Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Mobhare Matinyi amesema ukisoma JamiiForums hata kama umeingia umenuna utacheka tu kwa kuwa ni sehemu inayowapa watanzania uhuru wa kuzungumza.
Ameipongeza JamiiForums kwa kuandaa shindano la stories of Change ambalo halfa ya utoaji wa zawadi kwa washindi inafanyika leo, Oktoba 7, 2023 kwenye hoteli ya Hyatt Regency, the Kilimanjaro.
Amesema jukwaa la stories of change linatoa fursa nyingi ikiwemo ya kukuza kiswahili, lakini Tanzania ina mtandao huu mmoja unaotumiwa na watu zaidi ya milioni 20.
Ameisifu JamiiForums kwa kuanzisha jukwaa la JamiiCheck linalowashirikisha wananchi Mchakato wa kuhakiki usahihi wa maudhui yanayopatikana ndani na nje ya mtandao.
Pia, amesema Serikali inafuatilia kwa ukaribu mijadala ya JamiiForums, ile ya kufaa itachukuliwa na kufanyiwa kazi.
Katika hatua nyingine, Bwana Mobhare amesema JamiiForums ni taasisi ya mfano katika kuwajengea uwezo waandishi wa habari ambapo sasa mojawapo ya miradi yake ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari 600 nchi nzima ili kusaidia upatikaji wa taarifa za kutosha.
Zaidi, soma: Yanayojiri katika Usiku wa Utoaji Zawadi kwa Washindi wa Shindano la Stories of Change 2023
Ameipongeza JamiiForums kwa kuandaa shindano la stories of Change ambalo halfa ya utoaji wa zawadi kwa washindi inafanyika leo, Oktoba 7, 2023 kwenye hoteli ya Hyatt Regency, the Kilimanjaro.
Amesema jukwaa la stories of change linatoa fursa nyingi ikiwemo ya kukuza kiswahili, lakini Tanzania ina mtandao huu mmoja unaotumiwa na watu zaidi ya milioni 20.
Ameisifu JamiiForums kwa kuanzisha jukwaa la JamiiCheck linalowashirikisha wananchi Mchakato wa kuhakiki usahihi wa maudhui yanayopatikana ndani na nje ya mtandao.
Pia, amesema Serikali inafuatilia kwa ukaribu mijadala ya JamiiForums, ile ya kufaa itachukuliwa na kufanyiwa kazi.
Katika hatua nyingine, Bwana Mobhare amesema JamiiForums ni taasisi ya mfano katika kuwajengea uwezo waandishi wa habari ambapo sasa mojawapo ya miradi yake ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari 600 nchi nzima ili kusaidia upatikaji wa taarifa za kutosha.
Zaidi, soma: Yanayojiri katika Usiku wa Utoaji Zawadi kwa Washindi wa Shindano la Stories of Change 2023