"Msukule" wa Mapenzi...

Bebii pamoja na kwamba hii thread imenigusa ila nashukuru umenifanya nicheke lol, ukiona unamchukia hivyo ujue bado unampenda sana tu samahani kwa hili, ila siku upendo ulionao kwake ukikutoka utashangaa humchukii wala nini utakua unamuona wa kawaida tu..

tunafurahi sana kuona kwamba hata kama sisi mods hatupo around, vijana mnajadili mada bila mikwaruzano wala kuenda offu topik, hii imenipa moyo sana na nitashauriana na mods wenzangu tuanzishe JF nyengine zikuwepo 2. Hivyo basi Kwa niaba wa ya waifu (ambae juzi kwa bahati mbaya ameibiwa handbag yake), na kwa niaba ya jirani yangu (ambae alipima ukimwi juzi akaonekana anao), na kwa niaba ya mwajiri wangu (ambae anavuta bangi kabla breakfast) napenda kuchukua nafasi hii kuwashkuru nyote. Mbarikiwe sana

bek to topik: muda hautoshi kucomment.

nawahi press conference
mwajiri wak yupi anavuta bangi jf? najitoa mi na bangi tofauti nieleweshe
 
Yaani we acha tu, Mbu baba leo umeamkia wapi? yaani hii thread lol kama alivyosema the boss kwamba anadhani ashakua msukule bora ye anadhani mi ndio nishakua msukule kabisaaaaaaaaaa yaani mtu anakuacha kwa mbwembwe zisizo mfano halafu mambo yakienda ndivyo sivyo huko anaanza usumbufu, kibaya kama mmeshazaa ndio kizaa zaa kinaanzia hapo.

1. Mmama anatishia mtoto anaumwa n.k kumsumbua baba
2. Baba nae anatishia kukunyang'anya mtoto kisa unajifanya uko busy so hata mtoto wake huwezi pata muda wa kumwangalia.

Ngoja niishie tu hapa ila inauma sana sana sana kama yamekukuta, kwa kifupi niko natumika kama mzukule sasa na bado sijajua nitajinasua vipi.

kwa kweli inakera sana asee.


Maty naona tuna bahati saaana ya kukutana kwenye hii topic ya kutonesha....lol...
 
..

...leo tujadiliane hii kitu emotional rollercoaster. Pale mwenza wako (Psychological Abuser) anavyoutumia udhaifu wako. "Sleeping with the Enemy" ni sinema mojawapo inayotoa mfano mzuri wa hili.

Tujadiliane Ex- wife/husband/partner anapoendesha hisia zako atakavyo; -Swahili Slang- 'kuwekwa kidoleni,' 'kushikwa pembe,' 'kuwekwa mkononi,' etc na athari zake, kwa muda mfupi na muda mrefu.

Mbu ..Thanks a lot kwa hii mada. Kumbuka mada zako huwa zinatuumiza sana vichwa kwani zinalenga maisha halisi..

Mkuu..kuna kitu bado kinanisumbua..yaani maujanja yangu yote bado sijakubaliana na maana halisi ya mapenzi. Labda ni mshamba, au labda sijawahi kupenda au akili yangu bado imekumbatia maana ya mapenzi kuwa ni Myth. Yaani hakuna kitu kinaitwa mapenzi..au maana ya mapenzi inabadilika daima kama kinyonga...

Ninaposema mapenzi ni mysterious thing ni kwamba mambo yote yanayohusu mahusiano yanaendana na mazingira, feelings, wakati, umri, uchumi, dhiki, uchungu, furaha etc..

Kuna njia nyingi unaweza kuwa msukule wa mapenzi bila kujijua..na wakati ukiwa katika status hii ambayo inamahusiano na vitu nilivyotaja hapo juu..Yule mshiriki wa pili mara nyingi "EX" ana uwezo wa kushika remote control na kukuchezea atakavyo.. ni kwa sababu gani? hizi hapa..

First decision is always right! ..Ukitafakari sana huu usemi una ukweli..na katika mpenzi ni vigumu kumsahau mpenzi wako uliyemkabidhi moyo wako kwa mara ya kwanza..unahitaji kujenga mazingira kukwepa kishawishi cha kutosumbuliwa .. EX" akijua au kuona dalili toka kwako kuwa First decision or choice is always right! atakuchezea kwa remote control bila wewe kujijua..

Upendo wa kweli kwa watoto na uchungu wa mwana..Yaani ukitengana na mke/rafiki/mume mliopata na nae watoto ..msukule na jinamizi la watoto litakuandama.. ni uchungu wa mwana na wala sio wewe..na wala sio msukule..Utafanya chochote kile bila kujijua

Faith..tamaduni..mila .. etc... Mwenza wako anakudhalilisha ..anakupiga..lakini wazee, wachungaji na jamii inakupa moyo.."ndoa ni uvumilivu" zidisha maombi..yaani utabaki msukule..hadi maombi yako yawe ya kweli..

Uchumi na kukosa kujiamini..yaani ukifikiri kitachofuata ukitoka kwenye mahusiano kina kuacha hoi...utabaki unaogopa..na utakubali kukumbatia msukule bila kujijua....Hii ni moja ya weakness za binadamu ambazo ni`kuogopa changes au kuogopa ku-take risk!

Thanks again bro, Nawakilisha hayo....
 
Sina cha kuongeza ni ugonjwa huu omba usikukute unakataa dawa nyingi tu, wakati mwingine hupati dawa kabisa
 
Ndo maana namuambie VOR kuwa hapo ni kuwa hajajijua kuw anatumiwa haijalishi hata kama mapenzi au mlianchana bila kupenda kwenu kile kitendo cha wewe kuwa mtumwa wa kile anachokitaka tayari ni msukule

Mkuu hapa hakuna mtu anayekushikia Bunduki..., matakwa yake unayo haki ya kuyakataa na kuyapinga..., kutokuyakataa kwako inamaanisha yafuatayo:-
  • Unapenda hivyo anavyokusumbua na mwisho wa siku labda upo radhi mrudiane
  • Ni Bughuza anakusumbua na hapa una kila haki ya kutokupokea simu zake au akikuita wewe kukataa
  • Wewe ni mtu wa huruma na kila anapopata shida upo tayari kumsaidia kwa kila kitu without crossing the line (tenda wema uende zako usingoje kurudishiwa)
Kwahiyo mkuu tutaona kwamba hakuna mtu ambae hajui kinachotokea lakini kwa njia moja ama nyingine anachukulia poa (labda tu kwa wale ambao hawapendi na hizi attention zinakuwa usumbufu kwao)

Kwa kumalizia ni kwamba kuachana sio kujenga uadui na mnabaki kuwa marafiki na rafiki wa kweli hatafanya kitu ambacho kinaweza kikabomoa kwako..., (hata kama ni attention seeker atakachofanya ni itakuwa ni kukupa signal lakini sio kupiga simu usiku wa manane akijua kwamba wewe mke wako yupo hapo) sababu in so doing huyu atakuwa ni mchawi ambae hana utu,
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mbu amenikumbusha kitu........tatizo maswali yamekuwa mengi kuliko majibu.........labda niulize pamoja na usumbufu anaopokea vipi kuhusu hisia zake kwakwe bado anampenda?/au anahisi anamuonea huruma na si mapenzi yaliyomo ndani ya moyo wake.

naamini kuna watu wana ugonjwa wa kupenda sio wote ieleweke,kuna watu huwa wanakuja kwenye maisha yetu na huwa si rahisi kuwaondoa .......kwangu huwa nauita ugonjwa sijui kama niko sahihi kwa sababu hata mie ninao ..........mahusiano yatavunjika lakini upendo wangu hautafutika kwake hapo ndipo upande wa pili hutumia hiyo nafasi kucheza na wewe.

jingine ni ubinafsi tulioumbwa nao wanadamu hutaki kumuona akifurahi/kafanikiwa/kapendeza au ana mahusiano mengine kwake yeye ni kama ushindi.

...lol...Chauro, ndio huo ninaoita "ugonjwa" wa kujitakia!...kupenda usipopendwa.
Yaani pale unapompenda mtu, yeye anakufutia tope la miguu, anakupiga na chini kama pweza,
almuradi anakutoa thamani mpaka unajiona kweli hustahili kujipenda, kupendwa wala kumpenda yeyote.

Baada ya kujitoa kwake na kuanza maisha mapya, anakujia na usanii ambao ni pamoja na kukukumbushia
yote mazuri mliyopitia, i.e picha, matukio mbalimbali, nk...akiona hushtuki na hilo anakuja na gear ya kukupa sababu
umuonee huruma, kwani enzi hizo akipiga chafya tayari wewe mbio na viksi, maji moto, chai ya tangawizi, nk unambembeleza.

Akiona na hilo hushtuki nalo, anakupigia simu time zile anazojua utakuwa na Mpenzi/mume/mke wako mpya 'kukuonyesha' bado anauwezo ku control maisha yako... "msukule" wake!

 
Ohhh Nooooo!!! Nyamayao pole dada'ngu jamani...lohhh...
ila nawe kwanini unalala na simu-"On" wakati mumeo na watoto wapo hapo kando?
Unasubiri simu ya nani?

Kwanini hu mute hiyo simu kama wasiwasi wako unaweza kosa simu za ndugu?
Sikukusudia kukutibua Pole jamani, kunywa maji baridi utapoa...pole mydear.

cpo na watoto ndio sababu kubwa cm haziwezi kuwa off, na hata yeye hatakubali cm ziwe off kwa sasa coz ameshakuwa na kawacwac fulani, anahakikisha cm zote(zake/zangu) zipo on na mahali pa1, nikisema umenitibua ni kweli kabisa, bado kuna vuguvugu ya call ya juzi juzi, nipo kwenye wakati mgumu jamani.....
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mkuu hapa hakuna mtu anayekushikia Bunduki..., matakwa yake unayo haki ya kuyakataa na kuyapinga..., kutokuyakataa kwako inamaanisha yafuatayo:-
  • Unapenda hivyo anavyokusumbua na mwisho wa siku labda upo radhi mrudiane
  • Ni Bughuza anakusumbua na hapa una kila haki ya kutokupokea simu zake au akikuita wewe kukataa
  • Wewe ni mtu wa huruma na kila anapopata shida upo tayari kumsaidia kwa kila kitu without crossing the line (tenda wema uende zako usingoje kurudishiwa)
Kwahiyo mkuu tutaona kwamba hakuna mtu ambae hajui kinachotokea lakini kwa njia moja ama nyingine anachukulia poa (labda tu kwa wale ambao hawapendi na hizi attention zinakuwa usumbufu kwao)

Kwa kumalizia ni kwamba kuachana sio kujenga uadui na mnabaki kuwa marafiki na rafiki wa kweli hatafanya kitu ambacho kinaweza kikabomoa kwako..., (hata kama ni attention seeker atakachofanya ni itakuwa ni kukupa signal lakini sio kupiga simu usiku wa manane akijua kwamba wewe mke wako yupo hapo) sababu in so doing huyu atakuwa ni mchawi ambae hana utu,

With due respect i beg to differ with you hapo kwenye blue mkuu.
She knows exactly u haveyour own life. She knows exactly that you have a family and may be a new wife. She knows exactly kwamba muda wa usiku mara nyingi you will be with your family and with your wife. Kwa nini akupigie simu saa sita za usiku hata kama kuna matatizo yametokea. What will you do then kama ameona majambazi yanatembea kwenye dirisha lake. What will you do then kama unapigiwa simu usiku wa manane kuambiwa kuwa kuna mtu amemhurt moyo wake.
yeah hujashikiwa bunduki kukubali upokee simu zake but she is the person you know and she is not your enemy huwezi kukaitaa kupokea simu zake. Inakuwaje zinapokuwa kero sasa kutaka kukuharibia wewe na mwenza wako. Je umfanye adui yako kutopokea simu zake au uwe kila mara unareject call zake. And to your wife what will happen to her kila mara atakaposikia simu na unaireject will you raise an alarm to her kuwa kuna something fishy kinaendelea.

Sio uadui yes na wala hamjaachana kwa uadui but huoni yeye anajijengea mazingira ya wewe kumfanya adui na ukimuona sehem umkwepe kwa ajili ya usumbufu wake huo.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
cpo na watoto ndio sababu kubwa cm haziwezi kuwa off, na hata yeye hatakubali cm ziwe off kwa sasa coz ameshakuwa na kawacwac fulani, anahakikisha cm zote(zake/zangu) zipo on na mahali pa1, nikisema umenitibua ni kweli kabisa, bado kuna vuguvugu ya call ya juzi juzi, nipo kwenye wakati mgumu jamani.....

...pole sana dada'ngu wee...hebu jiliwaze na posts za Tulizo na VoR kwanza. Kuna kitu uta learn hawa waheshimiwa wawili wanavyoyatafakari na kuyakabili majanga haya.
 
Utumwa na utegemezi wa hisia!Unapompa mtu mamlaka ya kukuamulia ujisikieje ni hatari sana kwani wewe ni mtumwa kwake,akiwa na hasira roho juu,asipopokea simu unajistukia,ukimpigia sim asipocheka kwenye mazungumzo yenu inakuwa kazi,n.k....Kama yanakutokea hayo na mengine ya kufanana na hayo jua hayo sio mapenzi bali utumwa,Upendo wa kweli pale unapokuwa na maamuzi yako mwenyewe namna unavyotaka kujisikia,nje ya hapo ni matatizo!
Mkuu, hapo u spoke my past few weeks lyf, I was xactly as u described., was mor than mtumwa, it hurt me one day I called her two times n she ddn' pick up my call instead she ended, later when I called she picked t up n asked why she was cuttin my calls she said kwamba she just decided to as the way she decided to pick up that call. I was so so so hurt, i felt kudharauliwa n humiliated to th max coz of my feelings. I then asked 2 meet with her ili tuongee face2face, what she answered made me to find my way out thou it was nearly impossible. I decided to start my new life out of her n thanx God in few weeks I started to 4get her. Yday she called me n told me kwamba there was a deal concerning my career n when I asked her why she decided to give me that deal she said coz she cares for me and she'd love if I'll be doing the same. Now ts lyk amenitonesha kidonda kilichokuwa kinakaribia kupona. Its so painful when X brings back th gone memories.
 
cpo na watoto ndio sababu kubwa cm haziwezi kuwa off, na hata yeye hatakubali cm ziwe off kwa sasa coz ameshakuwa na kawacwac fulani, anahakikisha cm zote(zake/zangu) zipo on na mahali pa1, nikisema umenitibua ni kweli kabisa, bado kuna vuguvugu ya call ya juzi juzi, nipo kwenye wakati mgumu jamani.....
Pamoja na yoote mna matatizo ya kuaminiana,ni kazi kuishi kama mna tatizo hili tena kwenye mazingira haya!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
...lol...hilo la kutojijua unatumika au kutumiwa ndio "MSUKULE" wenyewe huo...inabidi mtu wa aina hii aombewe na kumwagiwa maji baridi sikioni!



...lahaula, Gaga hapo penye red unatugusa wengi...ila hizo feelings ni ngumu kuzielezea kama zina maanisha mazoea, huruma, au kumbukumbu,....lakini sio mapenzi. Kasheshe ni kumpata Mwenza ambaye nae atalielewa hilo.




...VoR,...umeiweka vizuri hii, hasa hapo penye red kiasi kwamba nimeukumbuka msemo wa "Screw Driver" -MwanajamiiOne.




...Maskini Maty, pole sana. Hatua ya kwanza tayari unaipitia sasa hiyo ya kukukera sana, ...kama alivyogusia AshaDii, time is a healer. Ni juu yako na ipo ndani ya uwezo wako ku disconnect hizo emotional attachments.

Kama ulivyogusia la mtoto, mkishazaa ni kasheshe. Hata akikunyang'ang'anya mtoto...ndio yale yale ya kupigiwa simu uende haraka, mtoto anaumwa...unamuacha kitandani mkeo/mumeo unakimbilia kwa Ex wako...kwani ukienda na mkeo/Mumeo, Ex-wako ananuna! Balaaa tupu!

Mbu we acha tu, saa nyingine akipiga namsikiliza namjibu tu ndio ndio mradi tu aridhike kwani sitaki kuanzisha uadui sasa binti yangu ameshakua mkubwa inaweza kumuathiri, na akiamua kumchukua sina pa kwenda kupinga kwani umri unaruhusu basi ndio hapo anapopatia kwa sababu anajua nampenda sana mtoto wangu and she is the only one i have sina mtoto mwingine masikini mie ndio ukimjibu hovyo tu anaanza naenda kumchukua nikae nae mwenyewe so inabidi nakua tu mpole, na hivi hayumo moyoni mwangu basi akishamaliza maongezi yake na mimi namsahau hapo hapo,

Halafu cha ajabu mtoto anakaa boarding ila huku mkoani ninakoishi sasa kila baada ya siku tatu simu ushaenda kumuona mtoto? jamani huyo mtoto anaonwa kila siku? Kaazi kweli kweli wandugu ila ukishakua mtu mzima kidogo ina unafuu
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Faith..tamaduni..mila .. etc... Mwenza wako anakudhalilisha ..anakupiga..lakini wazee, wachungaji na jamii inakupa moyo.."ndoa ni uvumilivu" zidisha maombi..yaani utabaki msukule..hadi maombi yako yawe ya kweli..

Uchumi na kukosa kujiamini..yaani ukifikiri kitachofuata ukitoka kwenye mahusiano kina kuacha hoi...utabaki unaogopa..na utakubali kukumbatia msukule bila kujijua....Hii ni moja ya weakness za binadamu ambazo ni`kuogopa changes au kuogopa ku-take risk!

Thanks again bro, Nawakilisha hayo....


Tulizo Mkuu kama kweli you don't know Mapenzi ni nini ni kwamba aidha you are in deep expected trouble OR ndio moja ya wale exceptions walojaliwa (thou rare) never to fall in love… Hata hivo nimependa saana your analysis… kuhusu USUKULE… Hii daima ni kwamba Yule ambae ni Msukule wa Mapenzi yeye anakua hajitambui/hajui kabisa hata kama mjanja vipi… na hii hutumika vibaya saaana na Ex's ambao ni abusers…

Hata hivo umelenga kwa Msukele alie bado na huyo mtu ambae anamuendesha which if fine, Ila tatizo saaana hua kama you have moved on kwa kua na mtu mwingine but emotionally stuck kwa huyo ex…. Issue ndio hapo….
 
Doh! Mbu maumivu yake tusome kwenye maandishi..........hapo sasa kupenda tusipopendwa kabla ya kugundua tulishapenda .........huwa tunahitaji kufanya nini kabla ya kupenda?maana wengine mioyo yetu ina viherehere sana.

Inawezekana kujali hisia za mtu usiyempenda?Najaribu kufikiria mengi Mbu usichoke maswali yangu.


...lol...Chauro, ndio huo ninaoita "ugonjwa" wa kujitakia!...
kupenda usipopendwa.
Yaani pale unapompenda mtu, yeye anakufutia tope la miguu, anakupiga na chini kama pweza,
almuradi anakutoa thamani mpaka unajiona kweli hustahili kujipenda, kupendwa wala kumpenda yeyote.

Baada ya kujitoa kwake na kuanza maisha mapya, anakujia na usanii ambao ni pamoja na kukukumbushia
yote mazuri mliyopitia, i.e picha, matukio mbalimbali, nk...akiona hushtuki na hilo anakuja na gear ya kukupa sababu
umuonee huruma, kwani enzi hizo akipiga chafya tayari wewe mbio na viksi, maji moto, chai ya tangawizi, nk unambembeleza.

Akiona na hilo hushtuki nalo, anakupigia simu time zile anazojua utakuwa na Mpenzi/mume/mke wako mpya 'kukuonyesha' bado anauwezo ku control maisha yako... "msukule" wake!

 
Yaliyopita, yamepita. Kwenye ugonjwa au kifo au shida yoyote, nitaenda kama binadamu mwingine, na si issue kwamba alikuwa X.
 
With due respect i beg to differ with you hapo kwenye blue mkuu.
She knows exactly u haveyour own life. She knows exactly that you have a family and may be a new wife. She knows exactly kwamba muda wa usiku mara nyingi you will be with your family and with your wife. Kwa nini akupigie simu saa sita za usiku hata kama kuna matatizo yametokea. What will you do then kama ameona majambazi yanatembea kwenye dirisha lake. What will you do then kama unapigiwa simu usiku wa manane kuambiwa kuwa kuna mtu amemhurt moyo wake.

Mkuu kuna watu sio considerate na wako selfish (yaani wenyewe wanajiangalia wenyewe na hawajali wenzao) sasa kama rafiki yako yupo hivi inabidi umuelewe, now mimi hata partner wangu akipigiwa simu kwamba EX wake ameingiliwa na majambazi sitakasirika, tena ndio nitatoa msaada wa kwenda kumsaidia sababu ndio ubinadamu; lakini kama anapiga simu anadanganya majambazi yamemuingilia wakati ni uongo basi huyo ni mchawi na huenda urafiki wetu ukaisha sababu hanitakii mema

yeah hujashikiwa bunduki kukubali upokee simu zake but she is the person you know and she is not your enemy huwezi kukaitaa kupokea simu zake. Inakuwaje zinapokuwa kero sasa kutaka kukuharibia wewe na mwenza wako. Je umfanye adui yako kutopokea simu zake au uwe kila mara unareject call zake. And to your wife what will happen to her kila mara atakaposikia simu na unaireject will you raise an alarm to her kuwa kuna something fishy kinaendelea.

Mkuu action zake zita-determine kama yeye ni rafiki au adui..!! kama ni kawaida yake kupiga simu usiku na kunisumbua bila sababu basi atanifanya niache kupokea simu zake, na kama huwa ananidanganya basi atanifanya niache kumuamini au kumsikiliza...., Mkuu "we are what we are" kama atachukulia urafiki wetu for granted huenda akanipoteza kabisa..., kama hatukuweza kuafikiana kama boyfriend/girlfriend na tukaachana unadhani itakuwa tabu kuacha kuafikiana kama marafiki ?, unajua kila relationship in price yake na kama mtu ata-abuse upole na consideration ya mtu na kumfanya kama mjinga maybe she/he does not deserve any attention na kwa kujenga nyumba yako vizuri inabidi umwambie na mwenza wako ili ajue.
 
Mi nakwambia sijuii Mbu leo amewaza nini kuja kututibua mashetani hapa, ninachoshukuru kwa upande wangu sina mapenzi nae kabisaaa namuona kama kaka yangu, kwa kweli kwa hili namshukuru Mungu. Ila ndio ningekua bado nampenda nahisi ningeteseka sana kwa kweli kwani ameshafanya kila aina ya mbinu, sasa amebaki kunitishia upuuzi tu hovyo kabisa.

...Nice one Maty,....keshatumia mbinu zote sasa ameamua 'kukutishia upuuzi'...lol...hivi mijitu ya aina hii wanafikiria nini vichwani mwao? yaani ukae unaogopa ogopa tu? ...huo sio utumwa wa mapenzi, ni kung'ang'ania "Msukule!"


Mkuu hapa hakuna mtu anayekushikia Bunduki..., matakwa yake unayo haki ya kuyakataa na kuyapinga..., kutokuyakataa kwako inamaanisha yafuatayo:-
  • Unapenda hivyo anavyokusumbua na mwisho wa siku labda upo radhi mrudiane
  • Ni Bughuza anakusumbua na hapa una kila haki ya kutokupokea simu zake au akikuita wewe kukataa
  • Wewe ni mtu wa huruma na kila anapopata shida upo tayari kumsaidia kwa kila kitu without crossing the line (tenda wema uende zako usingoje kurudishiwa)
Kwahiyo mkuu tutaona kwamba hakuna mtu ambae hajui kinachotokea lakini kwa njia moja ama nyingine anachukulia poa (labda tu kwa wale ambao hawapendi na hizi attention zinakuwa usumbufu kwao)

Kwa kumalizia ni kwamba kuachana sio kujenga uadui na mnabaki kuwa marafiki na rafiki wa kweli hatafanya kitu ambacho kinaweza kikabomoa kwako..., (hata kama ni attention seeker atakachofanya ni itakuwa ni kukupa signal lakini sio kupiga simu usiku wa manane akijua kwamba wewe mke wako yupo hapo) sababu in so doing huyu atakuwa ni mchawi ambae hana utu,

...kiukweli ndio hivyo, hasa hapo penye red. Lakini abusive relatinship mara nyingi zinaishia hivyo.
Kila unapojaribu kumsamehe abuser, yeye anautumia msamaha wako kwake kama mwanya au
upenyo wa yeye kujirudisha kwako..."msukule wake!"

With due respect i beg to differ with you hapo kwenye blue mkuu.
She knows exactly u haveyour own life. She knows exactly that you have a family and may be a new wife. She knows exactly kwamba muda wa usiku mara nyingi you will be with your family and with your wife. Kwa nini akupigie simu saa sita za usiku hata kama kuna matatizo yametokea. What will you do then kama ameona majambazi yanatembea kwenye dirisha lake. What will you do then kama unapigiwa simu usiku wa manane kuambiwa kuwa kuna mtu amemhurt moyo wake.
yeah hujashikiwa bunduki kukubali upokee simu zake but she is the person you know and she is not your enemy huwezi kukaitaa kupokea simu zake. Inakuwaje zinapokuwa kero sasa kutaka kukuharibia wewe na mwenza wako. Je umfanye adui yako kutopokea simu zake au uwe kila mara unareject call zake. And to your wife what will happen to her kila mara atakaposikia simu na unaireject will you raise an alarm to her kuwa kuna something fishy kinaendelea.

Sio uadui yes na wala hamjaachana kwa uadui but huoni yeye anajijengea mazingira ya wewe kumfanya adui na ukimuona sehem umkwepe kwa ajili ya usumbufu wake huo.

LOL, Mr Rocky you must have been there,...inputs zako zinaelezea hali halisi. Halafu kitu kibaya ni kwamba, jinsi anavyokuudhi nawe kuzidi kumchukia, ndivyo anavyoanza kukuganda tena kichwani....Pheewwww, what a miserable life!

Mkuu, hapo u spoke my past few weeks lyf, I was xactly as u described., was mor than mtumwa, it hurt me one day I called her two times n she ddn' pick up my call instead she ended, later when I called she picked t up n asked why she was cuttin my calls she said kwamba she just decided to as the way she decided to pick up that call. I was so so so hurt, i felt kudharauliwa n humiliated to th max coz of my feelings. I then asked 2 meet with her ili tuongee face2face, what she answered made me to find my way out thou it was nearly impossible. I decided to start my new life out of her n thanx God in few weeks I started to 4get her. Yday she called me n told me kwamba there was a deal concerning my career n when I asked her why she decided to give me that deal she said coz she cares for me and she'd love if I'll be doing the same. Now ts lyk amenitonesha kidonda kilichokuwa kinakaribia kupona. Its so painful when X brings back th gone memories.

Mbimbinho, kisa chako kinasikitisha, japo imenichukua muda mrefu ku decipher maneno uliyotumia.
Next time tumia maneno ya kawaida bana, sio sms...wengine sie ni wa mwaka 47.
Pole sana...ni hiari yako hapo kuchukuliwa "msukule" au la, bado una muda wa kuamua.
 
Mkuu kuna watu sio considerate na wako selfish (yaani wenyewe wanajiangalia wenyewe na hawajali wenzao) sasa kama rafiki yako yupo hivi inabidi umuelewe, now mimi hata partner wangu akipigiwa simu kwamba EX wake ameingiliwa na majambazi sitakasirika, tena ndio nitatoa msaada wa kwenda kumsaidia sababu ndio ubinadamu; lakini kama anapiga simu anadanganya majambazi yamemuingilia wakati ni uongo basi huyo ni mchawi na huenda urafiki wetu ukaisha sababu hanitakii mema



Mkuu action zake zita-determine kama yeye ni rafiki au adui..!! kama ni kawaida yake kupiga simu usiku na kunisumbua bila sababu basi atanifanya niache kupokea simu zake, na kama huwa ananidanganya basi atanifanya niache kumuamini au kumsikiliza...., Mkuu "we are what we are" kama atachukulia urafiki wetu for granted huenda akanipoteza kabisa..., kama hatukuweza kuafikiana kama boyfriend/girlfriend na tukaachana unadhani itakuwa tabu kuacha kuafikiana kama marafiki ?, unajua kila relationship in price yake na kama mtu ata-abuse upole na consideration ya mtu na kumfanya kama mjinga maybe she/he does not deserve any attention na kwa kujenga nyumba yako vizuri inabidi umwambie na mwenza wako ili ajue.


Friends with reason and hidden agenda always. Be careful sana mkuu maana we have friends but hatujui ndani ya mind zao wanawaza nini kwa ajili yetu au wanatuwazia nini kama ni mema au mabaya hatujui. Always hizo agenda zao za siri huwa wanazificha hawazionyeshi hata ukikutana nae umuulize what is in your mind hawezi kukupa jibu la nini anachokuwazia ila ndani mwake ana dirty mind. So be careful mkuu.




Hapo mkuu naweza kukuelewa. Na umeenda exactly kule nilikokuwa nakutaka. Marafiki wanauchukulia urafiki for granted na wanatake advantage kuwa unawasikiliza na wanataka pia wakutawale usiwe na maamuzi. For a lady akishajua madhaifu yako ndilo atakuwa anafanya kukuweka roho juu kila mara na kukutafuta wewe kuwa kitulizo chake wakati ana matatizo badala ya hata kumtafuta mwenza wake.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu

LOL, Mr Rocky you must have been there,...inputs zako zinaelezea hali halisi. Halafu kitu kibaya ni kwamba, jinsi anavyokuudhi nawe kuzidi kumchukia, ndivyo anavyoanza kukuganda tena kichwani....Pheewwww, what a miserable life!



Mbu hapo anakuwa kashakujua na you know anakujua udhaifu wako na wewe ulivyo so anatake advantage ya wewe kuwa vile ili azidi kukutumia na with time na unavyozidi kukasirika anajua tuu hutoacha kupokea simu zake wala sms zake hutoacha kuzijibu

 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Maty mbona unakuwa mtumwa kwa sababu ya mtoto?Furaha yako sio huyo mtoto,huo ndio ukweli!Usiumizwe amufu kufurahi hata kama atakuja kumchukua huyo binti,inaonekana anakuburuza kwa kumtumia huyo binti!Amua sasa kuishi kwa furaha bila kutegemea furaha ya kukopa kutokana na uwepo wa binti yako!
 
Back
Top Bottom