Msafara wa Makonda wapata ajali

Msafara wa Makonda wapata ajali

Kwahiyo hapo ulitaka usikie, waloumia ni Mwenyekiti wa CCM, katibu wa CCm, na viongozi wa CCM??.

Wee hujaona kua na Katibu Tawala Mkoa ' RAS ' kajeruhiwa? Ulitaka katibu tawala Mkoa, atumie usafiri wa Chama???.
RAS anafuata Nini kwenye msafara wa MC wa CCM?. Bora angekuwa Katibu Mkuu au Mwenyekiti wa chama. Sasa MC anatembeza kwenye msafara mavumbini mpaka ajali? Watumie akili siku nyingine.
 
Weee huna akili, unahisi Kifo Cha Mzee Lowassa, kingepunguza nyomi la Makonda kama angeamua kuendelea na Mikutano?.


Hata hivo, Makonda ni mwenye Hekima, Busara, na Mwenye Akili, kama Kiongozi wa Chama, anajua wajibu wake wa Kichama ni upi .
Wewe bado mtoto huwezi kunielewa. Nakuacha Kama ulivyo. Halafu makonda ana nyomi gani?. Mikutano inaandaliwa Wana CCM wanasafirishwa na watu kuandikiwa mabango ya kumsifu makonda. Pole pole mtaelewa tu.
 
Msafara wa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Paul Makonda umepata ajali leo Februari 11, 2024 katika eneo la Sululu, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, mkoani Mtwara.

Katika ajali hiyo, magari 13 yaligongana na kusababisha majeruhi kadhaa wakiwepo Mbunge wa Jimbo la Tandahimba, Katani Ahmed Katani na Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Bahati Geuza.

======
Msafara wa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Paul Makonda umepata ajali leo Februari 11, 2024 katika eneo la Sululu, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, mkoani Mtwara.

Katika ajali hiyo, magari 13 yaligongana na kusababisha majeruhi kadhaa wakiwepo Mbunge wa Jimbo la Tandahimba, Katani Ahmed Katani na Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Bahati Geuza.

View attachment 2900908
Ina maana kifo Cha mwanachama mwenzake hakimhusu!!?

Kwani akienda msibani atapungukiwa nini!!?

RIP comrade.Edo!
 
11 February 2024
Sululu, Masasi
Mtwara Tanzania

MSAFARA WA MWENEZI, MAGARI ZAIDI YA 13 YAGONGANA BAMPA TO BAMPA

Kutoka Sululu katika kata ya Wilaya ya Masasi Mjini katika Mkoa wa Mtwara, Tanzania. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2022, kata ilikuwa na wakazi wapatao 12,578


View: https://m.youtube.com/watch?time_continue=2&v=vm15PZ5uvMA

Apunguze ulimbukeni. U MC wa chama anataka awe treated Kama Rais?. Gari mbili au tatu zinatosha.
 
Back
Top Bottom