King Kong III
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 51,672
- 68,644
Bei zinatofautiana sana kwa sababu zifuatazo. Ubora wa miche, location na muuzaji mwenyewe alivyoipata. Jana nimenunua Tabata Aroma pale, bei ni Tsh 1000/ kwa mche, nikaacha kununua Mbagala mwisho pale jamaa anauza 500/ kwa mche sababu ya ubora. Pia niliacha kununua Mkuranga mjini kwa sababu ya bei kuwa kubwa, ni Sh 3000/ kwa mche. Wastani wa bei ni Tsh 400/ mpaka 4000/ kwa mche.
Pia waweza tumia cuttings, kila cutting moja huuzwa Tsh 200/ na inasafirishwa toka Tanga. Hii njia ni nzuri kama una large scale na mvua zipo. Ila kwa mwaka huu mvua ni magumashi, usijaribu labda huko Tanga ambako mvua ziko.
Malila unaweza nijuza mbagala na aroma maeneo gani yenye miche ya mitiki, nataka ninunue kama mia mbili hivi.