Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 40,000
Ninyi mnaojifanya kukosoa mafisadi, iweje leo mnatutapeli? inakuwaje mnatuuzia gazeti ambalo asilimia 90 ni tangazo? ni kweli mimi kama msomaji nilienda kibandani kununua tangazo au gazeti lenye habari na makala makini za kusoma na kuelewa?
mimi kijana mtanzania, jobless wenyewe mnatuita wasaka tonge, najiandaa wikinzima ili jumatano niweze kununua gazeti lenye makala na busara za waandishi lukuki nilizozizoea, naiingia kibandani na kuona gazeti limetuna, furaha ikanijaa kwamba labda jumatano hii kuna makala za nguvu, kumbe ni tangazo?
hivi hamuoni aibu kutuuzia robo gazeti na robotatu ikiwa ni tangazo tu? natambua mnafanya biashara. sawa. lakini kama mmeona leo kuna matangazo ya kuwalipa hela nyingi na yanayolazimika kuathiri utendaji wenu, kwa nini msitoe gazeti bure au kupunguza bei angalau kwa leo tu ili na sisi tusipoteze hela yetu kununua visivyotuhusu? kwa nini msituandikie juu kwamba gazeti lenu leo hii halina makala za waandishi mliowazoea na badala yake kuna tangazo ili tusiingie mkenge?
mmeniuzunisha sana na sikuamini kama pesa inaweza kununua utu wenu.
na kama mnajifanya kuwa watu huru katika masuala ya demokrasia kama makala ya LULa inavyomdai DPP, basi chapisheni barua yangu hii kwenye gazeti. vinginevyo nitajua kwamba wengi tunaojifanya wasafi sio wasafi bali tunatumia makosa ya wengine kutajirika na kupata umaarufu wa reja reja.
acheni kutafuta utajiri wa haraka wa kutuonyesha habari za kushtushwa (shocking news) juu ya gazeti wakati ndani ni matangazo tu. nimesikitishwa sana, nimefedheheswa sana na sikuafiki kitendo chenu hiki.
Wewe uliyandika ujumbe huu hauna maana hata blogu yako sitembelei -- kama kutangaza blogu ni kwa hoja kama hizi na lugha hizi basi wabongo tuna safari ndefu za mafanikio nina uhakika wewe utakuwa ni mhitimu wa mlimani
Msomaji ana haki ya kulalamika lakini uandishi wa namna hii pia haujakaa kiungwana, gazeti lingekuwa langu ningeweza kuifanyia marekebisho hoja ya mlalamikaji na ikasomeka vema na wazi kuwa ni malalamiko lakini ikiwa katika mtiririko ambao naweza kumwomba radhi akanielewa.Je ana hoja?
Who's this guy? Is it Mwanakijiji?
Msomaji ana haki ya kulalamika lakini uandishi wa namna hii pia haujakaa kiungwana, gazeti lingekuwa langu ningeweza kuifanyia marekebisho hoja ya mlalamikaji na ikasomeka vema na wazi kuwa ni malalamiko lakini ikiwa katika mtiririko ambao naweza kumwomba radhi akanielewa.
Inasikitisha kama alichoandika mhusika ndicho kilichotokea lakini bado sishangai kwani natambua safari bado ni ndefu, yani hata wao (Raia Mwema) yawezekana wakawa wanatumiwa bila wao kujua kuwa ndio hivyo wanatumiwa ama uchumi ndio unaochangia hali hii. Haya pia yanawezekana kuwa yaleyale kwa mwandishi wa barua pepe hii.
Mwanakijiji, katika Cheche unaandika kila unachotumiwa?
Jamaa anaonekana kuwa na machungu, lakini anajua Lula huyo ni nani? Si Mhariri wa gazeti hilo? I do get his/her concern lakini nachelea kuegemea upande wake ama upande wa Raia Mwema...mmeniuzunisha sana na sikuamini kama pesa inaweza kununua utu wenu.
na kama mnajifanya kuwa watu huru katika masuala ya demokrasia kama makala ya LULa inavyomdai DPP, basi chapisheni barua yangu hii kwenye gazeti. vinginevyo nitajua kwamba wengi tunaojifanya wasafi sio wasafi bali tunatumia makosa ya wengine kutajirika na kupata umaarufu wa reja reja.
Wewe uliyandika ujumbe huu hauna maana hata blogu yako sitembelei -- kama kutangaza blogu ni kwa hoja kama hizi na lugha hizi basi wabongo tuna safari ndefu za mafanikio nina uhakika wewe utakuwa ni mhitimu wa mlimani
Who's this guy? Is it Mwanakijiji?
Msomaji ana haki ya kulalamika lakini uandishi wa namna hii pia haujakaa kiungwana, gazeti lingekuwa langu ningeweza kuifanyia marekebisho hoja ya mlalamikaji na ikasomeka vema na wazi kuwa ni malalamiko lakini ikiwa katika mtiririko ambao naweza kumwomba radhi akanielewa.
Inasikitisha kama alichoandika mhusika ndicho kilichotokea lakini bado sishangai kwani natambua safari bado ni ndefu, yani hata wao (Raia Mwema) yawezekana wakawa wanatumiwa bila wao kujua kuwa ndio hivyo wanatumiwa ama uchumi ndio unaochangia hali hii. Haya pia yanawezekana kuwa yaleyale kwa mwandishi wa barua pepe hii.
Mwanakijiji, katika Cheche unaandika kila unachotumiwa?
If it is Mwanakijiji so what?
Umeleta hoja nzuri sana hapa.
Suala la kutumiwa bila wewe kujua, ni suala nyeti sana.
Unapewa ule kisha wakati wewe unakula watu wanakula kila kitu.
Nijiulizacho kila siku ni hiki.
Big Boss mwenyewe nyuma ya karibu kila mtu kutumiwa ni nani?
uzoefu wangu wa kuongea na viongozi wazito ndani ya serikali, ikiwa ni pamoja na mashushu wa muda mrefu sana unaonyesha kwamba kuna kundi la watu au wanao ogopwa siku zote na kila mtu.
Nijuavyo mimi watu hao si wana siasa wala wanajeshi ila ni watu waliojizazia nguvu nyingi za ajabu. Walitakalo kamwe halipingwi.
Huyo Big Boss wa kumfanya kila mtu ndani na nje ya CCM kijakazi ni nani au ni kina nani??
ukishakuwa big boss mpaka ukawa unaitishia "system" hatua
inayofuata ni "kupopolewa" tu na unabaki historia.