mdukuzi
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 22,323
- 56,062
Leo wanafunzi wa cuo kikuu cha dar es salaam wamefunga semester ya kwanza kwa mwaka huu wa masomo huku wanafunzi wanaoishi kampasi ya JK Nyerere zamani mlimani katika mabweni ya hall 2 na hall 5 wakimshukuru Mungu kwa kwenda likizo salama,hii ni kutokana na usalama mdogo wa mabweni hayo.
Alfajiri kuamkia siku ya ijumaa 7 feb 2013 kama itakumbukwa kulitokea upepo mkali sana katika jiji la Dar hali iliyopelekea majengo tajwa kuyumba na kutikisika mpka wanafunzi sita wakajeruhiwa na kulazwa kwa muda katika zahanati ya chuo kikuu.
Majengo hayo ilishashauriwa yasitumike kutokana na usalama wake.Kwa asiyeyafahamu ni yale majengo marefu kabisa ya ghorofa kumi lakini uongozi wa chuo umeziba masikio.
Ee mwenyezi Mungu apishilie mbali yasije kuporomoka wakati chuo kimefunguliwa.
Alfajiri kuamkia siku ya ijumaa 7 feb 2013 kama itakumbukwa kulitokea upepo mkali sana katika jiji la Dar hali iliyopelekea majengo tajwa kuyumba na kutikisika mpka wanafunzi sita wakajeruhiwa na kulazwa kwa muda katika zahanati ya chuo kikuu.
Majengo hayo ilishashauriwa yasitumike kutokana na usalama wake.Kwa asiyeyafahamu ni yale majengo marefu kabisa ya ghorofa kumi lakini uongozi wa chuo umeziba masikio.
Ee mwenyezi Mungu apishilie mbali yasije kuporomoka wakati chuo kimefunguliwa.