Msaada tafadhali, naachikaje?

Msaada tafadhali, naachikaje?

Mpaka hapo tayari ushaachika. Kama hakujali wala kukusikiliza basi ushaachika mida tu.
 
Kaa nae, mwambie umechoka na tabia zake 1,2,3,4......
Kisha mwambie unataka muachane from that moment. Ondoka zako na shikilia msimamo wako
 
Mi nachojua mahakama haimlazimishi mtu kuendelea na ndoa yake kama ameamua mwenyewe kuivunja, so sioni tatizo, simply leave him and start your new life. Akikufanyia fujo vyombo vya sheria vipo vitakulinda na wala havitakulazimisha kurudi kwa mumeo.
Unless sijakuelewa vizuri unachohitaji
 
Last edited by a moderator:
Habari za jumapili waungwana,
Kimya kingi kina mshindo mwingi....... iko hivi nataka kuachika. ..... sababu nimechoka. ( vituko vya pombe)

Vituko vimezidi nimekuwa nikiongea na tunayazungumza na mwenzangu ila anarudia yale yale. Nataka kusonga mbele niendelee na maisha maana kama kulia nimelia sana kama kuvumilia nimevumilia sana.
Msaada wako ni niambie nifanyaje au nitumie njia ipi niachike bila ugomvi bila mimi kuwa na mchepuko bila kumlipizia visa alivonifanyia. Pia sitaki kutoroka nataka nikiachika niondoke na mwanangu na si kuwa baada ya hapo ntaanza mahusiano mapya laah. Nataka nijitawale mwenyewe nifanye yale nnayotaka na kumpa mwongozo mzuri mwanangu aje kuwa mtu mzuri baadae.
Mwenzenu nimechoka nimechoka sitaki cha padri wala askofu wala maongezi ya familia wala kikao cha ukoo.
Naomba nisaidie ikiwezekana January nianze 2016 maisha mapya.
Ubarikiwe kwa maoni yako.

Pole sana....

Niko ndani ya ndoa miaka zaidi ya 10 sasa.

Ndoa si uvumilivu.... Ndoa ni upendo...

Huwezi kuvumilia vipigo,matusi wala yanayofanana na hayo...unless na wewe unayafanya....

Maamuzi unayo wewe...
 
Mkunde Jina lako linaniambia Wewe ni DaDa Yangu kikabila Ingawa Sitaki kuamini Hivyo.

Ingawa Sipo katika ndoa lakini kwa Hili nitajaribu kukushauri kwa Kiasi nijuavyo. Mapenzi au ndoa ni Ya mke na mume na Hata ikitokea mikwaruzano Hukaa na Kuijadili kisha Kutafuta Suluhu na Hatimaye kumaliza Ugomvi.

Kutaka Kujitawala bila kujua Athari Zake ni kukosa Maono Ya Mbele Uendako... Usiongee kwa kuwa upo na uwezo wa Hilo lakini angalia ni Athari Zipi ambazo zitampata mtoto kwa kukosa malezi Ya Baba?

Kusema Kuwa Huna Mchepuko na Wala Hata Ukiachwa Hutaanzisha Uhusiano mpya hapo ni Kujitetea tu lakini watu wenye Akili zetu tunaelewa kuwa yupo ambaye ameshakushika Sikio na Unataka Kuondoka Ili Ukajitawale Kwa Huyo Mtu..

Lakini Kumbuka Thamani ya mtu haipimwi kwa kulipa ovu kwa ovu bali kwa wema..

NDOA NI
UVUMILIVU
KUJALI
KUTHAMINI
KUHESHIMU.

Kuwa Muangalifu Dada Usije kuruka mkojo ukakanyaga Kinyesi.
Pole sana kwa mtazamo ulionao, baba anarudi pombe kila siku, anakutukana na kukudhalilisha mbele ya mwanao halafu bado wafikiri kuwa kila uleapo, lazima malezi ya wote wawili? Nina rafiki ambaye akimfumania mumewe anapigwa na panga anashikiwa, watoto wanaona, hakuna hali ya kulinda wala kumsaidia mtoto hapo, MKUNDE wewe wajua maisha unayoishi, usijevumilia ukafa ndani ya nyumba, ataoa mwingine, fanya ambalo kwako ni jema ameshauri mtu hapo juu uwe na concrete reason nenda mahakamani fanya utakalo, jinsi gani utaishi baada ya talaka pia ni juu yako, fanya mambo sahihi, mtangulize Mungu, hata kwenye biblia talaka haikatazwi inakatazwa kuolewa tena.
 
exactly!....mpuuzi tu,afu eti ni mama!....linajifikiria lenyewe tu hili zuzu!
....kwenye ndoa tungekuwa tunahesabiana makosa,NANI ANGESIMAMA?!

Ukute mumewe naye anaakili kama ninyi, Mungu utuepushe na Hili balaa.
 
Tanzania kungekuwa na 'no-fault divorce' ningekushauri uchukue mkondo huo.

Hapo huhitaji sababu ingine zaidi ya 'kumchoka' 'kutoendana' au kuwa na 'tofauti zisizoweza patanishwa'.

Huhitaji kuonyesha kosa alilofanya mwenza wako. Raha sana kwa kweli.

Ila kibongo bongo hapo itabidi utumie njia mbadala.

Jaribu hizi: acha kuoga na kujisafisha mara kwa mara; acha kupiga mswaki; acha kujiremba na kujipodoa; acha kunyoa kwapa na kule sehemu sehemu; acha kupaka deodorant na kiachie kikwapa kiteme harufu kali.

Kwa kifupi, kuwa mchafu halafu uone kama yeye hajakuacha.

Mbona umesahau nyepesi ambayo inawezekanika, usimpe unyumba ama kama hakupi unyumba kwa zaidi ya miezi kadhaa waweza tumia hilo kuomba talaka maana umechoka kuishi kama kaka na dada, ama mnyime akuchoke akuache.
 
MMMMhn,mie napita manake mwenyezi mungu hapendi watu waachane....


Nilitaka kumwambia hivo na amesema hataki vikao wala nn najaribu kujiuliza hivi alitaftiwa huyu mme au la na jee hakumuona before kwamba n mlevi au vipi
 
Wanawake wa kabila/lugha hiyo kwenye red wakishaona wameanza kujiweza kimaisha huanza vitimbi vya kutaka kuachika. Hatushangai kwa uamuzi wako huo. Ni dhahiri mumeo kuwa mlevi ni wewe unamfrustrate. Bahati mbaya huyo jamaa yako si mchaga mwenzio ndiyo maana hata mazungumzo naye wala na jamaa zake wala na viongozi wa kanisa lake huyataki.

We we nawe wawaza ukabila tu. Hii jamii yetu niyakinafiki mno kwahyo aendelee kuteseka tu kisa aogope kuambiwa ameanza kujiweza.
Asilimia kubwa watu wanateseka kwenye ndoa na kujifanya wavumilivu ili kufurqisha jamii uonekane una heshima. Life is too short to stress up kah! Mwishowe uage dunia kisa mtu mzima uliyekutana naye akiwa na meno 32 tena mlevi ndo hatari. mkunde find ua own happiness pia mwombe Mungu funga na kusali atakuonyesha njia. Kikubwa kwenye maisha ni kuwa na peace of mind.
 
Last edited by a moderator:
Mbona umesahau nyepesi ambayo inawezekanika, usimpe unyumba ama kama hakupi unyumba kwa zaidi ya miezi kadhaa waweza tumia hilo kuomba talaka maana umechoka kuishi kama kaka na dada, ama mnyime akuchoke akuache.

Hivi mtu unathibitishaje kwamba mwenzako hakupi unyumba?
 
Mkunde ni jina la mwanangu fulani. Nimestuka kuliona hapa ika bht yeye bado olewa. Sasa mwanangu nikuukize: ulevi kaanza lini? Kabla au baada ya kuwa wote? Hiyo jeuri ya pesa si ndio ilikufanya ukamfuata? Wewe si ndio hutimizi majukumu ya mke ndani ndio maana anakushikisha adabu? Hujagundua tu? Hlf umeshamuonesha kiburi cha wazi2 kbs kwamba unataka juondoka. Uliwahi jiuliza nn kimepelekea hayo kutokea? Unafikiri ni mwanaune gani anataka kuoneshwa kibri na ke? Usipokuwa makini hutaondoka na ukiondoka bila kupata muafaka itakupa shida sana baafaye. Ndoa ni yakonaye , na ni nyie tu mtaoweza ijenga sio padre, askofu, papa baba yako au mama yako. Kuwa makini mwanangu jifunze kumpenda km zile siku za mwanzo za malavidavi ninihino n.k.
 
Hmm! Ngoja niseme pole tu .
Bora ukosee kujenga nyumba kuliko kukosea KUOA AMA KUOLEWA....NDOA HIZI HAZINA FORMULA WENGINE WANAISHI RAHA MSTAREHE UTADHANI MAPACHA WENYE KUFANANA KWA 100%. NA HUKU WENGINE WAKIISHI KWA KUVIZIANA HUKU KILA MMOJA AKIOMBA ANGALAU BASI AWE MJANE. AMA MGANE , MMOJAWAPO ATANULIE MBELE ZA HAKI ANGALAU KIFO KIWATENGANISHE TU.
 
Back
Top Bottom