizi kwa wengine,na inakufanya unakuwa kibri,au bwege kwa wengine, au mwingine akivuta anapenda kuchekacheka ht kwa jambo la kipuuzi, mi nilikuwa navuta wakati nna 25yrs, ,,kiukweli haifai hata kidogo, ila kuna wengine wakivuta inawachukua poa kabisa,,,,,mi nimevuta katika Mapito ya uvulana, nna ushaidi haifai ht kidogo,,,,,,faida zake ni chache kuliko madhara yake, NA MIRUNGI PIA INALETA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA SEVENTY PERCENT,,,,
 
sigara chanzo cha lug cancer na heart diseases,pombe ndo chanzo cha vifo vingi duniani achilia mbali ajali hata magonjwa ya kuambukiza kwa ukimwi pamoja na magonjwa yatokanayo tokana na utumiaji wapombe...mzungu mjanja sana leo mmarekani ana legalize taratibu bangi nakitu kashaifanyia reasearchmdamrefu ana pinga vikali matumizi ya sigara kwasababu sisi niwajinga tunapinga tu..!! mmea ulioteshwa na Mkuu wa hii dunia unapataje mamlaka ya kuuita haram??
 
Kumbe jamii forums kuna wavuta bhangi wengi hivi?sasa nimepata majibu ya maswali mengi niliyokuwa najiuliza kuhusu members wa jamii forums
 
Ila Kiukweli bange Ina madhara na inaleta ht uchizi kwa wengine,na inakufanya unakuwa kibri,au bwege kwa wengine, au mwingine akivuta anapenda kuchekacheka ht kwa jambo la kipuuzi, mi nilikuwa navuta wakati nna 25yrs, ,,kiukweli haifai hata kidogo, ila kuna wengine wakivuta inawachukua poa kabisa,,,,,mi nimevuta katika Mapito ya uvulana, nna ushaidi haifai ht kidogo,,,,,,faida zake ni chache kuliko madhara yake, NA MIRUNGI PIA INALETA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA SEVENTY PERCENT,,,,

Wewe hauko peke yako,tatizo lenu akili zenu zimelalia kwenye uvutaji tu wa bangi.Wengi wanaopinga kuhalalishwa kawa bangi humu wamekazana kuzungumzia uvutaji tu,hii inatokana na ukosefu wa uelewa sahihi wa matumizi ya bangi na historia ya matumizi ya bangi bila kusahau sababu halisi iliyofanya bangi kuharamishwa.

Watu wengi wanadhani bangi imeharamishwa kutokana na madhara yanayotokana na uvutaji wake,hapa ndipo watu wanapokosa elimu sahihi.Fuatilia marijuana act ya mwaka 1937 iliyoanzishwa na serikali ya marekani na baadaye kuwa enforced UNO kama sheria ili itumike duniani kote kuharamisha bangi.Sheria ya kuharamisha bangi Tanzania haijatungwa na serikali ya Tanzania,Tanzania tumelazimishwa kuifuata tu.Pia wengi hawajui hata hiyo sheria inasemaje.

Nikupe mfano tu:Salimia ni dawa inayotumika kuchua misuli ili kupunguza maumivu,na imeandikwa 'for external use only',ukinywa salimia utakufa.Pia kisu hutumika kukatia matunda na vitu vingine,lakini ukimchoma mwenzako kisu tumboni waweza kumwua,kazi ya kisu si kuua.Mpaka hapo utakuwa umeelewa kwamba uharamu wa kitu hutegemea matumizi yake.

Sasa tunakuja kwenye matumizi sahihi na yenye faida ya bangi:
1.Bangi hutumika kutengenezea kamba ngumu zaidi ya katani,zilitumika kipindi cha zamani kwenye majahazi.Ulikuwa unajua hili?
2.Bangi ilitumika kutengenezea karatasi zenye ubora kuliko hizi za sasa.Ulikuwa unajua hili?
3.Bangi ilitumika kutengeneza bodi ngumu za magari na hata kuta za nyumba.Ulikuwa unajua hili?
4.Mchakato wa bangi unaweza kutengenezea/kuzalisha methanol na gesi ya kupikia.Ulikuwa unajua hili?
5.Bangi inarutubisha ardhi iliyochoka pale inapopandwa.Ulikuwa unajua hili?
6.Mafuta ya mbegu za bangi hutumika kama kipodozi cha asili cha ngozi na kuikinga ngozi dhidi ya mionzi ya jua.Ulikuwa unajua hili?

Sasa kuna matumizi mawili ambayo ndiyo yamefanya bangi iharamishwe.Matumizi haya ndiyo yanaifanya bangi iitwe mmea mtakatifu.
1.Bangi inaweza kuchakatwa na kutengeneza dawa ya cancer/saratani na magonjwa lukuki kama mchangia mmoja alivyobainisha humu.Kama ulikuwa hujui,hii hii sigara/tumbaku ambayo imehalalishwa,wakati inaposababisha madhara kwenye mapafu bangi inaweza kurudisha mapafu katika hali yake ya kawaida.Pia kama ulikuwa hujui,pale Ocean Road CI,kuna dawa za kuzuia kichefuchefu na kupunguza/kutuliza maumivu kwa wagonjwa wa cancer,dawa hizi zimetengenezwa kwa kutumia bangi,wanakuua kwa chemo na mionzi lakini wanakutuliza kwa bangi.Ulikuwa unajua hili?Hata mimi naweza kutengeneza dawa ya cancer kwa kutumia cannabis/bangi.Haya mambo sio ya kufikirika,ni uelewa tu,wengi hatuna uelewa ndio maana tunapinga hovyo.Soma/uliza utajua tu.

2.Ekari moja ya bangi huzalisha lita zaidi ya 1500 za diesel.Diesel inayotokana na bangi ina faida nyingi zaidi ya petroleum diesel.Hebu fikiria jinsi ambavyo tungeitumia bangi kuzalisha umeme na kuendesha mashine kubwa viwandani.Hatuna uelewa ndio maana tunapata shida.Hata mimi naweza kukutengezea cannabis biodisel na ukatumia kwenye generator yako.Jambo hili si la kufikirika,ni uelewa tu,ndio maana tunasema someni vitabu,na education is power lakini watu wanadharau na kupinga hovyo.Misaafu inasema,"watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa".

Engine za kwanza kabisa kutengenezwa na Henry Ford na Rudolf Diesel miaka ya 1890 ziliendeshwa kwa mafuta ya diesel yaliyotokana na bangi/cannabis/hemp.Soma/uliza utajua tu.

Sasa matumizi haya mawili ndio mwiba kwa wafanyabiashara wakubwa wa kimarekani ambao ndio walikuwa wameshikilia serikali kipindi kile cha miaka kuanzia 1910.Kina Rockefeller,Morgan,Carnegie na wengine wakalazimisha kuanzishwa kwa sheria hiyo ili kudhibiti mass production ya cannabis.

Ukitaka kujua kama kweli bangi inazalisha diesel kwa wingi,usipinge,badala yake usome/uulize.Ukitaka kujua kama kweli bangi inatibu cancer,usipinge,badala yake usome/uulize.

Huyu mbunge aliyeanzisha hoja hii yuko sahihi kabisa,lakini ameanzisha hoja hii wakati bado uelewa wake kuhusu bangi ni mdogo.Kama ningekuwa mimi basi watu wengi ule ndio ungekuwa muda wao kuelewa ukweli uliojificha kuhusu bangi.

Fahamu kwamba uhalali na uharamu wa kitu chochote kile hutegemea na matumizi yake.Natoa rai kwa wote mpende kosoma vitabu na vyanzo vingine ili tuondokane na ujinga na ushabiki usio na faida.
 
Wewe hauko peke yako,tatizo lenu akili zenu zimelalia kwenye uvutaji tu wa bangi.Wengi wanaopinga kuhalalishwa kawa bangi humu wamekazana kuzungumzia uvutaji tu,hii inatokana na ukosefu wa uelewa sahihi wa matumizi ya bangi na historia ya matumizi ya bangi bila kusahau sababu halisi iliyofanya bangi kuharamishwa.

Watu wengi wanadhani bangi imeharamishwa kutokana na madhara yanayotokana na uvutaji wake,hapa ndipo watu wanapokosa elimu sahihi.Fuatilia marijuana act ya mwaka 1937 iliyoanzishwa na serikali ya marekani na baadaye kuwa enforced UNO kama sheria ili itumike duniani kote kuharamisha bangi.Sheria ya kuharamisha bangi Tanzania haijatungwa na serikali ya Tanzania,Tanzania tumelazimishwa kuifuata tu.Pia wengi hawajui hata hiyo sheria inasemaje.

Nikupe mfano tu:Salimia ni dawa inayotumika kuchua misuli ili kupunguza maumivu,na imeandikwa 'for external use only',ukinywa salimia utakufa.Pia kisu hutumika kukatia matunda na vitu vingine,lakini ukimchoma mwenzako kisu tumboni waweza kumwua,kazi ya kisu si kuua.Mpaka hapo utakuwa umeelewa kwamba uharamu wa kitu hutegemea matumizi yake.

Sasa tunakuja kwenye matumizi sahihi na yenye faida ya bangi:
1.Bangi hutumika kutengenezea kamba ngumu zaidi ya katani,zilitumika kipindi cha zamani kwenye majahazi.Ulikuwa unajua hili?
2.Bangi ilitumika kutengenezea karatasi zenye ubora kuliko hizi za sasa.Ulikuwa unajua hili?
3.Bangi ilitumika kutengeneza bodi ngumu za magari na hata kuta za nyumba.Ulikuwa unajua hili?
4.Mchakato wa bangi unaweza kutengenezea/kuzalisha methanol na gesi ya kupikia.Ulikuwa unajua hili?
5.Bangi inarutubisha ardhi iliyochoka pale inapopandwa.Ulikuwa unajua hili?
6.Mafuta ya mbegu za bangi hutumika kama kipodozi cha asili cha ngozi na kuikinga ngozi dhidi ya mionzi ya jua.Ulikuwa unajua hili?

Sasa kuna matumizi mawili ambayo ndiyo yamefanya bangi iharamishwe.Matumizi haya ndiyo yanaifanya bangi iitwe mmea mtakatifu.
1.Bangi inaweza kuchakatwa na kutengeneza dawa ya cancer/saratani na magonjwa lukuki kama mchangia mmoja alivyobainisha humu.Kama ulikuwa hujui,hii hii sigara/tumbaku ambayo imehalalishwa,wakati inaposababisha madhara kwenye mapafu bangi inaweza kurudisha mapafu katika hali yake ya kawaida.Pia kama ulikuwa hujui,pale Ocean Road CI,kuna dawa za kuzuia kichefuchefu na kupunguza/kutuliza maumivu kwa wagonjwa wa cancer,dawa hizi zimetengenezwa kwa kutumia bangi,wanakuua kwa chemo na mionzi lakini wanakutuliza kwa bangi.Ulikuwa unajua hili?Hata mimi naweza kutengeneza dawa ya cancer kwa kutumia cannabis/bangi.Haya mambo sio ya kufikirika,ni uelewa tu,wengi hatuna uelewa ndio maana tunapinga hovyo.Soma/uliza utajua tu.

2.Ekari moja ya bangi huzalisha lita zaidi ya 1500 za diesel.Diesel inayotokana na bangi ina faida nyingi zaidi ya petroleum diesel.Hebu fikiria jinsi ambavyo tungeitumia bangi kuzalisha umeme na kuendesha mashine kubwa viwandani.Hatuna uelewa ndio maana tunapata shida.Hata mimi naweza kukutengezea cannabis biodisel na ukatumia kwenye generator yako.Jambo hili si la kufikirika,ni uelewa tu,ndio maana tunasema someni vitabu,na education is power lakini watu wanadharau na kupinga hovyo.Misaafu inasema,"watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa".

Engine za kwanza kabisa kutengenezwa na Henry Ford na Rudolf Diesel miaka ya 1890 ziliendeshwa kwa mafuta ya diesel yaliyotokana na bangi/cannabis/hemp.Soma/uliza utajua tu.

Sasa matumizi haya mawili ndio mwiba kwa wafanyabiashara wakubwa wa kimarekani ambao ndio walikuwa wameshikilia serikali kipindi kile cha miaka kuanzia 1910.Kina Rockefeller,Morgan,Carnegie na wengine wakalazimisha kuanzishwa kwa sheria hiyo ili kudhibiti mass production ya cannabis.

Ukitaka kujua kama kweli bangi inazalisha diesel kwa wingi,usipinge,badala yake usome/uulize.Ukitaka kujua kama kweli bangi inatibu cancer,usipinge,badala yake usome/uulize.

Huyu mbunge aliyeanzisha hoja hii yuko sahihi kabisa,lakini ameanzisha hoja hii wakati bado uelewa wake kuhusu bangi ni mdogo.Kama ningekuwa mimi basi watu wengi ule ndio ungekuwa muda wao kuelewa ukweli uliojificha kuhusu bangi.

Fahamu kwamba uhalali na uharamu wa kitu chochote kile hutegemea na matumizi yake.Natoa rai kwa wote mpende kosoma vitabu na vyanzo vingine ili tuondokane na ujinga na ushabiki usio na faida.
Ahsante ndugu
 
Back
Top Bottom