Msidhani wote tunapapatikia hilo

Msidhani wote tunapapatikia hilo

Ma Mshuza

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2019
Posts
251
Reaction score
1,253
Nimekwazika sana na baadhi ya wanaume washamba wa magari, wanadhani wanawake wote ni washamba wa magari. Magari siyo issue siku hizi.

Natembea zangu kwa miguu kutafuta voucher taratibu pembeni ya barabara gari nime-park sehemu. Anakuja mtu anasimamisha gari miguuni pangu kidogo anigonge mpaka nimeanguka kwa mshtuko.

Bila aibu anakuja kuninyanyua eti naomba nikupeleke unakoenda mrembo.

Nimemrabua kibao na kumwambia ampeleke mama yake. Magari ya mikopo yanawafanya mnakuwa na vidudu washa kila mwanamke mnadhani ni cheap chinese goods.

Nimemwambia yeye na gari lake wote naweza wapakiza kwenye gari yangu kigari chenyewe ni kisubaru. Nimemwambia aje nimpakize kwenye Toyota Harrier.

Wanaume acheni kudhani kila mwanamke anayetembea ni sababu hana gari au atakuwa anapapatikia magari. Huo ni ushamba, tusije vunjana miguu bure kwa mambo yenu ya kitoto. Hivi vitoto vya siku hizi havina hata busara.

Jamani. Habari zenu? Za siku? nimekuja na mahasira yangu mwenyewe hata sikusalimia.

Mwanaume unapaswa kuwa mstaarabu ndo utapata wadada wastaraabu.
 
Mshkaj kaja akusaidie ww unamlenga kibao na maneno juu duh, ungetumia tu busara ya kumpotezea kiaina ingekua poa
 
Alitaka kunigonga...kaja kufungia break miguuni tena upande wa kulia wa barabara hiyo yote anipe lift.sikupenda.nimemchapa kibao ajifunze ustaarabu.mi sipendi ujinga hivyoo.

Mshkaj kaja akusaidie ww unamlenga kibao na maneno juu duh, ungetumia tu busara ya kumpotezea kiaina ingekua poa
 
Alitaka kunigonga...kaja kufungia break miguuni tena upande wa kulia wa barabara hiyo yote anipe lift.sikupenda.nimemchapa kibao ajifunze ustaarabu.mi sipendi ujinga hivyoo.
Niliamua kukupuuza tu, ningeweza kukurudishia na usingenifanya chochote. Kumbe ulijiona shujaa!?
 
Mbona kama Bongo Movie hii,yaani umeanguka kwenye kadamnasi ya watu lakini wote hawakupi msaada waaina yoyote mpaka anashuka yule dereva wakati huo wwe bado uko chini unamsubiri aje akuinuwe baada ya hapo unamzaba kibao! Haaaaahaaaaa!!
 
Nadhani hoja ulizotoa zina mashiko kabisa ILA ule msukumo wa hasira uliopo ndani yako unaongea mambo mengi kuliko hata Yale wanayoyajua wale wanaokuzunguka. Natumaini LA kumchapa kibao ni geresha na sio kweli ILA kama umemchapa kweli kibao ninaweza kushawishika kukuuliza aina ya ndoto unazoota usiku.

Siku njema.

Ahsante
 
Mmmh...! Kwa lipicha hilo wewe ndio umtukane aliekusimamishia gari? Sina uhakika. Any way pole sana,usije ukahamishia kwangu taarabu
 
Labda una chura ndo ilimchanganya baharia. Siku nyingini fikiri kabla ya kutenda. Mfano umempiga kibao kadondoka vibaya akafariki huoni utakuwa matatizoni wewe? Kwa maelezo yako uliyotoa nimeyasoma kwa makini sana sijaona tatizo lolote baharia alilotenda.

Kwanza, alikusogolea kwa karibu kwa umakin bla kukugonga ingawa ww ulihis tofauti. Pili, alikuita kwa bashasha na upendo "mrembo" bila shaka huku akitabasamu, alikuwa sahihi.

Tatu, akatoa ofa yakukupeleka unapopataka bahati ilioje ingkuwa huna usafiri au usafiri wako ungekuwa umeharibika. Nasisitiza baharia alikuwa sahihi.

Nne, baharia alikuwa sahihi kwakuwa alionesha nia ya kuchangamkia fursa haraka alipoiona Kama tunavyohimizwa na ajenda za chama chetu tukufu cha mabaria.

Tano, naskitika kuwa umehatarisha nafasi za warembo wengine kwa ubinafsi wako usio na maana. Imagine baharia akianza kuogopa kuwafata warembo kwa style hio, ikiwa Kuna maelefu ya warembo barabarani wanatembea ili iwakutane na fursa Kama hizo.

Mwisho, baharia atakuwa amefanya kosa kubwa Sana, ambalo litafanya ww kuombwa radhi na chama cha mabaria wote ikiwa itabainika kuwa huna chura, Hunashape kali na huna mvuto.
 
Funny thing about women; if someone they don't like, does something, it's creepy and strange. Wakati another man, might do the same thing and they'd considered it cute and sweet. What matters ni level of interest tu.

Huyo mashkaji hakukuvutia tu, lasivyo usingereact hivyo(if the whole story is true anyway).

Kama na wewe unavyolidharau gari la mwenzako na wengine wanalichukulia gari la aina yako hivyo hivyo.

Next time be humble and just politely tell someone you ain't interested. It doesn't hurt to be kind.
 
Hii hadithi tamu ila sukari imezidi, kama vipi mods waipeleke jukwaa la utani
 
Kumekucha Tanzania nchi ambayo chura ya mwanamke inathaminika kuliko chochote
 
Foresta Subaru vs harrier!! MPAMBANO HUU JAMANI KWAWANAOJUA UZURI WAGARI NATHAMANI YAKE
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom