October man
JF-Expert Member
- Nov 23, 2017
- 3,632
- 5,023
- Thread starter
- #81
Vizuri kama usalama upo kiongozi. Nna kalikizo kasiku mbili kurudisha morali kidogo.
Unajua najifunza vitu vingi sana kwenye huu uzi.
Jambo la kwanza, kila mmoja ana matatizo na shida zake za kutosha hata kama hasemi au hawaambii watu.
Pili, sio kila unaemsaidia atakuja kukusaidia kwa kiwango ulichojitoa kwake. Ukiwa na huo mtazamo, utaishia kufadhaika na kugombana na watu bila sababu.
Mwisho, mtafuta suluhu na mfumbuzi wa matatizo yako ni wewe mwenyewe. Hakuna mtu ataipa shida yako kipaumbele au kuielewa vizuri kuliko wewe inayokukabili. Tuliza akili kutafuta suluhu stahiki.
Tatizo moja linaweza kuwapata watu wawili tofauti, mmoja akajiua, mwingine akaamua kwenda barabarani akawa ombaomba, mwingine akatafuta mtu akamweleza shida yake apate mtaji ajishughulishe na chochote kuliko kuwa tegemezi.
Ukiamua kumsaidia mtu msaidie tu kama una nafasi. Ubinadamu siku hizi mdogo. Mungu anajua atakavyoweza kukulipia hata kama sio kwako, kuna namna utalipwa tu, wema hauozi.
October man hiyo namba inaandika jina gani? Unaweza ni PM.
RRONDO uwe na siku njema kapteni.
sawa mkuu