Kufuta Sherehe za Uhuru wa Tanganyika huku Sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar zikiachwa ni ishara ya kuiua kabisa Tanganyika , hatutakubali kirahisi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,561
217,865
Leo 9 Disemba ni siku ya kumbukumbu ya Uhuru wa Tanganyika , Siyo kumbukumbu ya Uhuru wa Tanzania wala Tanzania Bara , kwahiyo upotoshaji wowote kuhusu sherehe hizi tutaupinga kwa nguvu zote bila kujali cheo cha mpotoshaji wala ukubwa wake

Mara kadhaa tumeshuhudia kuzimwa kwa sherehe za Uhuru wa Tanganyika kwa kisingizio cha ETI PESA ZA SHEREHE HIZO ZIELEKEZWE KWENYE HUDUMA ZA JAMII , Hivi huduma za jamii kama ujenzi wa mabweni na mengineyo hazitengewi bajeti ? kwanini hela za sherehe za Uhuru zipelekwe huko , nani kawatuma kufanya haya , kwanini ?

Kinachosikitisha ni kwambs , Wakati Watanganyika wananyimwa Sherehe za Uhuru wao , Wazanzibar ambao nchi yao haikumezwa na jina Tanzania wangali wanaendelea kusherehekea SIKU YA MAPINDUZI MATUKUFU kwa mbwembwe , hivi hawa mbona wao hawazuii sherehe kwa kisingizio cha kujenga mabweni , au watoto wao hawasomi ?

Sasa tunaanza kuona dhahiri nia ovu ya kuifukia Tanganyika na kuiinua Zanzibar , Nachukua nafasi hii kutangaza jambo hili kuwa miongoni mwa KERO MPYA ZA MUUNGANO , na jambo hili litatuliwe haraka .

Ni Utumwa na ni Aibu kubwa kwa nchi yoyote ile kupuuza Sherehe za Uhuru wake yenyewe kwa Visingizio vyovyote vile .

NITASEMA KWELI DAIMA FITNA KWANGU MWIKO
 
Akili zenu wanachadema sijui tusemejee, SHEREHE zimevunjwa Kwa faida au ni Kwa hasara, yaaani na wewe unashangilia mamilioni ya fedha yanategetea kununua mashati na kofia huku jamiii ikiwa shule hazina mabwenii?? Mimi nilidhani ungesemema hata hizo garama za mabinduzi bajeti take iangalie kutatua Tatizo la kijamiiii.
 
HappyBirthday TANGANYIKA
IMG_1015.jpg
 
Akili zenu wanachadema sijui tusemejee, SHEREHE zimevunjwa Kwa faida au ni Kwa hasara, yaaani na wewe unashangilia mamilioni ya fedha yanategetea kununua mashati na kofia huku jamiii ikiwa shule hazina mabwenii?? Mimi nilidhani ungesemema hata hizo garama za mabinduzi bajeti take iangalie kutatua Tatizo la kijamiiii.
Kwamba wakisitisha sherehe ndiyo. Hayo yatatekelezwa, maadhimisho ni kumbukizi safi kwa vizazi vijavyo......
Jamaa ni.lama kuuliza swali je maadhimisho ya uhuru ya Tanganyika yanapigwa burn ila ya zanzibar itahadhimishwa !!! Ni sahihi
 
Back
Top Bottom