Unajuaje kwamba vitabu vya kiroho havikujazi ujinga?
Habari za firauni zimeandikwa kwenye peer reviewed journals za Egyptologists.
Hujathibitisha kwamba nguvu za giza zipo.
Ujinga unatoka wapi katika mambo ya kiroho???
Hebu soma chanzo cha nguvu za giza :::::
BIBLIA inasema hivi kumhusu Muumba wetu: Mungu ni nuru na hakuna giza kamwe katika muungano na yeye. (1 Yohana 1:5) Hilo ni kweli hasa kuhusu mambo ya kiroho. Kwa hiyo, je, Mungu wa kweli anaweza kuwa ndiye chanzo cha uchawi? Au je, kuna nguvu fulani ya uovu inayoongoza uchawi?
Baadhi ya mazoea ya kiuchawi ambayo watu hujihusisha sana nayo ni uaguzi na kuwasiliana na pepo kutia ndani unajimu, ubashiri wa kutumia namba, usomaji wa viganja, kuwasiliana na wafu na vilevile ulozi. Mazoea hayo yana historia ndefu, kwani mengi kati yake yalianzia Babiloni la kale, ambalo magofu yake yanapatikana huko Iraki. (Isaya 47:1, 12, 13) Kutoka Babiloni, mazoea ya uchawi yalienea kote katika ulimwengu wa kale na kutia mizizi katika tamaduni na jamii nyingi.
Fikiria tukio lililotokea katika jiji la Filipi lililokuwa katika Makedonia ya kale. Kikundi kidogo cha wahudumu Wakristo, kilichotia ndani mtume Paulo na daktari Luka, kilikutana na msichana aliyekuwa na nguvu za kufanya uchawi. Ona jinsi Luka, mwandikaji wa Biblia, alivyofunua chanzo cha nguvu hizo. Aliandika hivi: Kijakazi fulani mwenye roho, roho mwovu wa uaguzi, akakutana nasi. Yeye alikuwa akiwapatia mabwana zake faida nyingi kwa kufanya ufundi wa kubashiri.Matendo 16:16-18.
Naam, msichana huyo hakupata nguvu hizo kutoka kwa Mungu wa kweli, Yehova, bali kutoka kwa roho mwovu. Hiyo ndiyo sababu Paulo pamoja na waandamani wake walikataa kumsikiliza. Huenda unajiuliza hivi: Roho waovu ni nani? Nao walitoka wapi? Hebu ona majibu ya Biblia.
Roho Waovu Ni Nani?
Mapema kabla ya kuwaumba wanadamu, Yehova aliumba wana wa Mungu wa roho huko mbinguni, wenye akili na walio wengi sana. (Ayubu 38:4, 7) Kama wanadamu, wao pia wana uhuru wa kuchagua, na kwa muda mrefu walikuwa washikamanifu kwa Mungu. Lakini kwa ghafula hali hiyo ya furaha ilikatizwa. Jinsi gani?
Baada ya Mungu kuwaumba wanadamu, kiumbe mmoja wa roho alianza kutamani kitu ambacho hakikuwa chake ibada. Kama vile mtu mwenye ustadi anavyoweza kufanya ionekane kana kwamba sauti inatoka katika mwanasesere, malaika huyo mwovu alitumia nyoka kumshawishi mwanamke wa kwanza, Hawa, asimtii Muumba wake. (Mwanzo 3:1-6) Biblia inamtaja malaika huyo mwasi kuwa yule nyoka wa zamani, yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani. (Ufunuo 12:9) Yesu alimtaja kuwa muuaji ambaye hakusimama imara katika kweli, halafu akaongeza hivi: Anaposema uwongo, yeye husema kulingana na mwelekeo wake mwenyewe, kwa sababu yeye ni mwongo na ndiye baba ya uwongo.Yohana 8:44.
Baadaye, wana wengine wa roho wa Mungu wa kweli walijiunga katika uasi huo wa Shetani. (Mwanzo 6:1, 2) Wanajulikana kama wale malaika waliofanya dhambi na wale malaika ambao hawakubaki mahali pao pa kwanza bali wakayaacha makao yao wenyewe yanayofaa, au mahali pao walipogawiwa huko mbinguni. (2 Petro 2:4; Yuda 6) Wakaja kujulikana kama roho waovu. (Yakobo 2:19) Zaidi ya hilo, wameazimia kuwaondoa watu wengi iwezekanavyo kutoka kwenye ibada ya kweli, kama vile tu walivyowafanya Waisraeli katika nyakati za Biblia. (Kumbukumbu la Torati 32:16, 17) Vivyo hivyo leo pia, kama vile ilivyokuwa nyakati zilizopita, Shetani pamoja na roho waovu hutumia ujanja kufundisha uwongo wa kidini.2 Wakorintho 11:14, 15.
Jilinde!
Hata ingawa roho waovu wana nguvu zinazopita zile za wanadamu, kupitia msaada wa Mungu, tunaweza kuchukua msimamo kuwapinga na kuwa washindi. (1 Petro 5:9) Hata hivyo, ili kupata msaada huo, tunahitaji kujifunza yale ambayo Mungu anataka tufanye na kutenda kupatana nayo. Akizungumza kuhusu Wakristo walioishi wakati wake, mtume Paulo aliandika hivi: Sisi . . . hatujaacha kusali kwa ajili yenu na kuomba kwamba mjazwe ujuzi sahihi wa mapenzi yake katika hekima yote na utambuzi wa kiroho, ili mtembee kwa kumstahili Yehova kwa kusudi la kumpendeza yeye kikamili.Wakolosai 1:9, 10.
Wale ambao walipata ujuzi huo sahihi walitia ndani watu kadhaa kutoka jiji la Efeso ambao walifanya uchawi. Ona jinsi ujuzi kuhusu kweli ulivyowasaidia. Biblia inasema hivi: Hesabu kubwa ya wale wa