macho_mdiliko
Platinum Member
- Mar 10, 2008
- 28,214
- 56,829
Nimekuelewa mkuu. Hapa key word ni ''kupoteza muda'' au ''killing time'' kama wanavyosema waingereza. Kwangu mimi kupoteza muda ni ku-engage kwenye activities ili muda uende, hasa hasa mtu anapokuwa yupo free na anataka muda uende kwa haraka(kwa sababu kukaa bila ya kufanya kitu mtu anaboreka). Ukichukulia neno ''kupoteza muda'' kama ni kukaa bila kufanya chochote, sidhani kama ni sahihi kwa sababu neno linatumika kama ''idiomatic expression'' yaani maneno yake hayamaanishi tendo linalotendeka. Kwa mfano ''kutafuta kipande cha mkate''. Hii inamaanisha kutafuta kipato na siyo mkate wenyewe.Mkuu haya mambo unayoyafanya sio kupoteza muda
