Hujajibu maswali.
Hilo, hata kama litakuwa kweli, halithibitishi kwamba uchawi upo na si stories tu.
DALILI KUWA UCHAWI UPO, KUTOKA KATIKA QURANI NA KATIKA SUNNAH (MAFUNDISHO YA MTUME (SAW))
Katika Surat Yunus aya ya 77 MwenyeziMungu anasema:
"Akasema Musa:"Mnasema (hivi) juu ya haki ilipokujieni, (kuwa) Huu ni uchawi? (Mbona umefaulu basi) Na wachawi hawafaulu".
Hii ni dalili kwamba uchawi upo na MwenyeziMungu anatufundisha katika aya hii kwamba uchawi haufaulu.
Na katika sutaul Falaq akasema:
"Na (najikinga na) shari ya wale wanaopuliza mafundoni".
Katika kuifasiri aya hii, mmoja katika maulamaa wakubwa wa tafsiri ya Qurani Imam Al Qurtuby amesema:
"Maana ya neno "Nafaathaat", ni wachawi wanapopuliza katika nyuzi huku wakizipiga fundo.
Na Ibni Kathiyr katika tafsiri yake akinukuu kutoka kwa Ikrimah na Mujahid na Al Hassan Al Basry (RA) amesema:
"Hawa wanaopuliza mafundoni ni wachawi, na MwenyeziMungu anatuamrisha tujiepushe na shari zao.
Amma hadithi za Mtume (SAW) zinazotufahamisha kwamba uchawi upo na kwamba uchawi ni katika madhambi makubwa sana, ni hizi zifuatazo:
Kutoka kwa Abi Huraira (RA) kwamba Mtume (SAW) amesema:
"Jieupusheni na (mambo) saba Yaangamizayo'.
Wakasema:
'Ni yepi hayo ewe Mjumbe wa MwenyeziMungu?"
Akasema:
"Kumshirikisha MwenyeziMungu, Uchawi, kuiuwa nafsi iliyoharimishwa na MwenyeziMungu ila kwa haki yake, kula riba, kula mali ya yatima, kurudi nyuma (kukimbia) katika vita vya Jihadi (huku ukiwaacha wenzio wanapigana), na kuwasingizia uwongo wanawake wema wasio na makosa".
Bukhari na Muslim
Ndugu yangu Muislamu, Mtume (SAW) aliposema kuwa mambo hayo 'Yanayomuangamiza', maana yake ni kuwa yanamuangamiza mtu katika moto wa Jahannam.
Ukirudia kuisoma tena hadithi hiyo utaona kuwa Mtume (SAW) ameutanguliza uchawi kabla ya dhambi ya kuuwa, ingawaje kuuwa ni dhambi kubwa sana, na MwenyeziMungu anasema katika Suratu Nnisaa aya ya 93
"Atakayemuuwa Muislamu kusudi, basi jaza yake ni Jahannam atakuwa humo milele na MwenyeziMungu Ataghadhibika naye na Atamlaani na amemtayarishia adhabu kubwa".
Juu ya ukubwa wa dhambi hiyo ya kuuwa, lakini Mtume(SAW) ameipa uzito zaidi dhambi ya Uchawi kwa kuiweka nafasi ya pili baada ya Shirki na kabla ya dhambi ya kuuwa.