Msaada: Mwanangu amekuwa addicted na catoon (katuni)

Msaada: Mwanangu amekuwa addicted na catoon (katuni)

Du miaka 5 unampa Home work
Hata chekechea hawawapi hivyo ngoja afike STD IV au V
mpe katuni za aina nyingi mfano za Lugha ya Kiingereza Boomerang, CT Catoon mbona zinamafunzo mengi na atakuwa mwepesi wa lugha kuliko Comedian za akina Joti

mmhh!
na yawezekana alianza kumpa homework akiwa hata na miaka 2 au 3
 
Bora cartoon addicted kuliko wa game addicted atajuta
 
mpatie katuni zenye mafunzo.

Sio siku nzima, mpangie muda maalum, ikiwezekana muwekee ratiba ukutani na hakikisha anaifuata
 
Mchape muelimishe juu ya mila na desturi zetu za kiafrica tatizo la wazazi wengi mnawafundisha watoto mila na desturi za nje ya africa huko nikuiga kunya kwa tembo jielimishe ww kisha watoto wafuate nyao zako
 
Nakumbuka baba yangu alikua anachomoa vitu kwenye tv haifanyi kazi.... Mpaka nakua ndo ananisimulia alivyokua anafanya..ili tv isiwake.... You can do this also if you deemed it fit.
 
KINACHO TUPONZA WAZAZI wa kileo tuna act tunawapenda sana watoto wetu sana
aiwezekani mtu uangalie tv tangu asubuhi,hivi wewe mzazi uwezi zima tv na kupiga marufuku mtu yeyote kuwasha?
usasa unatuharibu uwezi weka tv chumbani kwa mtoto eti ni kwenda na wakati hiyo aiwezekani.
suluhisho panga mda wa mwanao kuangalia tv na kuna aina ya katuni tom and jerry sawa na zile za wanyama wa kawaida
but kumruhusu kuangalia zombi una mpa rho za kishetani mwanao
mwenye masio na asike

Haswaaaaaaaaa
Kingine ni malezi ya dada wa kazi...yeye anaona akimwekea tv mtoto hamsumbui kumbe hajui anaharibika

Cha ajabu wazazi wanadhani wakiishi miezi 2 bila tv watapungua uzito?

Chujua tv tia kwenye box hifadhi huko mbali miezi 2 na umoangie ratiba uone kama atalilia tv.... pia tuwe wakali kiasi enzi zile mie nakumbuka ukijiliza unapigwa jicho tu unafuta mchozi...siku hizi mapenzi kwa wanetu yamezidi
 
Haswaaaaaaaaa
Kingine ni malezi ya dada wa kazi...yeye anaona akimwekea tv mtoto hamsumbui kumbe hajui anaharibika

Cha ajabu wazazi wanadhani wakiishi miezi 2 bila tv watapungua uzito?

Chujua tv tia kwenye box hifadhi huko mbali miezi 2 na umoangie ratiba uone kama atalilia tv.... pia tuwe wakali kiasi enzi zile mie nakumbuka ukijiliza unapigwa jicho tu unafuta mchozi...siku hizi mapenzi kwa wanetu yamezidi

Dah kweli id yako imeenda sawa na ulivyo...
 
It is dangerous to own a TV set when you are raising kids.

Jaribu umwekee ratiba ya muda na vipindi vya kuangalia. Muda mwingine zima TV kabisa.

Baada ya muda atazoea na ataelewa muda gani wa TV.
 
Mtoto umleavyo ndvyo akuavyo wahenga walisema. Wewe unamfungulia katuni muda wote na unaridika? Eti ukizima TV ni kilio mtindo mmoja? Wewe unaogopa mtoto kulia? Mchelea mwana kulia ulia yeye wahenga walisema pia, kwa hiyo unafikiri alia anakufa au anapatwa na madhara. Mpe kwanza elimu kuliko kumfungulia makatuni hayo, mbona elimu ya mtoto wa umri huo ni nzuri, unamtafutia vitabu vizuri vya hadithi za watoto unakaa naye na kumsimulia mpaka mwenyewe anafurahi. Unampangia muda wa kuangalia katuni na atazoea tu. Acha alie na ukiona anandekeza kulia lia kuwa mkali. Wahenga walisema na hata vitabu vya dini vinatuhasa tusimnyime mtoto fimbo. "Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; bali yeye ampendaye humrudi mapema. … Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali. … Usimnyime mtoto wako mapigo; maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. Utampiga kwa fimbo, na kumwokoa nafasi yake na Kuzimu. … Fimbo na maonyo hutia hekima; bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye (Mithali 13:24; 22:15; 23:13-14; 29:15).
Kwa hiyo sikwambii umwadhibu mtoto wako anapong'ang'ania luninga kuona TV ila nakwambia mfunze na mpangie muda na hakikisha anakubaliana nao, wewe ndiye unaweza kumpangia siyo kila anachotaka anajipangia
Salama wakuu!

Mimi nina mtoto wa miaka 5 mtoto huyu anapenda sana katuni anaweza kuangalia katuni asubuhi mpaka jioni bila kuchoka

Na ikitokea ukizima Tv ni kilio mtindo mmoja mpaka uwashe

Kuhusu shule anasoma chekechea na huwa nikimpaga home work natumia nguvu za ziada sababu ya katuni

Je kuangalia katuni kwa masaa mengi kunaweza kumwadhiri?

Au katuni zinaweza kumjengea uwezo zaidi?

Naombeni kueleweshwa wanajamvi natarajia majibu mazuri kutoka kwenu
 
TV is very very harmful my friend.

However the damage has been done, no use reprimanding you.

Now you need to be stern. It may seem a little harsh but the earlier the better.

1. Weka time limit ya mda wa kuangalia TV. If it is for one hour then stick to this. say 3 to 4 is okay time since jua bado kali.4 to 6 atoke ndani ya nyumba akacheze na agemates zake. 6 to 7 muda wTa kuoga na kusoma kidogo.

2.Monitor your househelps. Wafanyikazi wa ndani waache kutumia TV kama baby sitter ili wapunguze muda wa kuwaangalia watoto wao wapate kupiga domo na kufanya mengine. How you achieve this is up to you.

3,Ongea na mwanao na jaribu kumpa reasoning ya kwanini the world does not revolve around TV. Anza na wewe mwenyewe kumuonyesha kuwa haina umuhimu wa hivyo kwa kuji restrict kuitizama muda wote unapokuwa nyumbani.

Of course it aint easy but like I said earlier, the earlier you cure this addiction, the better.

Good Luck.
 
Haya ni mambo ya nyakati. Kuyaondoa ni ngumu; labda kupunguza damage. Mimi wa kwangu kazi kubadilisha tu, mara cartoon kwenye tv; akichoka hapo mbio kwenye computer games. Lakini naamini watoto wanabadilika tabia; sio kama watu wazima.

Huyo anayesema wazungu hawaangalii katuni, hajui asemalo. Kama ni rate ya kuangalia tv, sisi watitu ni asilimia 10 tu; wakati wazungu ni zaidi ya 85%. Nenda ughaibuni ukashuhudie mambo.
 
Achana naye huyo dogo ale raha duniani. We kama hukuangalia katuni ukiwa mdogo usimbanie dogo. KAMA UNAMWOGOPA AKILILIA KATUNI KWA NINI UOGOPE MADHARA YA KATUNI KWAKE??.
By the way tangu akiwa mdngo ulikuwa unaondoka unamwacha kalala, unarudi unamkuta kalala-hujui katuni hizo ndo anaona kama mamake??
 
Swali dogo wewe kama mzazi mwenzangu ni kwamba ujiulize ulikotoka na ulipo je inaridhisha? Je ni kwa malezi yapi uliyoyapata yakakufikisha hapo ulipo? Kama hayakuridhishi je ni mpango upi ulionao juu ya kizazi chako? Usitengenezewe jinsi ya kulea mwanao wewe mwenyewe angalia malezi uliyoyapata yaliyofaa na yale uliyoyakosa yaliyofaa ongeza kwa mwanao. Lakini sijui kusema hili lile ni vigumu sana kumbuka akili ya kibinaadamu huenda na vinasaba yaani genes kwa hiyo wewe na mwanao hamna tofauti kubwa sana kitabia kana kwamba hutokea wakati mtoto akavumbua tabia zake kutokana na malezi ya kukalilishwa, fulani anafanya hivi na vile na mimi pia nifanye, sijui mwanasaikolojia kaniambia hivi hebu chukua ushauri kutoka kwa mwanasaikolojia aliyesomea China na nenda kwa aliyesomea India harafu uniambie tofauti utakazo zipata harafu jiulize kwanini?
 
Wow, nimepitia comments zote na nyingi zinafurahisha, zingine zinachekesha, zingine zinasikitisha. nashukuru sana mawaidha ya Faizafox. Mimi nilishamaliza malezi ya watoto wadogo niko kwenye malezi ya watoto wakubwa (believe me it is also a challenge)

Katuni ni nzuri sana ila unatakiwa kujua ni aina zipi aziangalie. Kuna Nursery rhymes, alphabet, numeracy, science, geography, life skills, etc. Kwa mfano, kuna cartoons za "Going to market" au going to hospital, at the police station, visiting a farm, etc, etc, ..... Ukizichagua vizuri unaweza usihitaji kumpeleka "tuition".

Kikubwa kilichokuwa kinanisumbua ni uwiano mbaya wa kinachofundishwa huko chekechea (usually horrible, hasa kwa sisi tusioweza kupeleka watoto kwenye shule za uhakika) na ideal situation inayoonyeshwa kwenye video. Walimu ni wabaya, wasiojua kufundisha, kiingereza kibovu, etc. Hata hizi wanazoita academy ni tatizo. Ole wako mwanao awe anafundishwa na mhindi halafu unampa kanda za England. Atachanganyikiwa kwenye pronounciation.

Pamoja na hizo cartoons, mzoeshe kuangalia documentaries hasa za wildlife, history, arts and cultures. Mara nyingi ukiwa karibu na mwanao unakuwa ndio "role model" kwa hiyo unachopenda wewe anajitahidi kukipenda. Jitahidi uwe unafuatilia vitu vya muhimu ambavyo unafikiri vitamjenga kwenye all spheres of child development. Of utmost importance, ni kupata muda wa kumjengea uwezo wa ku-interact na watu halisi. Mazungumzo ya kifamilia, kwenda kwenye bustani au shambani, ujijengee utaratibu wa "technology free hour" ili muweze kuzungumza pamoja, hasa wakati wa chakula, kufua, kufagia mazingira, etc.

naomba niishie kapa kwa sasa.
 
Du miaka 5 unampa Home work
Hata chekechea hawawapi hivyo ngoja afike STD IV au V
mpe katuni za aina nyingi mfano za Lugha ya Kiingereza Boomerang, CT Catoon mbona zinamafunzo mengi na atakuwa mwepesi wa lugha kuliko Comedian za akina Joti
Kwani homework ni nini kaka???!!!
 
Salama wakuu!

Mimi nina mtoto wa miaka 5 mtoto huyu anapenda sana katuni anaweza kuangalia katuni asubuhi mpaka jioni bila kuchoka

Na ikitokea ukizima Tv ni kilio mtindo mmoja mpaka uwashe

Kuhusu shule anasoma chekechea na huwa nikimpaga home work natumia nguvu za ziada sababu ya katuni

Je kuangalia katuni kwa masaa mengi kunaweza kumwadhiri?

Au katuni zinaweza kumjengea uwezo zaidi?

Naombeni kueleweshwa wanajamvi natarajia majibu mazuri kutoka kwenu
Pamoja na kwamba hujaeleza ni katuni series ipi mtoto anatezama(kuna Tom and Jerry, The Flints etc)huo umri ni umri unaoitwa kitaalamu 'formative' yaani ni umri wa kujenga mustakabali wake wa maisha ya baadaye.
Hicho kitu ambacho wewe unaita 'addiction' ni kitu kilichoko kwenye nafsi ya mtoto kilichokubaliana na kuvutiwa na katuni. Kuna uwezekano mkubwa katuni hizo zimeamsha kipaji fulani alicho nacho mtoto. Kuna uwezekano mtoto ana vipaji vifuatavyo:
1.Kuigiza na ubunifu wa mizaha ya kuchekesha
2.Uchoraji na kupamba
Vipaji hivi vitajitokeza na kudhihirika atakapofikia umri wa miaka 7+.Dalili zake ni mtoto kuwa mtundu sana kwa kufanya 'vitu visivyoeleweka'

Kwa sasa mchanganyie katuni aina tofauti zenye mafundisho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom