Kabla sijasoma post za wengine, naomba nichangie kabla kichwa hakijachakachuliwa.
Hapa naona tatizo zaidi ya ulokole.
Wazazi wako wanaweza kuwa wamekuwa na matatizo katoika ndoa yao kwa muda mrefu ambayo hajakupatiwa ufumbuzi.
Labda, kutokana na baba yako kuwa bize, attention ilipungua kwa mama, hii ikamfanya mama kuwa mpweke kwa kipindi kirefu. Lakini alivumilia for the sake ya ndoa.(Mama yako alikuwa na kazi?)
Baada ya mama yako kukutana na rafikiye mwenye matatizo ya kansa (wote wana frustration zao za maisha), wakaungana na kutafuta faraja kwenye ulokole. Na kama ulokole umeweza kujaza gap iliyotengenezwa na baa yako, hakuna jambo mama anaweza kuwaelewa eti aachane na ulokole wake.
Walokole wanachofanya ni kujaza gap iliyosababishwa na matatizo yako, kama huna imani nzuri unaweza kuwa 'brain washed'.
Suluhu ya maumivu ya muda mrefu katika ndoa sio rahisi kuyatibu kijuu juu, imagine tangu miaka ya 80 wameoana it's 30+ years. Kwanza inategemea na uelewa, utayari wa wenza wote wawili. Huwezi mlazimisha mama aelewe, hujui amekuwa akiumia kiasi gani kimya kimya, huwezi mlaumu baba, huwezi jua ni kiasi gani anaamini alikuwa najitoa kwa familia.
Hapa inabidi wewe kijana ukae nao, mtafute chanzo cha mama kujikuta kwenye ulokole mkali kiasi hicho, ndio muanze kufatuta suluhisho. Kumlaumu mama peke yake itaongeza ukubwa wa tatizo. Usiegemee upande wowote, kuwa neutral ili uweze kuona mambo kwa upana wake.
Mungu akutie nguvu usuluhishe wazazi wako.