johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,968
- 141,975
Mzee Msekwa amesema wakati muungano unaasisiwa yeye alikuwa ni Katibu wa bunge na ndiye aliyeupeleka Ikulu muswada huo baada ya kupitishwa na bunge ili ukasainiwe na iwe sheria.
Mzee Msekwa anasema alipofika Ikulu na kumweleza Rais kuwa wabunge wote kwa kauli moja wamepitisha mswada wa muungano Mwalimu Nyerere kwanza alikunywa glass ya Wine kwa furaha kisha akausaini pale pale kuwa sheria.
Mjadala unaendelea.......
Source: Star tv
Mzee Msekwa anasema alipofika Ikulu na kumweleza Rais kuwa wabunge wote kwa kauli moja wamepitisha mswada wa muungano Mwalimu Nyerere kwanza alikunywa glass ya Wine kwa furaha kisha akausaini pale pale kuwa sheria.
Mjadala unaendelea.......
Source: Star tv
Aliyekuwa katibu wa Bunge wakati Tanganyika na Zanzibar zinaungana leo kwenye sherehe ya kumbukumbu ya muungano ameelezea yaliyojiri kwenye matukio na historia ya muungano.
Msekwa amesema chimbuko la Muungano wa Tanzania ni mapinduzi kwani Nyerere asingeweza kuzungumza na Sultan Jamsheed kuhusu muungano na wakati huo ilikuwepo haja ya kuyalinda mapinduzi hayo.
Msekwa amesema Jamsheed aliongoza kwa hila kwani inaaminika chama cha Afro shirazi kilishinda uchaguzi na Jamsheed kuiba matokeo.
Msekwa amesema jambo ambalo wengi hawalijui ni usiri mkubwa uliotawala mazungumzo baina ya marais wawili, Nyerere na Karume. Sababu kuu ikiwa hofu kubwa iliyokuwepo kwamba yangejulikana mapema, zingetengenezwa njama za kuhujumu.
Makubaliano ya Muungano yalisema Rais wa kwanza wa Jamhuri atakuwa Nyerere na makamu wake atakuwa Abeid Karume ili kuondoa haja ya kufanya uchaguzi kwasababu tayari wamewekwa na sheria.