Msaada: Mpenzi mpya kazira nifanyaje?

Msaada: Mpenzi mpya kazira nifanyaje?

Habari wapendwa.
Hapa Niko kwenye kizingumkuti sielewi nifanyaje. Kuna mwanaume amekuwa akinitafuta kwa muda mrefu baadaye nikamkubalia lakini akawa anaishi Dar na Mimi Niko Mbeya, HV karibu ni kama wiki hivi akaniambia unakuja Mbeya ili tufanye makubaliano vizuri maana tokea namkubalia hatujakutana tupange mikakati ya maisha yetu ya mapenzi. Jana Ijumaa kakwea pipa kutoka Dar kuja Mbeya kwa dhumuni hilo kwamba atakaa ijumaa,jumamosi na kugeuza Dar siku ya Jumapili.
Ukiwa njiani nilimuomba nije kumpokea nikiwa na rafiki yangu wa kike akakubali.
Alipofika muda wa SAA kumi na mbili kasoro tulimpokea vizuri na kumpeleka kwenye hotel ambayo nilimfanyia booking na alipopumzika km dk kumi tukatoka nae kwenda sehemu ya kula ambayo iko mbali kidogo na hapo alipofikia. Tulikaa hapo hadi SAA tatu usiku tukiwa na rafiki yangu na hakuna maongezi yoyote ya Mimi na yeye yaliyoendelea pale.
Baada ya hapo tayari usiku tulimuaga kuondoka ili na yeye akapumzike alipofikia akaanza kukataa akitaka nikakutane nae kimwili, nikakataa kwa kuwa nyumbani si kuwa nimeaga na bado sio makubaliano yetu kufika na kuanzia Kudo kabla hatijaongea chochote kilichomleta.
Alikuwa serious kunitaka nikalale nae ili hali sina wazo wala kujua kuwa kaka kwa hilo so si kujiandaa kuaga nyumbani kuwa sintarudi hivyo nilimsihi asibiri kesho yake ndo tutajua vizuri kama nitalala nae au la.
Alikubali tukaondoka na rafiki yangu, na kwa kuwa ilikuwa usiku nilimsihi rafiki yangu anisindikize nyumbani ili wazazi wasiwe na maswali mengi juu ya kuchelewa kurudi.
Cha kushangaza baada tu ya kuachana jamaa alibadilisha mawazo kuwa anaondoka kesho yake kabla hata hatujapngea chochote kilichomleta Mbeya kisa nimemnyima mchezo.
sasa naomba ushauri; Je huyu ni mwanaume nzuri wa future kweli kama kasusa kisa kukosa mchezo ambao hata haukuwepo kwenye makubaliano yetu?
Je ,ananipenda kwa that?
Nini haswa kilichomkwaza hadi akasusa akaamua kuondoka kabla azma yake haijatimia?
Je nimfuate Dar tukayajenge huko????
ASANTENI IN ADVANCE KWA USHAURI
Naamin mpaka hapo we si bikra, we ungeendelea tu kubet kama ulivyofanya kwa wengine. Unaona sasa unaanza kujuta kwa kitu ambacho hamtumii EFD machine.
 
ndoa na sex ni vitu viwili tofauti! huyo wa zamani haukuwayi sex naye? mtu kutoka ku fly toka DSM alitegemea toka kwako zaidi ya sex!!!
 
wewe kiboko arudishiwe na nauli
Yeah, si bora mtu angeenda mwanza akarudi na sato kuliko mbeya kaambulia baridi.
Nyie nao wadada mnapishana na bahati, mwanaume mwenyewe wa dar asingezid bao 2.
Shauri yake huyo mdada aeendelee kupigwa shombo za wasafa na wanyaki wenzie.
 
Yeah, si bora mtu angeenda mwanza akarudi na sato kuliko mbeya kaambulia baridi.
Nyie nao wadada mnapishana na bahati, mwanaume mwenyewe wa dar asingezid bao 2.
Shauri yake huyo mdada aeendelee kupigwa shombo za wasafa na wanyaki wenzie.
ha ha haah yaan ww unaonekana ungedai kabisa
 
dawa yenu kuja na rafiki kama hivyo
Sema jamaa alibugi, ange act hali ya hewa inamsumbua akamwagiza mwenyeji wake akamchukulie dawa then fasta achukue no ya shosti ake. Ile anazingua tu, angeona mashoti walivyo na huruma. Asingelala kavu.
 
wala usimfate dar maana atakupa mimba na ataruka mita mia na utakuja hapa jf kuomba ushauri na Bahati mbaya Siku hiyo sitokuwa na bundle ya kukupa ushauri.

hivi alitaka sex kwa misingi IPI?

mulisha Pima afya? wanaume wengine majanga.

asikutishe kwa kupanda pipa dar to mbeya. watu wanatoka kwa trump mpaka hapa na papuchi hawapati kirahisi hivyo sembuse huyo???
 
Tanya hebu nenda na wakati

Wanaume wa kupanda ndege dar to mbeya kuja tuu kuongea bila kula papuchi last seen yao ilikua kipindi cha kina Nuhu
Aiseee umenigusa uvungu wa moyo wangu. Hata niwe mvumilivu kiasi gani siwezi kwea pipa halafu nilale peke yangu. Istoshe Mbeya na baridi lile
 
Don't regret kama ni wa kwako atarudi tu, kuwa wazi kwake na msimamo wako wa kutofanya nae mapenzi sasa hivi,na asiporudi pia don't feel bad ukute hakuwa na malengo na wewe,na haukuwa mpango wa mungu uwe nae
 
Sema jamaa alibugi, ange act hali ya hewa inamsumbua akamwagiza mwenyeji wake akamchukulie dawa then fasta achukue no ya shosti ake. Ile anazingua tu, angeona mashoti walivyo na huruma. Asingelala kavu.
 
hahaaa... Dar to Mbeya et amekuja mpange mipango bora ungemchana laivu kwa simu asije...Ushauri wangu usije ukajiroga ukaenda Dar atapiga gemu la hasira na kupita milango yote au akutoe collabo kulipia cost zke
 
Habari wapendwa.
Hapa Niko kwenye kizingumkuti sielewi nifanyaje. Kuna mwanaume amekuwa akinitafuta kwa muda mrefu baadaye nikamkubalia lakini akawa anaishi Dar na Mimi Niko Mbeya, HV karibu ni kama wiki hivi akaniambia unakuja Mbeya ili tufanye makubaliano vizuri maana tokea namkubalia hatujakutana tupange mikakati ya maisha yetu ya mapenzi. Jana Ijumaa kakwea pipa kutoka Dar kuja Mbeya kwa dhumuni hilo kwamba atakaa ijumaa,jumamosi na kugeuza Dar siku ya Jumapili.
Ukiwa njiani nilimuomba nije kumpokea nikiwa na rafiki yangu wa kike akakubali.
Alipofika muda wa SAA kumi na mbili kasoro tulimpokea vizuri na kumpeleka kwenye hotel ambayo nilimfanyia booking na alipopumzika km dk kumi tukatoka nae kwenda sehemu ya kula ambayo iko mbali kidogo na hapo alipofikia. Tulikaa hapo hadi SAA tatu usiku tukiwa na rafiki yangu na hakuna maongezi yoyote ya Mimi na yeye yaliyoendelea pale.
Baada ya hapo tayari usiku tulimuaga kuondoka ili na yeye akapumzike alipofikia akaanza kukataa akitaka nikakutane nae kimwili, nikakataa kwa kuwa nyumbani si kuwa nimeaga na bado sio makubaliano yetu kufika na kuanzia Kudo kabla hatijaongea chochote kilichomleta.
Alikuwa serious kunitaka nikalale nae ili hali sina wazo wala kujua kuwa kaka kwa hilo so si kujiandaa kuaga nyumbani kuwa sintarudi hivyo nilimsihi asibiri kesho yake ndo tutajua vizuri kama nitalala nae au la.
Alikubali tukaondoka na rafiki yangu, na kwa kuwa ilikuwa usiku nilimsihi rafiki yangu anisindikize nyumbani ili wazazi wasiwe na maswali mengi juu ya kuchelewa kurudi.
Cha kushangaza baada tu ya kuachana jamaa alibadilisha mawazo kuwa anaondoka kesho yake kabla hata hatujapngea chochote kilichomleta Mbeya kisa nimemnyima mchezo.
sasa naomba ushauri; Je huyu ni mwanaume nzuri wa future kweli kama kasusa kisa kukosa mchezo ambao hata haukuwepo kwenye makubaliano yetu?
Je ,ananipenda kwa that?
Nini haswa kilichomkwaza hadi akasusa akaamua kuondoka kabla azma yake haijatimia?
Je nimfuate Dar tukayajenge huko????
ASANTENI IN ADVANCE KWA USHAURI
Sasa anatest vipi kama unamfaa au la? Hayo mambo ya kubana ya mwaka 47
 
Back
Top Bottom