Msaada: Nitapambana vipi na Mchawi?

Msaada: Nitapambana vipi na Mchawi?

Bila ya wewe ku define ajabu inawezekana tusielewane kwa kuwa tunaongelea vitu viwili tofauti.

Naomba unipe link ya hapo nilipopinga kuwepo maajabu nione nimepinga vipi kwa maneno yangu mwenyewe.

Mada ili inahusu "Dunia na maajabu yake"

https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/756250-dunia-na-maajabu-yake-4.html
 
Biblia yasema "HAPANA UCHAWI WALA UGANGA JUU YA ISRAELI.
[HESABU 23:23]
Una damu ya Yesu ya kumshinda mchawi (Shetani) ?
 
Biblia yasema "HAPANA UCHAWI WALA UGANGA JUU YA ISRAELI.
[HESABU 23:23]
Una damu ya Yesu ya kumshinda mchawi (Shetani) ?
Amen Mtumishi. Dawa ya hao ni Yesu Kristo.

WAPIGE KWA MOTO WA JINA LA YESU KRISTO MASHETANI WOTE WANAOHARIBU MAWAZO, Omba maombi haya.

Kwa mamlaka ya Jina la YESU KRISTO mwana wa MUNGU aliye hai ninawashia moto mashetani wote mnaoniletea mawazo mabaya kwenye akili yangu, mnaopindisha mawazo yangu ambayo MUNGU ameniwekea kwa jina la YESU KRISTO . Ninawasha moto kwa mashetani yote yanayonijia kupindisha njia zangu kwa damu ya mwana kondoo, kuanzia leo mimi sio maskini kwa jina la YESU KRISTO. Imeandikwa; "mwana wa MUNGU alidhihiriswa ili azivunjee kazi za ibilisi kuzimu," Ninazivunjavunja kazi zote za kuzimu kwa jina la YESU KRISTO, mnaopindisha mawazo ya maendeleo yangu ninawafyeka kwa upanga wa KRISTO. Katika jina la YESU enyi jeshi la mashetani mliotumwa kuja kuniletea matatizo kwenye maisha yangu ninawatetekeza kwa moto wa MUNGU aliye hai.

Imeandikwa, "neno la MUNGU ni moto ulao." Ninawateketeza mashetani wote mliotumwa na waganga wa kienyeji, wachawi mmetokea kuzimu ninawateketeza kwa moto wa Mungu kwa jina la YESU KRISTO.

Asante BWANA YESU kwa kunipa ushindi mkuu.

Ni katika jina la MUNGU BABA, MUNGU MWANA na MUNGU ROHO MTAKATIFU nimeomba. Amen.
 
MWITE SHUJAA WA MSALABA YESU KRISTO KWA MAOMBI HAYA NA UTASHINDA

Tunawafuata adui zetu palepale walipo, tunawatokea kwenye ulimwengu wa Roho na kuwakanyaga na kuwanyanganya mali zetu na vitu vyetu vyote kwa nguvu ya msalaba wa YESU KRISTO . Kwa jina la YESU nimepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na nguvu zote za yule adui kwa jina la YESU. Kwa nguvu ya msalaba ninawafuata wachawi, waganga wa kienyeji na adui zangu wote katika ulimwengu wa roho waliokaa kikao kinyume na mimi, ninawaponda vichwa kwa jina la YESU KRISTO. Imeandikwa wakamshinda kwa damu ya mwanakondoo, ninawashinda kwa damu ya YESU KRISTO.

Ninazikanyaga mamlaka zote za giza kwa damu ya mwanakondoo. Kwa nguvu ya msalaba, kwa damu ya mwanakondoo ninawashambulia wote mnaotumia baraka yangu, ninauponda uzao wa joka katika jina la YESU KRISTO. Ninawashambulia mashetani katikati ya uzao wa wanadamu kwa jina la ESU. Kwa damu ya mwanakondoo, ninavifuatilia vipawa vyangu vilivyofichwa katika mashimo kwa jina la YESU.

Ninaitumia nguvu ya msalaba kwa jina la YESU KRISTO, waliofichwa kwenye mashimo, kwenye mapori, baharini, kwenye mwezi, kwenye, kwenye anga ninawarudisha kwa damu ya YESU KRISTO. Kwa jina la YESU KRISTO ninaamuru warudishwe, natumia nguvu ya msalaba kwa damu ya YESU KRISTO, biashara zilizofungwa, kazi zilizofungwa ninazifungua kwa jina la YESU KRISTO. Nakwenda msalabani, msalaba wa furaha, msalaba wa ukombozi, msalaba wa ushindi, msalaba wa nguvu, msalaba wa maarifa nakata rufaa hapo kwa jina la YESU KRISTO.

Asante BWANA YESU kwa ajili ya kunifia msalabani, asante kwa ajili ya nguvu iliyomo ndani ya msalaba. Asante kwa ukombozi, uponyaji na msamaha wako.

Ni katika jina la YESU KRISTO nimeomba .
Amen.
 
Dawa ni Yesu Kristo Wa Nazareth aliye hai...

Yesu aliyemfufua Lazaro na ambaye kuzimu na mizimu ilitetemeka kwaajili yake....

Mwite Yesu atakusaidia....

CC: Eiyer Ntuzu Mkuu wa chuo

Ni kweli mkuu hakuna kama Yesu Kristo, kuna sala moja mkuu Telefunken amemuelekeza jinsi ya kuvunjilia mbali nguvu za giza... Damu ya Yesu hakuna inachoshindwa...
 
Last edited by a moderator:
Mwambie Yesu Kristo ambaye ni Mungu Mkuu.

Curse those demons in the Name of Jesus. Rebuke the diabolical powers in the name of Jesus.

HEBU FANYA HAYA MAOBI YA KUSARAMBATISHA UCHAWI


Baba katika Jina la Yesu.


Laana zote nilizo tupiwa na wabaya wangu zimeshindwa kwa jina la Yesu na nazivunja na kuzisambaratisha kwa Damu ya Yesu. Mshindwe wote mnao tuma laana kwangu katika Jina la La Yesu.


Nawavunja na kuwaharibu na kuwakatakata Wachawi wote kwa damu ya Yesu.


Nasambaratisha kila neno la uovu lililosemwa juu yangu na familayangu katika jina la Yesu.


Naharibu na kuisambaratisha madhabahu yenu mliyo fanyia kafara kwa damu ya Yesu.


Navunjavunja na kubomoa kila uovu na uchawi mnaonifanyia katika jina la Yesu.


Nairudisha misukule yote na majini yote yawarudie nyie na kuwalipa dhambi zote mnazo fanya katika jina la Yesu.


Naharibu kila uchawi, kila urogi, kila ndumba kila aina ya uovu ambao mnaufanya ili uniumize mimi na familia yangu katika jina la Yesu.


Nawateketeza kupitia damu ya Yesu Wachawi wote walio tumiwa kunitumia uchawi katika jina la Yesu.


Nawateketeza na kuwaharibu majini yote yaliyo tumwa kuja kufanya kazi hiyo waliyo tumwa na Wachawi katika jina la Yesu.


Nawateketeza na kuwauwa Makuhani wote ambao walienda kunishitaki kwa Wachawi ili waniharibie maisha, nawateketeza kupitia damu ya Yesu. Nawachoma kwa Moto wa Roho Mtakatifu katika Jina la Yesu.


Nateketeza aina zote za vyombo vya kichawi vilivyo tumiwa kuja kunichunguza katika jina la Yesu.


Naharibu fikra zao zote ambazo wanazitumia kufanya kazi zao za kichawi katika jina la Yesu.


Nafuta kumbukumbu zoote zangu ambazo wamewapa Mashetani, Majini, Roho chafu, nafuta hizo kumbukumbu kwa kutumia damu ya Yesu, katika jina la Yesu aliye hai.


Nawateketeza waweka kumbukumbu wa kimashetani kupitia damu ya Yesu aliye hai. Naharaibu na kuchoma kupitia moto wa Roho Mtakatifu makabrasha yote yenye kumbukumbu zangu katika jina la Yesu.


Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuharibu maisha yangu na ubomoa kupitia damu ya Yesu.


Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuniua nauvunja na kuuteketeza kupitia damu ya Yesu.


Kila uchawi ulio fanywa ili kuja kuiba mali zangu, nauvunja na kuubomoa na kuuharibu kupitia damu ya Yesu.


Kila uchawi ulio fanya kuja kuniharibia familia yangu, nausambaratisha na kuuvunja na kuubomoa katika jina la Yesu.


Kila neno la kichawi lililo tumwa ili kuja kuniharibia, kunidhihaki, kunitendea mabaya nalirudisha kwa aliye lituma katika jina la Yesu.


Kila uovu, uchawi, wanga, ndumba, ramli, yaliyo tumwa kuja kwangu navunja yote hayo kupitia damu ya Yesu na katika Jina la Yesu.


Nyota yangu ambayo wanaita nairudisha kupitia damu ya Yesu. Nyota yangu ya baraka nailinda na kuzungushia na kuizingira na damu ya Mwana Kondoo katika jina la Yesu.


Namteketeza yule mtu aliye kuja kuiba nyota yangu katika jina la Yesu.


Nateketeza mbinu zote wanazo tumia ili kuja kuiba nyota yangu katika jina la Yesu.


Nateketeza wivu wao, chuki yao, laana zao, maovu yao na kila aina ya uchafu ambao wanao kwa ajili yangu katika jina la Yesu.


Naizungushia na kuizingira nyumba yangu na damu ya Yesu.


Naishungushia na kuizingira familia yangu na damu ya Yesu.


Nashungushia na kuzingira maisha yangu yote na damu ya Yesu.


Navunja laana zote zilizo semwa na mabau zangu katika jina la Yesu.


Navunja laana zato ambazo zilisemwa bila ya mimi kufahamu, nazivunja na kuziharibu kupitia damu ya Yesu na katika jina la Yesu.


Narudisha kila mali walizo ziiba kutoka kwangu katika jina la Yesu.


Narudisha kila baraka walizo ziiba kwangu katika jina la Yesu.


Narudisha amani na upendo katika familia yangu.


Damu ya Yesu ipo juu ya Maisha yangu na inasafisha kila uovu, kila uchawi unaaribiwa na damu ya Yesu katika jina la Yesu.


Leo hii mtaiona Nguvu iliyopo katika damu ya Yesu.


Katika Jina la Yesu aliye hai ninaomba.


Amen
Amina.. nimebarikiwa sana
 
Back
Top Bottom