Msiba mkubwa kutokea UDSM ikiwa...

Msiba mkubwa kutokea UDSM ikiwa...

hakuna mwanafunzi anayependa kubebwa kila mtu anapenda privacy lakini kwa udsm mwaka wa kwanza pekee ndio wana guarantee ya kupata accomodation ,the rest ni bahati na sibu ukikosa inabidi utafute mtu wa kukubeba maana kukaa /kupanga mtaani nako ni changamoto kubwaa kwa shule jinsi ilivyo ngumu.UDSM waliifaidi wa enzi za nyerere
 
Huyo aliyeyakagua na kutoa wito wa kutokutumika ni nani? Sisi tumefika pale miaka ya 98 tukaambiwa mara yamekaa upande sijui yameegama, mara sijui yametitia upande, lakini hatukuwahi kuona tatizo hata siku moja zaidi ya kukatika kwa zile kingo za kwenye viambaza vya nje. Mimi sidhani kama uongozi wa UDSM ni mzembe kiasi hicho kwamba usijui hali halisi ya majengo hayo. Hakuna kiongozi yeyote wa chuo ambaye anapenda wanafunzi wengi kiasi kile wanaoishi kwenye vyumba hivyo wafe. Bila shaka wamejiridhisha na usalama wake ndiyo maana wamewaacha wanafunzi humo. Hao walioumia walianguka kutoka vyumbani au ilikuwaje? Na kwanini waanguke, au pressure? Huko unakosema kuyumba, ni mechanism ya majengo yote ya Ghofofa kufanya hivyo kwa ajili ya shock absorption.

Heri ulikuwepo,kuna watu humu ndani wanashuk uzandiki wa kiwango cha hali ya juu.

Huyu mdukuzi ndio kabisa,kadai kuna wanafunzi walilazwa Baada ya lile tukio kitu ambacho hakipo Kabisa, na waliumia kwa kujigonga kwenye kingo za Ngazi, na hakuna hata mmoja akiyelazwa zaidi ya kupewa tiba na kurudi vyumbani mwao kwa maandalizi ya Mitihani ya Kumaliza Semester!

Majengo haya yangekuwa imara sidhani kama uongozi wa Chuo ungejenga majengo MAWILI ya recreation jirani na Hall 6 na Yombo 5.

Baada ya Tukio baaadhi yetu walipata Wasaa wa kuongea na baadhi ya Watumishi (Lecturers Civil Engineering) haya Mahengo ni imara kuliko tunavyodhani na Yamekuwa yakikaguliwa mara kwa Mara.
 
Ukweli wako ni upi? Kwamba majengo yale ni salama salimini? Current users ni waongo? Kwamba sikuwa resident wa hall 5 academic yr 1998/99?
Nina mashaka na wewe, lazima utakuwa NGWINI!

Ndio uelewa wako umeishia hapa,Yale Majengo ni salama salimini.

Viongozi wa Chuo sio wajinga kama wewe.

Acheni kukurupuka kujaza server za Jf bila kufanya Uchunguzi.
 
Ninashangaa kwani wahandisi wa hayo majengo ni wakuaminika sana. Yameshukaje kiwango?
 
Majengo yale hall two na five sio kama magotofa yenu ya kariakoo. yale yalijengwa yakajengeka na wajenzi wajengaji. usitumie macho na hisia tumia vipimo vya kisayansi ku ya condemn

Hall 2 na Hall 5 yalijengwa ma waisrael waliokuwa pia wamejenga Kilimanjaro Hotel kama sikosei. Foundation yake ina rollers halafu kuta zake ni flexible. Kwa hiyo jengo linahimili deflection kiasi fulani bila kuvunjika kuta, na vile vile huwa linabadili bearing ili kupunguza effects za terrestrial magnetic forces.

Tatizo kubwa la majengo yale sasa kwa takariban miaka 15 ni pale walipoweka double decks na kufanya yachukue watu zaidi ya capacity yake. Kwa mara ya kwanza yalikuwa designed kuwa kila chumba kiwe cha mtu mmoja, baadaye tukaongeza kufanya kila chumba kitumiwe na wanafunzi wawili, lakini mwishoni walipoweka double deck na kufanya kila chumba kitumiwa na watu wanne au zaidi basi hiyo iliweka stress sana katika structures za jengo na huenda sasa hivi yamechoka kweli.
 
Majengo yale hall two na five sio kama magotofa yenu ya kariakoo. yale yalijengwa yakajengeka na wajenzi wajengaji. usitumie macho na hisia tumia vipimo vya kisayansi ku ya condemn

Nimekaa hall 2 floor ya kumi 2009 siyo kiivyo unavyosema... Yaani sometimes concrete pieces zinadondoka kutoka juu... Kama uko chini inakula kwako... Kiujumla yalikuwa imara ila muda wake umekwisha yataleta maafa yale.
 
Nimekaa hall 2 floor ya kumi 2009 siyo kiivyo unavyosema... Yaani sometimes concrete pieces zinadondoka kutoka juu... Kama uko chini inakula kwako... Kiujumla yalikuwa imara ila muda wake umekwisha yataleta maafa yale.

Hivyo vipande vya concretes ni Matokeo ya Kubomoa Viambata vilivyokuwa vimechomoza kwenye hayo majengo.

Tatizo mnakurupuka kuja kulalamika hapa, maana baada ya tukio viongozi wenu waliufuata uongozi wa Chuo, (Estates) Waliambiwa Haya majengo yapo imara na yamekuwa yakikaguliwa mara kwa mara.
 
Ukweli wako ni upi? Kwamba majengo yale ni salama salimini? Current users ni waongo? Kwamba sikuwa resident wa hall 5 academic yr 1998/99?
Nina mashaka na wewe, lazima utakuwa NGWINI!

Wewe mpuuzi kwanza unajua maana ya neno NGWINI. baba yako ndio ngwini. wewe umemaliza chuo juzi juzi sana hata sasa bado una studentisys mentality. kama kichwani una nazi badala ya ubongo kaa kimyam..
 
Yangu ni Poleni wanachuo. Hiyo ndiyo Elimu yenyewe. Unahatarisha maisha yako miaka 5 halafu ukitoka hakuna ajira. Nashauri;
- Serekali ipunguze udahili, iweze kwanza kuwahudumia hawa hawa waliopo sasa hivi. Warudi kwenye standard inayokubalika. TBS isiwe tu kwenye vipodozi, iingie hata kwenye taasisi kubwa kama hii inayowachukua watoto wetu na kwenda kuwa ning'iniza kwenye kamba ya mauti. Likidondoka pale, hawana hata Life Insurence. Wanazikwa kama bata wa jirani tu. Kilio ni cha familia husika tu. Hata mngeshusha bendera zote zisipepee kabisa, mwanangu atarudi?
- Serekali hii sikivu, wapunguzeni hao vijana muwaweke wenye kulingana na vyumba hivyo.
- Wataalamu wa ujenzi mlioko nchini, nendeni mkayakague, kama hayafai, piga ban. Mbona wanachoma tani za vipodozi, mnashindwa nini ku ban hayo majengo mabovu? Ulimwengu utawalaani siku hao watu watakapo anguka nalo.
 
Hivyo vipande vya concretes ni Matokeo ya Kubomoa Viambata vilivyokuwa vimechomoza kwenye hayo majengo.

Tatizo mnakurupuka kuja kulalamika hapa, maana baada ya tukio viongozi wenu waliufuata uongozi wa Chuo, (Estates) Waliambiwa Haya majengo yapo imara na yamekuwa yakikaguliwa mara kwa mara.

Ndugu wakati huo hakuna ujenzi wala ubomozi wowote uliokuwa ukifanyika.. Ukifika pale hata leo utagundua even plaster iliyopigwa nje inamong'onyoka... Hii kitu italeta maafa na kama hujawahi ishi pale usiongee tu jaribu kufika pale ujionee.
 
haya majengo yana miaka zaidi ya 50 hatukatai kwamba ni imara kwani hata roli la tani 7 ukilibebesha tani 15 litachoka kabla ya muda tatizo hapa ni overloading,capacity ya kubeba mtu mmoja kwa chumba sasa ni watu wanne ,kubebana ndio point ya kujadili kwani uimara utapungua tu,siku ya kianguka ndio utasikia tume zinaundwa kwa gharama wakati tume inaweza kufanya kazi kabla ya maafa
 
leo wanafunzi wa cuo kikuu cha dar es salaam wamefunga semester ya kwanza kwa mwaka huu wa masomo huku wanafunzi wanaoishi kampasi ya jk nyerere zamani mlimani katika mabweni ya hall 2 na hall 5 wakimshukuru mungu kwa kwenda likizo salama,hii ni kutokana na usalama mdogo wa mabweni hayo.

Alfajiri kuamkia siku ya ijumaa 7 feb 2013 kama itakumbukwa kulitokea upepo mkali sana katika jiji la dar hali iliyopelekea majengo tajwa kuyumba na kutikisika mpka wanafunzi sita wakajeruhiwa na kulazwa kwa muda katika zahanati ya chuo kikuu.

Majengo hayo ilishashauriwa yasitumike kutokana na usalama wake.kwa asiyeyafahamu ni yale majengo marefu kabisa ya ghorofa kumi lakini uongozi wa chuo umeziba masikio.

Ee mwenyezi mungu apishilie mbali yasije kuporomoka wakati chuo kimefunguliwa.
gud idea yasitmike toa mbadala wake wapelekwe waph hall 3
si wako kimya wanajihoji kwa hli
 
Ndugu wakati huo hakuna ujenzi wala ubomozi wowote uliokuwa ukifanyika.. Ukifika pale hata leo utagundua even plaster iliyopigwa nje inamong'onyoka... Hii kitu italeta maafa na kama hujawahi ishi pale usiongee tu jaribu kufika pale ujionee.

Naifahamu Udsm wewe, wadanganye wengine huko...

Ni jengo gani kati ya Hayo Mawili lilikopigwa Kiraka ! Au hiyo Plaster na inamomonyoka!
ACHA UONGO.
 
Back
Top Bottom