Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

Zomba ni kweli, wabunge wanachota millioni 10 kwa mwezi sasa...Halafu inashangaza sisi wananchi tunaendelea kupiga makelele CCM Oyee, Chadema Oyee, CUF Oyee wakati hawa watu hakika hawana maana kabisa wala Uzalendo rohoni mwao wakiendesha hoja bungeni za mgomo, Dr.Ulimboka, Muungano na madudu mengine kutupoteza sisi wananchi kuelewa kilichofanyika..

I mean sasa hivi naanza kukosa kabisa imani ya hawa viongozi wetu wote! mtanisamehe viongozi wangu lakini hii sii kupigania haki wala M4C - I think time has come kwetu sisi wananchi kuchukua jukumu hilo maanake nilisikia mpango huu mapema kwamba badala ya kuongeza posho zilizokataliwa, wafanye ongezeko la mshahara wao na imekuwa. Huu ni mpango wa CCM baada ya mgomo wa kwanza wa madaktari, kuwaonyesha wananchi kwamba hao Chadema mnaowatetea sana mbona nao wanachukua mishahara mikubwa?. Mbona nao wanafanya yale yale maduidu ya CCM?.. Nikajiuliza sana lakini nikasema Chadema hawatakubali hili.. Heee kumbe wamejaa tele leo hii nao wamejitikwa zigo la ndizi kichwani wakati wanajua fika sii wabunge wanaotakiwa kutekeleza maendeleo majimboni bali Halmashauri zao. Kwa taarifa yenu hili swala litaibuka wakati wa Uchaguzi na Chadema mtashindwa kujitetea kwa wananchi.

Hili ongezeko kiuhalisia lilitakiwa kuongezwa ktk Halamshauri za majimbo yao maana wabunge wengi wanafanya kazi za Halamshauri ili kujenga majina yao wakati sii jukumu lao kutumia madai haya haya ya ongezeko la mshahara au posho zao. Mimi naomba viongozi wa Chadema walioko hapa janvini, watupe majibu ya swala hili hapa hapa JF maana wanatembelea sana. Hii habari ya sisi kushabikia vitu nadhani huu utakuwa mwisho wake, wengine hatuwezi kuwa bendera.

Kama serikali yetu inavyofanywa ombaomba na nchi matajiri ndivyo nao wana imani ya kuchukua kodi zetu halafu wanadai kwamba wanatusaidia bila fedha hawawezi kumudu maisha na sijui kutoa misaada majimboni. Nani kawambia tunahitaji misaada badala ya ujenzi wa nchi kwa kodi zetu?.. Fedha yetu inangia kwao mfuko mmoja inatoka mfuko mwingine wakidai ni uwezo wao?.. Itafika wakati mbunge atakuwa kama RC na ndio maana tunajichanganya..Hii haikubaliki kabisa, inaondoa imani zetu kwa hawa viongozi wetu na sasa naanza kurudi nyuma kujitazama upya!..

Si kweli kuwa mshahara wa Wabunge ni million 10 kwa mwezi:

UKWELI KUHUSU MISHAHARA YA WABUNGE
Jun 21st 2012, 17:14
http://1.bp.blogspot.com/-k1RiR2FloJY/T-NV574J6aI/AAAAAAAC9sU/1CBpWOgCxc0/s1600/bu.jpg

Wakati Bunge liko kwenye mchakato wa Bajeti ya 2012/13, yameanza kujitokeza maneno na taarifa mbalimbali juu ya kupanda kwa mishahara ya watumishi wa Umma wakiwemo Wabunge. Mathalani, siku ya Jumatano tarehe 20 Juni 2012, gazeti moja linatokalo kila siku lilikuwa na habari yenye kichwa kisemacho "Mishahara ya Wabunge juu".



Ofisi ya Bunge imeona ni vyema kutoa ufafanuzi juu ya suala zima la mishahara ya Wabunge ili umma uweze kuelimika ipasavyo juu ya taratibu zinazotawala jambo hili kama ifuatavyo:


· Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ambayo inajumuisha Fungu Na. 42 lenye Bajeti ya Bunge bado haijasomwa Bungeni, na hivyo haiwezekani leo hii kueleza kuwa kuna nyongeza ya bajeti inayohusu mishahara kwa Wabunge.
· Si kweli kwamba mishahara ya Wabunge imeongezwa toka kiwango wanacholipwa sasa, kwa kuwa mishahara yao kama ilivyo ya watumishi wote wa umma, hurekebishwa kwa waraka maalum toka Ofisi ya Rais, na si Kamisheni au Kamati yoyote ya Bunge.
· Waraka wa mwisho wa toka Ofisi ya Rais unaotoa Masharti ya Kazi ya Mbunge ulitolewa tarehe 25 Oktoba 2010, na kueleza kuwa Mbunge atalipwa mshahara katika ngazi ya LSS (P) 2, na ni waraka huo unaotumika mpaka sasa.
· Mapendekezo ya ongezeko la 32% ya Bajeti ya Ofisi ya Bunge yaliyooneshwa kwenye kitabu cha Bajeti namba 2, cha matumizi ya kawaida yaliyowasilishwa mezani ni ya matumizi mengine ambayo hayana uhusiano na ongezeko la mishahara.


Mwisho, Ofisi ya Bunge wakati wote inathamini sana mchango wa vyombo vya habari katika juhudi za kuelimisha umma juu ya kazi za chombo chao cha uwakilishi. Hata hivyo, Ofisi inasikitishwa sana na habari za upotoshaji zinazotolewa kwa lengo la kujenga chuki kati ya Wabunge na watu wanao wawakilisha.
Kwa mantiki hiyo, tunazidi kuwasihi Waandishi waandike habari au makala baada ya kufanya utafiti wa kina kuhusu jambo husika na pale inapobidi waweze kupata ufafanuzi toka Idara husika katika Ofisi ya Bunge, ili kuepuka kuupotosha umma.

Imetolewa na:
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa
Ofisi ya Bunge,
S.L.P 941, DODOMA.
21 Juni 2012
 
Si kweli kuwa mshahara wa Wabunge ni million 10 kwa mwezi:

UKWELI KUHUSU MISHAHARA YA WABUNGE
Jun 21st 2012, 17:14


Wakati Bunge liko kwenye mchakato wa Bajeti ya 2012/13, yameanza kujitokeza maneno na taarifa mbalimbali juu ya kupanda kwa mishahara ya watumishi wa Umma wakiwemo Wabunge. Mathalani, siku ya Jumatano tarehe 20 Juni 2012, gazeti moja linatokalo kila siku lilikuwa na habari yenye kichwa kisemacho "Mishahara ya Wabunge juu".


Ofisi ya Bunge imeona ni vyema kutoa ufafanuzi juu ya suala zima la mishahara ya Wabunge ili umma uweze kuelimika ipasavyo juu ya taratibu zinazotawala jambo hili kama ifuatavyo:

· Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ambayo inajumuisha Fungu Na. 42 lenye Bajeti ya Bunge bado haijasomwa Bungeni, na hivyo haiwezekani leo hii kueleza kuwa kuna nyongeza ya bajeti inayohusu mishahara kwa Wabunge.
· Si kweli kwamba mishahara ya Wabunge imeongezwa toka kiwango wanacholipwa sasa, kwa kuwa mishahara yao kama ilivyo ya watumishi wote wa umma, hurekebishwa kwa waraka maalum toka Ofisi ya Rais, na si Kamisheni au Kamati yoyote ya Bunge.
· Waraka wa mwisho wa toka Ofisi ya Rais unaotoa Masharti ya Kazi ya Mbunge ulitolewa tarehe 25 Oktoba 2010, na kueleza kuwa Mbunge atalipwa mshahara katika ngazi ya LSS (P) 2, na ni waraka huo unaotumika mpaka sasa.
· Mapendekezo ya ongezeko la 32% ya Bajeti ya Ofisi ya Bunge yaliyooneshwa kwenye kitabu cha Bajeti namba 2, cha matumizi ya kawaida yaliyowasilishwa mezani ni ya matumizi mengine ambayo hayana uhusiano na ongezeko la mishahara.

Mwisho, Ofisi ya Bunge wakati wote inathamini sana mchango wa vyombo vya habari katika juhudi za kuelimisha umma juu ya kazi za chombo chao cha uwakilishi. Hata hivyo, Ofisi inasikitishwa sana na habari za upotoshaji zinazotolewa kwa lengo la kujenga chuki kati ya Wabunge na watu wanao wawakilisha.
Kwa mantiki hiyo, tunazidi kuwasihi Waandishi waandike habari au makala baada ya kufanya utafiti wa kina kuhusu jambo husika na pale inapobidi waweze kupata ufafanuzi toka Idara husika katika Ofisi ya Bunge, ili kuepuka kuupotosha umma.

Imetolewa na:
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa
Ofisi ya Bunge,
S.L.P 941, DODOMA.
21 Juni 2012
Zomba, Hizi kamba tu tunapigwa changa la macho kwa sababu hakuna hata siku moja wananchi tumetangaziwa ongezeko la mishahara ya wabunge isipokuwa kwa kushtukizwa. Hilo ongezeko la asilimia 32 ni pamoja ni mahitaji yote yanayotakiwa kufanyika bungeni 2012/13 na bajeti yao imepita. Bila shaka hata mfanyakazi serikalini kuongezewa mshahara lazima kuna waraka maalum unaopitishwa ili mshahara wake upande lakini hutanguliwa na bajeti yake kuwepo yaani fedha kuwepo tayari kwa maandalizi ya kupandisha mishahara. Haiwezekani serikali, mahakama, bunge au hata shirika binafsi kupandisha mishahara wakati fedha hiyo haipo ktk bajeti ya matumizi ya mwaka..

Madaktari leo wanagoma ni kwa sababu wameona ktk bajeti hii hakuna ongezeko linaloelekezwa kupandisha mishahara yao na ndio maana wamegoma. Lakini pia ili mishahara mipya ianze inatakiwa makubaliano yafikiwe, na taratibu zifuatwe kupata go ahead. sitegemei bunge wangekuja na kusema ktk bajeti hii mishahara ya madaktari imepanda toka Tsh laki 7 hadi millioni, ingeleta vurugu kubwa nchini kwa taaluma nyinginezo na ndio maana kila kitu wanapitishia milango ya nyuma ktk ulipaji mishahara na madeal yao.

Ni kutokana na bajeti ya serikali tunaweza kujua kuna mpango gani wa kuboresha umeme au maji lakini kabla ya shirika lolote kuleta generator zake kuna mkataba ambao lazima upitishwe kisheria, Bunge halipitishi mikataba hii ila fedha huwepo tayari kwa kazi hiyo. Sasa kwa sababu leo hatuna mkataba basi ina maana hakunampango wala fedha zilizotengwa kwa ajili hiyo?. Kumaliza ubishi huu tunaiomba ofisi ya bunge iorodheshe hapa hilo ongezeko la asilimia 32 ni kwa matumizi gani ( moja baada ya jingine) na sii kuuma maneno.
 
Zomba, Hizi kamba tu tunapigwa changa la macho kwa sababu hakuna hata siku moja wananchi tumetangaziwa ongezeko la mishahara ya wabunge isipokuwa kwa kushtukizwa. Hilo ongezeko la asilimia 32 ni pamoja ni mahitaji yote yanayotakiwa kufanyika bungeni 2012/13 na bajeti yao imepita. Bila shaka hata mfanyakazi serikalini kuongezewa mshahara lazima kuna waraka maalum unaopitishwa ili mshahara wake upande lakini hutanguliwa na bajeti yake kuwepo yaani fedha kuwepo tayari kwa maandalizi ya kupandisha mishahara. Haiwezekani serikali, mahakama, bunge au hata shirika binafsi kupandisha mishahara wakati fedha hiyo haipo ktk bajeti ya matumizi ya mwaka..

Madaktari leo wanagoma ni kwa sababu wameona ktk bajeti hii hakuna ongezeko linaloelekezwa kupandisha mishahara yao na ndio maana wamegoma. Lakini pia ili mishahara mipya ianze inatakiwa makubaliano yafikiwe, na taratibu zifuatwe kupata go ahead. sitegemei bunge wangekuja na kusema ktk bajeti hii mishahara ya madaktari imepanda toka Tsh laki 7 hadi millioni, ingeleta vurugu kubwa nchini kwa taaluma nyinginezo na ndio maana kila kitu wanapitishia milango ya nyuma ktk ulipaji mishahara na madeal yao.

Ni kutokana na bajeti ya serikali tunaweza kujua kuna mpango gani wa kuboresha umeme au maji lakini kabla ya shirika lolote kuleta generator zake kuna mkataba ambao lazima upitishwe kisheria, Bunge halipitishi mikataba hii ila fedha huwepo tayari kwa kazi hiyo. Sasa kwa sababu leo hatuna mkataba basi ina maana hakunampango wala fedha zilizotengwa kwa ajili hiyo?. Kumaliza ubishi huu tunaiomba ofisi ya bunge iorodheshe hapa hilo ongezeko la asilimia 32 ni kwa matumizi gani ( moja baada ya jingine) na sii kuuma maneno.

Naanza chini kwenda juu:

1) ongezeko la asilimia 32 ni kwa matumizi gani = Ni wapi palipoongezwa asilimia 32?

2) hakunampango wala fedha = Jee, unaongelea bajeti yenya mapato "0" au ipi?

3) Sasa kwa sababu leo hatuna mkataba = Mkataba upi na nani ambao hauna?

Ukimaliza kujibu hayo, ntakuongezea niliyoweka nyekundu kwenye barua (post) yako.
 
Naanza chini kwenda juu:

1) ongezeko la asilimia 32 ni kwa matumizi gani = Ni wapi palipoongezwa asilimia 32?
Nanukuu Ofisi ya Bunge:- Mapendekezo ya ongezeko la 32% ya Bajeti ya Ofisi ya Bunge yaliyooneshwa kwenye kitabu cha Bajeti namba 2, cha matumizi ya kawaida yaliyowasilishwa mezani ni ya matumizi mengine ambayo hayana uhusiano na ongezeko la mishahara.

2) hakunampango wala fedha = Jee, unaongelea bajeti yenya mapato "0" au ipi?
Bajeti iliyopitishwa majuzi.. Je,ni kiasi gani kimeonmgezeka ktk matumizi ya Bunge ukilinganisha na mwaka 2011/12?..3)
Sasa kwa sababu leo hatuna mkataba = Mkataba upi na nani ambao hauna?
Katika bajeti ya mwaka huu unajua ni mikataba gani tayari imehspitishwa tokana na bajeti hiyo?
Ukimaliza kujibu hayo, ntakuongezea niliyoweka nyekundu kwenye barua (post) yako.
Malizia tu mkuu wangu ni vizuri sana ukiandika unachokijua wewe kuhusu ongezeko la mishahara ya wabunge maana wabunge wenyewe ndio wamemwaga mboga mitaani...Kwa majisifa ya mtatuweza?.. sisi ndio tunaendesha nchi..
 
Mapendekezo ya ongezeko la 32% ya Bajeti ya Ofisi ya Bunge yaliyooneshwa kwenye kitabu cha Bajeti namba 2, cha matumizi ya kawaida yaliyowasilishwa mezani ni ya matumizi mengine ambayo hayana uhusiano na ongezeko la mishahara.

Jee, hiyo ina maanisha kuwa mishahara ya wabinge ni Million 10? au hujui maana ya matumizi ya kawaida?

Bajeti iliyopitishwa majuzi.. Je,ni kiasi gani kimeonmgezeka ktk matumizi ya Bunge ukilinganisha na mwaka 2011/12?..3)

Jee ulitaka bajeti isiongezeke? bajeti imepanda kwa asilimia nyingi tu, lakini haimaanishi kuwa wabunge wamepandishiwa mishara kufikia millioni 10.

Katika bajeti ya mwaka huu unajua ni mikataba gani tayari imehspitishwa tokana na bajeti hiyo?

Nakuuliza wewe, soma post yangu vizuri, na wewe unarudisha swali kwangu mimi? siijuwi ndio maana nikakuuliza.

Malizia tu mkuu wangu ni vizuri sana ukiandika unachokijua wewe kuhusu ongezeko la mishahara ya wabunge maana wabunge wenyewe ndio wamemwaga mboga mitaani...Kwa majisifa ya mtatuweza?.. sisi ndio tunaendesha nchi..

Nnacho kijuwa mimi ni kuwa hakuna mshahara wa Millioni 10 kwa mbunge. Kama wewe unaujuwa tueleze ni Mbunge yupi anaepokea mshahara huo au aliyeahidiwa kuwa atapewa mshara huo.


 
Mapendekezo ya ongezeko la 32% ya Bajeti ya Ofisi ya Bunge yaliyooneshwa kwenye kitabu cha Bajeti namba 2, cha matumizi ya kawaida yaliyowasilishwa mezani ni ya matumizi mengine ambayo hayana uhusiano na ongezeko la mishahara.

Jee, hiyo ina maanisha kuwa mishahara ya wabinge ni Million 10? au hujui maana ya matumizi ya kawaida?

Bajeti iliyopitishwa majuzi.. Je,ni kiasi gani kimeonmgezeka ktk matumizi ya Bunge ukilinganisha na mwaka 2011/12?..3)

Jee ulitaka bajeti isiongezeke? bajeti imepanda kwa asilimia nyingi tu, lakini haimaanishi kuwa wabunge wamepandishiwa mishara kufikia millioni 10.

Katika bajeti ya mwaka huu unajua ni mikataba gani tayari imehspitishwa tokana na bajeti hiyo?

Nakuuliza wewe, soma post yangu vizuri, na wewe unarudisha swali kwangu mimi? siijuwi ndio maana nikakuuliza.

Malizia tu mkuu wangu ni vizuri sana ukiandika unachokijua wewe kuhusu ongezeko la mishahara ya wabunge maana wabunge wenyewe ndio wamemwaga mboga mitaani...Kwa majisifa ya mtatuweza?.. sisi ndio tunaendesha nchi..

Nnacho kijuwa mimi ni kuwa hakuna mshahara wa Millioni 10 kwa mbunge. Kama wewe unaujuwa tueleze ni Mbunge yupi anaepokea mshahara huo au aliyeahidiwa kuwa atapewa mshara huo.


Zomba! mkuu wangu tuache uswahili, hatubishani ila tunafahamishana..Wewe nambie hizo asilimia 32 zilizopanda zimepandishwa kwa matumizi yapi? kama unajua hakuna mishahara ktk makadirio hayo bila shaka unajua villivyomo ktk ongezeko hilo au sivyo? Je, ni matumizi yapi yaliyoongezewa mfuko ama kuongezwa..

Hayo ya mikataba nimeshasema fedha zinatengwa kabla ya mikataba kuwekwa nikiwa na maana huwezi kuweka mkataba na mtu wakati huna mpango wa kupata fedha ktk kugharamia matumizi yake iwe hata tunategemea misaada, huwa tunaahidiwa fedha kwanza kwa ajili ya ujenzi wa mradi fulani halafu ndio mipango ya mkataba inafuata au sivyo?..Sasa unaponiliuza ni mikataba gani nashindwa kukuelewa japokuwa tayari bungeni imeshaandaliwa bajeti kwa miradi ya maendeleo.
 
Zomba! mkuu wangu tuache uswahili, hatubishani ila tunafahamishana..Wewe nambie hizo asilimia 32 zilizopanda zimepandishwa kwa matumizi yapi? kama unajua hakuna mishahara ktk makadirio hayo bila shaka unajua villivyomo ktk ongezeko hilo au sivyo? Je, ni matumizi yapi yaliyoongezewa mfuko ama kuongezwa..

Hayo ya mikataba nimeshasema fedha zinatengwa kabla ya mikataba kuwekwa nikiwa na maana huwezi kuweka mkataba na mtu wakati huna mpango wa kupata fedha ktk kugharamia matumizi yake iwe hata tunategemea misaada, huwa tunaahidiwa fedha kwanza kwa ajili ya ujenzi wa mradi fulani halafu ndio mipango ya mkataba inafuata au sivyo?..Sasa unaponiliuza ni mikataba gani nashindwa kukuelewa japokuwa tayari bungeni imeshaandaliwa bajeti kwa miradi ya maendeleo.

Hivi Bungeni hakuna gharama zinazoongezeka? Kuongezeka bajeti kwa asilimia 32 hakumaanishi zote ni za mishahara, mishahara imeshasemekana kuwa watumishi wote wa umma wataongezewa mishahara asilimia 10 mpaka 20. Bunge lina gharama zake za kimaendeleo pia, mfano mmoja tu, mbali ya gharama za kuendesha bunge kuongezeka pia kuna nia ya kujenga ofisi za wabunge ambazo hazijakamilika kote nazo zinahitaji fedha. Isitoshe, inabidi tupongeze kwa sasa tunaziona na kuzijuwa hata bajeti za bunge na kuweza kuzijadili, kabla ya Kikwete kuwa Rais tulikuwa hatujui kabisa bajeti ya bunge, hata wabunge wenyewe walikuwa hawajui.

Nakataa kuwa mishahara ya wabunge imeongezwa na kuwa Millioni 10. Huu ni ni upotoshaji wa makusudi.
 
Mkandara naona huna thread nyingine ya kutoa mchango wako ndio maana umeamuwa kupoteza muda wako na huyu Zombi kibaraka wa wala nchi.
Huyu akili zake ni empty half glass, shake well before use.
 
Last edited by a moderator:
Hivi Bungeni hakuna gharama zinazoongezeka? Kuongezeka bajeti kwa asilimia 32 hakumaanishi zote ni za mishahara, mishahara imeshasemekana kuwa watumishi wote wa umma wataongezewa mishahara asilimia 10 mpaka 20. Bunge lina gharama zake za kimaendeleo pia, mfano mmoja tu, mbali ya gharama za kuendesha bunge kuongezeka pia kuna nia ya kujenga ofisi za wabunge ambazo hazijakamilika kote nazo zinahitaji fedha. Isitoshe, inabidi tupongeze kwa sasa tunaziona na kuzijuwa hata bajeti za bunge na kuweza kuzijadili, kabla ya Kikwete kuwa Rais tulikuwa hatujui kabisa bajeti ya bunge, hata wabunge wenyewe walikuwa hawajui.

Nakataa kuwa mishahara ya wabunge imeongezwa na kuwa Millioni 10. Huu ni ni upotoshaji wa makusudi.
Kama unajua mishahara haipo bila shaka unajua wameongeza wapi? Tunarudi pale pale - Ni matumizi gani yaliyoongezewa asilimia 32? - Kukataa kujibu ni upotoshaji kama ulivyokuwa ukifanywa miaka yote nyuma..
 
Kama unajua mishahara haipo bila shaka unajua wameongeza wapi? Tunarudi pale pale - Ni matumizi gani yaliyoongezewa asilimia 32? - Kukataa kujibu ni upotoshaji kama ulivyokuwa ukifanywa miaka yote nyuma..

Hivi huelewi kuwa bajeti hupanda kila mwaka na aghalabu sana kushuka? kwani ni wapi walipokataa kuonesha matumizi na matumizi yote yapo kwa vifungu katika bajeti ya kila wizara na idara. Unaweza kupitia na kujionea mwenyewe zikisha chambuliwa bungeni, kwa sasa bado zinajadiliwa kwa hiyo haiwezi kuwa ni kielelezo tosha kwani huwa kuna mabadiliko hutokea, hutokea bajeti nzima kupingwa na kuandikwa upya, ilitokea bajeti iliyopita. Tusubiri, halafu tubishane kuhusu mshahara wa wabunge kuwa ni Million 10. Ambao si ukweli.
 
Hivi huelewi kuwa bajeti hupanda kila mwaka na aghalabu sana kushuka? kwani ni wapi walipokataa kuonesha matumizi na matumizi yote yapo kwa vifungu katika bajeti ya kila wizara na idara. Unaweza kupitia na kujionea mwenyewe zikisha chambuliwa bungeni, kwa sasa bado zinajadiliwa kwa hiyo haiwezi kuwa ni kielelezo tosha kwani huwa kuna mabadiliko hutokea, hutokea bajeti nzima kupingwa na kuandikwa upya, ilitokea bajeti iliyopita. Tusubiri, halafu tubishane kuhusu mshahara wa wabunge kuwa ni Million 10. Ambao si ukweli.
Swali langu rahisi sana.. Maadam wewe umeisha chambua na kujua mishahara haikuongezwa kwa wabunge. Nambie hizo asilimia 32 ulizo quote zimeongezwa wapi na wapi. Hii ya kwani hujui, haiwezi kusaidia mjadala huu maana tunataka kujua fedha za walipa kodi zitatumika vipi ktk ongezeko hilo la bungeni.. Wewe ulokuja hapa na kudai sivyo, ndio unatakiwa uwe na majibu - Hutaki unaacha...
 
Swali langu rahisi sana.. Maadam wewe umeisha chambua na kujua mishahara haikuongezwa kwa wabunge. Nambie hizo asilimia 32 ulizo quote zimeongezwa wapi na wapi. Hii ya kwani hujui, haiwezi kusaidia mjadala huu maana tunataka kujua fedha za walipa kodi zitatumika vipi ktk ongezeko hilo la bungeni.. Wewe ulokuja hapa na kudai sivyo, ndio unatakiwa uwe na majibu - Hutaki unaacha...

Hivi wewe kama hujaichambuwa umejuwaje kuwa mshahara umefikia Million 10? una ushahidi wowote wa kutuaminisha hivy? nakuhakikishia siyo za mshahara wa Millioni 10 kwa mwezi asemae hivyo si mkweli na nimekuwekea juu huko barua ya kutoka ofisi za bunge au hukuiona? Nakuwekea tena hapa:

UKWELI KUHUSU MISHAHARA YA WABUNGE
Jun 21st 2012, 17:14


Wakati Bunge liko kwenye mchakato wa Bajeti ya 2012/13, yameanza kujitokeza maneno na taarifa mbalimbali juu ya kupanda kwa mishahara ya watumishi wa Umma wakiwemo Wabunge. Mathalani, siku ya Jumatano tarehe 20 Juni 2012, gazeti moja linatokalo kila siku lilikuwa na habari yenye kichwa kisemacho "Mishahara ya Wabunge juu".


Ofisi ya Bunge imeona ni vyema kutoa ufafanuzi juu ya suala zima la mishahara ya Wabunge ili umma uweze kuelimika ipasavyo juu ya taratibu zinazotawala jambo hili kama ifuatavyo:

· Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ambayo inajumuisha Fungu Na. 42 lenye Bajeti ya Bunge bado haijasomwa Bungeni, na hivyo haiwezekani leo hii kueleza kuwa kuna nyongeza ya bajeti inayohusu mishahara kwa Wabunge.
· Si kweli kwamba mishahara ya Wabunge imeongezwa toka kiwango wanacholipwa sasa, kwa kuwa mishahara yao kama ilivyo ya watumishi wote wa umma, hurekebishwa kwa waraka maalum toka Ofisi ya Rais, na si Kamisheni au Kamati yoyote ya Bunge.
· Waraka wa mwisho wa toka Ofisi ya Rais unaotoa Masharti ya Kazi ya Mbunge ulitolewa tarehe 25 Oktoba 2010, na kueleza kuwa Mbunge atalipwa mshahara katika ngazi ya LSS (P) 2, na ni waraka huo unaotumika mpaka sasa.
· Mapendekezo ya ongezeko la 32% ya Bajeti ya Ofisi ya Bunge yaliyooneshwa kwenye kitabu cha Bajeti namba 2, cha matumizi ya kawaida yaliyowasilishwa mezani ni ya matumizi mengine ambayo hayana uhusiano na ongezeko la mishahara.

Mwisho, Ofisi ya Bunge wakati wote inathamini sana mchango wa vyombo vya habari katika juhudi za kuelimisha umma juu ya kazi za chombo chao cha uwakilishi. Hata hivyo, Ofisi inasikitishwa sana na habari za upotoshaji zinazotolewa kwa lengo la kujenga chuki kati ya Wabunge na watu wanao wawakilisha.
Kwa mantiki hiyo, tunazidi kuwasihi Waandishi waandike habari au makala baada ya kufanya utafiti wa kina kuhusu jambo husika na pale inapobidi waweze kupata ufafanuzi toka Idara husika katika Ofisi ya Bunge, ili kuepuka kuupotosha umma.

Imetolewa na:
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa
Ofisi ya Bunge,
S.L.P 941, DODOMA.
21 Juni 2012


Hivi unataka ufahamishwe vipi zaidi ya hii barua ya kutoka Bungeni inavyojieleza?
 
Zomba,
Dah mkuu wangu ubishi umeuanza lini?.. Wee siku zote uko bongo miaka yote... Mshahara wa Wabunge aliyekuja kuusema wazi alikuwa Dr.Slaa wakati akiwa bungeni hakuna mbunge,waziri wala rais aliyewahi kututangazia mshahara wa wabunge na posho zao. Hatujui mshahara wa rais wetu, waziri mkuu na wengine tukiwaondoa Mwinyi na Nyerere. Kifupi nasema hivi wabunge wanashukua fedha nene sana na hata siku moja hawatasema wanachukua ngapi isipokuwa ongezeko au pounguzo hapa na pale hadi upate kuona matumizi yake ndio tunashtuka.

Hakuna mkataba wala matumizi yanayofanyika yakapitishwa kwanza bungeni isipokuwa serikali na bunge wenyewe wanaamua wapige wapi. Sisi tunakuja shitukia ikija report ya Mkaguzi mkuu wa mahesabu wa serikali which is too late tumeisha liwa. Mfano fedha za Richmond zilikuwepo lakini hakuna aliyejua watanunua generator used one, mpya au kuweka umeme wa upepo, jua na kadhalika. Tukapigwa changa la macho la EL lakini siku zilizotengwa ungeweza kabisa kupinga hakuna bajeti iliyotengwa ili kununua mitambo ya Richmond maana haipangwi na Bunge letu.. Hivyo hivyo ktk matumizi ya kawaida utaambiwa hivi ama vile lakini fedha huombwa zikifika ofisini hapo ndio mchezo unaanza.

Nimefanya kazi wizara ya Habari, Mifugo kama mhasibu..Fedha zimekuwa allocated tayari kwa matumizi na hakuna anayepanga in advance shilingi kwa shilingi itatumika kiasi gani ktk kila Item na wapi isipokuwa kupanga matumizi kulingana na makadirio ya mahitaji. Nimeona ufujaji wa fedha na jinsi viongozi wanavyotunga safari na mikutano. At the end kila mwaka huwa tuna deficit yaani tuna matumizi makubwa kuliko makadirio. Fedha ipo wanaweza kabisa kuongeza mishahara kwa sababu hawahitaji rruksa ya mtu bana wote hawa wamoja. Ubishi huu sintouweza maadam naamini kabisa kwamba serikali yetu inatumia fedha vibaya sana na sasa naliona hata Bunge letu kwa tamaa ile ile linachukua mkondo huo huo wa kujirusha na fedha za walipa kodi..
 
Zomba,
Najua wapi tunaposhindana sasa, Ok niseme kiswahili fasaha badala ya kutumia neno mshahara niseme PATO la mbunge limeongezeka kufika 10,000,000 hilo nalo hukubalini nalo?
 
Zomba,
Najua wapi tunaposhindana sasa, Ok niseme kiswahili fasaha badala ya kutumia neno mshahara niseme PATO la mbunge limeongezeka kufika 10,000,000 hilo nalo hukubalini nalo?

Sikubaliani nalo. Pato la wabunge ni zaidi ya Million kumi.

Soma kichwa cha habari kinasemaje. Jee, ni sawa hivyo au upotoshaji huo?
 
Sikubaliani nalo. Pato la wabunge ni zaidi ya Million kumi.

Soma kichwa cha habari kinasemaje. Jee, ni sawa hivyo au upotoshaji huo?
Sasa muda wote huu ulikuwa wapi kujieleza maana ilikuwa rahisi tu kusema Mshahara ni Tsh mil3, marupurupu ya posho za vikao, mafuta na kadhalika ni Tsh kadhaa jumla Tsh millioni 12. ningekuelewa mkuu wangu.

Unajua huku majuu hata mcheza Basketball huweka mkataba wa mshahara wa Millioni 40 kwa mwaka, mwingine millioni 100 kwa miaka mitatu na kadhalika na tunaelewa kinachosemwa lakini ndani yake kuna vipengele kibao.. Kama hukuelewa ama hukubaliani unajieleza unachofahamu halafu utafahamishwa mgao wenyewe unakuwaje hadi ikasema mshahara wake ni millioni 40 kwa mwaka..By the way mwanao Hasheem Thabit kasaini mkataba wa miaka miwili kwa NBA minimum salary ya 900,000. Huyu dogo sijui vipi tu yaani aibu tupu, anaharibu vibaya sana
 
Sasa muda wote huu ulikuwa wapi kujieleza maana ilikuwa rahisi tu kusema Mshahara ni Tsh mil3, marupurupu ya posho za vikao, mafuta na kadhalika ni Tsh kadhaa jumla Tsh millioni 12. ningekuelewa mkuu wangu.

Unajua huku majuu hata mcheza Basketball huweka mkataba wa mshahara wa Millioni 40 kwa mwaka, mwingine millioni 100 kwa miaka mitatu na kadhalika na tunaelewa kinachosemwa lakini ndani yake kuna vipengele kibao.. Kama hukuelewa ama hukubaliani unajieleza unachofahamu halafu utafahamishwa mgao wenyewe unakuwaje hadi ikasema mshahara wake ni millioni 40 kwa mwaka..

Sasa unaongelea PATO la mbunge au mshahara au marupurupu? unanchanganya sana.

Nimekuuliza kuhusu kichwa cha habari hujanijibu.

Unafikiri Pato la mbunge kama Mbowe ni dogo? ukumbi wa Bilicanas pekee si mchezo kipato chake. Sasa chukuwa kina Nchambis, Abood wana mabasi hayana hesabu ukienda kwa Mohamed Dewji ndiyo usiseme, Mzee wa vijisenti ana Ng'ombe wasio na idadi maana akiwahesabu leo, akienda kesho wameongezeka kwa kuzaana.

Tusipindishe maana ya Mshahara huo ni upotoshaji wa makusudi kabisa. Soma kichwa cha habari useme kama huo si upotoshaji ni nini?
 
Sasa unaongelea PATO la mbunge au mshahara au marupurupu? unanchanganya sana.

Nimekuuliza kuhusu kichwa cha habari hujanijibu.

Unafikiri Pato la mbunge kama Mbowe ni dogo? ukumbi wa Bilicanas pekee si mchezo kipato chake. Sasa chukuwa kina Nchambis, Abood wana mabasi hayana hesabu ukienda kwa Mohamed Dewji ndiyo usiseme, Mzee wa vijisenti ana Ng'ombe wasio na idadi maana akiwahesabu leo, akienda kesho wameongezeka kwa kuzaana.

Tusipindishe maana ya Mshahara huo ni upotoshaji wa makusudi kabisa. Soma kichwa cha habari useme kama huo si upotoshaji ni nini?
Bilcana tena, ndio maana tunatumia neno mshahara, sio upotoshaji.. Unaona sasa ulivyopotosha wewe hapa?. tunazungumzia mshahara wa Mbunge changanya vyote ambavyo ni wajibu wake kama mbunge mkuu wangu sio kila kitu anachoingiza nje ya bunge. Tunaposema mshahara wa Daktari hatuunganishi na vibanda vyake vya kuuza nguo za China..
 
Bilcana tena.... tunazungumzia Pato la Mbunge mkuu wangu sio kila mtu.. Tunaposema pato la Daktari (mshahara) hatuunganishi na na vibanda vyake vya kuuza nguo za China..

Tunarudi palepale, unaongelea mshahara wa mbunge? au pato la mbunge? au marpurupu ya Mbunge?

Kichwa cha habari kinasema "Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 10,000,000/-"

Nini usichotaka kukubali? kuwa Kichwa cha habari kinapotosha ukweli?

Mimi nasema Mshahara wa mbunge haujafika Million 10. Huu ni upotoshaji wa makusudi kabisa "gutter politics".
 
Wanabodi.

Marupurupu ya wabunge ikiwamo mishahara imeongezwa kutoka Sh7.4 milioni kwa mwezi hadi Sh11 milioni kwa mwezi, hatua ambayo imeibua mjadala mwingine mzito miongoni mwao mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe alizikataa posho akisema mbunge anapokuwa kazini haijataji kulipwa.

Chadema pamoja na wabunge wake wanafanya siri wananchi wasijue sababu wakijua itakuwa tatizo, Chadema walikuwa wanapinga posho lakini wao wamekuwa wa kwanza kushirikiana na CCM kuchukua hizo posho mpya wameanza kuchukuwa toka Ijumaa...hata hivyo kuna kundi la wabunge wanapinga posho hizo mpya pamoja na mishahara wakitaka nyongeza hiyo ya fedha zielekezwe katika sekta za jamii.

Hadi mwezi uliopita mbunge alikuwa akipokea Sh7.4 milioni kwa mwezi ambazo kati ya hizo Sh2.5 milioni ni kwa ajili ya mafuta, Sh2.3 mshahara, Sh 170,00 kwa ajili ya mshahara wa dereva, 100,000 kwa ajili ya katibu wa mbunge na posho ya jimbo.
 
Back
Top Bottom