MSAADA: Mama kabadilika baada ya kuwa Mlokole

MSAADA: Mama kabadilika baada ya kuwa Mlokole

Ofukozi popote wanapoweza saidiwa ku-reason pamoja panafaa kwa muda huu

Ila asianze kunyooshea mtu kidole, Kaunga ndoa ngumu jamani

Bora kwa wanawake wa sasa waliojiwezesha, ila wale wa kale akikumbana na abyusi hasa za kihisia walikuwa wanakufa nazo kimya kimya. Anaogopa kulalamika jamii haitamwelewa, utasikia wanasema 'yaani mmeo anakukumbuka kwa kila kitu afu unalalamika? una lako jambo'

Sijui kama nafasi ya kuridhishana(kufeel uwepo wa mwenzako ndoani) ilikuwa inapewa kipaumbele kivile, mie naona iko complicated sana hii. Haihitaji haraka wala majibu ya juu juu.

Na point ambayo mama ameshafikia anahitaji uelewa zaidi kuliko hukumu, wakimsumbua wanaweza jikuta mama kahama nyumbani anaenda kuishi chumba kimoja, hii ni kiakili zaidi.

Nimeupenda mchanganuo wako, na ndio maana counseling nzuri inatakiwa. Changamoto ni kumfanya huyo mama kwenda au hata kukubali hiyo counseling na ndio maana nikashauri aende kupatiwa hiyo counseling kwa mlokole ambaye kwa maoni yangu huwa ana dig kutafuta root causes ya matatizo mbali mbali.
 
Last edited by a moderator:
Pole Sokwe.. Mama yako anahitaji msaada wa haraka hiyo aina ya ulokole sio kabsaa Mungu hatafutwi kwa vitimbwi hivyo.. Chunguza hilo kanisa, mchungaji, waumin jinsi wanavyo endesha mambo ili ujue pakuanzia kumshaur
 
Imani huja kwa kusikia, na kwa kusikia kutoka katika neno la Mungu. Imani zote, zote uzijuazo, huja kwa kusikia. Ila imani ya Kikriso huja kwa kusikia maneno ya Kristo. Kwa hiyo imani ya kikristo huja kwa kusikia maneno ya Kristo. Imani isiyoendana na neno la Kristo sio imani ya kweli as far as Christianity is concerned. Tatizo leo watu wameweka imani kwa watu badala ya Mungu. Utasikia mtu anasema mimi nasali kwa flani, mimi nasali kwa apostle flani, na anfanya yote ayasemayo postle huyo hata kama ni kinyume na mapenzi na neno la Mungu. Kama tusipokuwa na maarifa, tutaangamia

Nakubaliana na wewe kabisa Iron. Imani haiji kwa sababu ya mtu fulani au mchungaji au padre au sijui mtume, imani inakuja kwa njia ya kumwani Kristo. Na ukiristo siku zote unahubiri upendo. Haitoshi tu kudai kwamba mtu ana imani. Imani ya kweli huambatana na matendo. Yakobo aliandika: “Imani bila matendo imekufa.” (Yakobo 2:26). Mtu anapotenda kwa imani akiwa katika majaribu, anasitawisha sifa ya uvumilivu. Ili kufanikiwa, Mkristo anahitaji kumwomba Mungu ampe hekima, akiwa na imani kwamba Mungu atampa. Uvumilivu humfanya mtu akubaliwe na Mungu. Kama unavyosema ndugu yetu mama alikuwa Mkatoliki basi ningekushauri nenda kama uko Dar es Salaam waone EMMAUS CENTER UBUNGO, DAR ES SALAAM, BEHIND UBUNGO BUS TEMINAL VIA UBUNGO DARAJANI. P. O. Box 76255, Dar Es Salaam. Au anaweza kumwona Fr Baptse Mapunda (Tunda la Kanisa) sina uhakika na spelling la jina lake la kwanza
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa!!!! Mungu hapendi utengano wa familia na inawezekana anapata mafundisho sio ambayo inamfanya ana act kama anavyofundishwa, ila anahitaji amwombe Roho Mtakatifu amwongoze na asome biblia mara kwa mara kwa uongozo wa Roho wa Mungu.
 
Kama ni makanisa haya mapya ya Efatha, Ufufuo na Uzima,mzee wa upako,mito ya baraka na Gwajima mzee wa misukule yaani ni balaa tupu.Kuna mama jirani yetu ameachana na mume wake kwa sababu eti yeye amepewa kuombea nyumba ya Nabii na Mtume Mwingira kwa hiyo huyo mama anaamka asubuhi na mapema kwenda kuhudumia nyumba ya mchungaji anarudi usiku wa manane na siku nyingine analala huko.Kwa hiyo mume wake ameamua kumpiga chini maana sasa kwa kifupi ni kwamba mume wake anaona mke yupo responsible kwa Mwingira kuliko kwa mume wake.Haya makanisa haya mapyamapya yana mambo ndugu zanguni yaani muwe macho sana.
 
Uzoefu kidogo nilio nao ni kwamba mtu anapoingia kwenye 'hizi imani', juhudi zozote mtakazokuwa mnafanya 'kumkomboa' zitapelekea yeye kujichimbia zaidi huko ili 'kukemea roho zenu mbaya'...
Kwa kiasi fulani method ambayo inafanya kazi, ni kuonyesha kumsapoti (sio kwa maneno), bali kwa kuwa karibu nae, kumpenda zaidi, kutumia mda wowote utakaopatikana kustorisha nae, akileta stori za kushawishi uingie ulokoleni, usipinge, msikilize, then kaa kimya, au mwambie aendelee kukuombea ili siku ukifunuliwa uingie humo (kimoyo moyo unajua kuwa hutaingia), nk...
Lengo la kufanya hivi ni kumjengea hali kuwa nyumbani kuna 'kampani', na ni mahali pa furaha kwake. mda si mrefu (atakapopata frustration huko), atapakumbuka nyumbani na 'kurudi kundini.
But mkimtreat kama 'aliyepotea', mjue kwamba atazidi kupotea.
By the way, kwa hali ya kiuchumi nyumbani kwenu, it is likely mama ameenda huko out of frustration za aina fulani. Nyumbaza matajiri mara nyingi watu wako 'bize' na hazina furaha...

Tuko umeeleza vizuri kabisa. Kwa kuongezea kwenye red, makanisa haya yanayojiita ya kiroho yenye watu wanaojiita mitume na manabii yanatumia matatizo ya watu kujiendeleza. Amini usiamini, mtu mzima kuamua kuokoka ujue kuna kitu kiko nye ya uwezo wake kukisolve na anafikiria kanisa ndo kimbilio la mwisho. Hapa kutakuwa na mgogoro wa kifamilia kati ya baba na mama ambao umekuwa na kupelekea mama kuwa frustrated na kutafuta tulizo kanisa. Pia, inaonekana mama hawaamini hata watoto wake kwani matatizo ya wazazi angewaeleza kwa kiai fulani. Sisi tunatua migogoro ya wazazi wetu kwa sababu ni wa wazi kwetu.
 
Nashukuru kwa ushauri wenu wapendwa ila Nina mtihani mgumu, mama yangu alikuwa muumini wa kawaida sana! Sasa tangu ameingia makanisa hayo anarudi vumbi tupu, nikiongea nae kwa simu ni jina la yesu mwanzo mpaka mwisho wa maongezi, hata sielewi kwa kweli, ila nashukuru sana kwa kunitia moyo.
 
Mama yangu Ana miaka 58, inawezekana Ana frustration kwenye ndoa yake siwezi kataa japo sina ushaidi , ila ktk maisha yangu yote sijawahi kuona wazazi wangu wakigombana kwa kweli, sijawahi kuona baba yangu akirudi nyumbani usiku wa manane, amechelewa ni saa 2 usiku na Sio mlevi, ni mtu anayesaidia sana wenye shida na ni mwepesi kusamehe, japokuwa naishi mbali na nyumbani sidhani Kama amebadilika na amekuwa akinisisitiza sana nirudi nyumbani Ili niweze kumsaidia biashara zake kwani amechoka kusafiri.
 

Falsafa mbaya kabisa!


Kama unaamini huyo mama yetu yupo sawa, unaweza kuniambia kwa imani hiyo aliyonayo anamsaidiaje mumewe (ambaye yeye anaamini ni mchawi) ili aachane na uchawi wake kwa kutumia chuki na kujitenga?

Maelezo yako ndio hasa chachu ya mafarakano katika jamii. Mchungaji mwenye ufahamu na maarifa hawezi kumwambia muumini wake aache kutumia dawa na yeye awe anamuombea tu. Nafikiri muanzisha mada ameeleza jinsi rafiki wa mama yake alivyofariki kwa kansa ya ziwa sababu ya imani kama yako.

Yooote ulioandika yanakosa maana kwa jambo moja tu: NDOA YA WATU IKO HATARINI. Mchungaji asiyeweza kumuita mume kanisani na kuliweka mezani suala lao, hana nafasi katika Kristo (upatanishi). Mimi nikiwa mchawi, ndugu zangu hawatanisaidia kwa kunitenga bali kwa kunipenda na kuniombea ili nami nibadilike na kumfuata Mungu kama wao.

Kama mama na mchungaji wake hawana uthubutu wa kumkabili mchawi mmoja kwa maombi na kumshinda, basi nina mashaka na Yesu wao. Baba hakupaswa kuchukiwa (kama inavyodhaniwa mchawi) bali alipaswa kuhuishwa.

Mchungaji HAPASWI kumwambia mama kuwa mumeo ni mchawi. Alichopaswa kufanya ni kumuombea rehema ili kwamba, matatizo ya nyumbani kwake yakome. Katika hali ya Kimungu, baba angeanza kupata shida na yeye mwenyewe angejikiri na kubadilika.

Asante sana Mwana Mtoka Pabaya kwa maelezo yako mazuri na ya kujenga kiimani. Maana huyu mwenzetu alianza kutuposha kwa imani zake za kuamini RC si kanisa la kweli na imani zake za kila kitu ni uchawi au mashetani. Sina maelezo zaidi bali kumwomba mtoa hoja hasifuate maelezo ya huyu Mbetwa
 
Wapendwa wanajf naombeni ushauri, mama yangu ameingia kwenye makanisa ya kilokole japokuwa familia nzima ni wakatoliki, tangu ameingia kwenye makanisa hayo maisha yake yamebadilika sana, hana ukaribu na mumewe yaani baba yetu! Kwa mfano walikuwa wanasali pamoja asubuhi na jioni pamoja sasa haiwezekani tena kwani Ana amini baba yangu ni mchafu! ashirikiani na ndugu zake yaani wajomba na shangazi zetu japokuwa wamefanya jitihada kubwa kujaribu kutafuta muda kuzungumza nae imeshindikana! Kwani anatoka nyumbani saa 11 alfajiri na kurudi usiku.

Baba yetu amekuwa kwenye kipindi kigumu sana kiasi cha kuniomba kuzungumza nae kwani Mimi ni mtoto wa kwanza kwenye familia yetu nimeshindwa kuzungumza nae kwa sasa kwani naishi Japan na familia yote ipo tanzania, natarajia kurudi nyumba kwa likizo fupi mwezi wa 12, kuna kipindi Mdogo wangu alikuwa anasumbuliwa na tumbo akampeleka kwenye maombi akaonekana Ana mapepo yaliyokuwa anadai baba yetu ndie anamloga bwana Mdogo!

Nilipopata taarifa hizo nilishtuka sana nikamuomba Mdogo wangu aende hospital kwa uchunguzi bahati nzuri Nina rafiki yangu tulisoma pamoja ni dr wa matumbo pale muhimbili, baada ya kufanyiwa uchunguzi alionekana na bacteria h. Pylori ambao walisababisha apate ulcers pia, baada ya matibabu amepona kabisa! Baba yangu ni mfanya biashara mkubwa sana na msomi Sio Kwamba najisifia ila ndio ukweli, alifanya kazi kwenye jumuia ya Africa mashariki miaka ya 80, akaamua kuacha kwa hiyari yake na kijiingiza kwenye biashara tangu miaka hiyo, anafanya biashara ulaya na Middle East na marekani, baba yangu anaweza kuwa mchawi?

Japokuwa habari hizi hazijamfikia Kama zikimfikia anaweza akapata heart attack Kama Sio stroke, kuna mama aliyemuintroduce mama yangu kwenye makanisa haya ya kilokole alikwisha fariki na cancer ya ziwa kwani alikataa matibabu ya hospital! Napata Shaka ikitokea mama kuumwa huenda akakataa Kwenda hospital pia au kuficha maradhi yake, poleni kwa post yangu ndefu, naombeni michango yenu.
Ndugu hilo tu ndo linakupa pressure wala usiwaze sana..mbona..kimsingi huyo bi mkubwa wako..anasumbuliwa na kitu kinaitwa wokovu wa mwanzoni..yani kile kiraruraru cha baada ya kuokoka nin na viru kama hivyo ila namsikitikia kimtindo maana kwa jinsi scenario zainavyokwenda obviously ameingia kwenye kanisa chaka..siku hizi imani imekua hatari sana makanisa mengi na design kama vile wameshamteka hivi maaana kama hata ukihudhuria hayo makanisa point ya msingi ni kutoa sadaka na kupanda mbegu..toa pesa inayokuuma etc etc nkt Yesu baba yake ni Mungu lkn alikua anafanya vitu bure..we kama vipi shikilia imani yako haya kila lenye mwanzo lina mwisho..wa mama wengine kumbe wanatafutaga matatizo wenyenyewe sasa..saa 11 alfajiri hadi usiku ndo kusali gani..tafikiri wanataka kuhamisha mlima..!!!
 
Haya mambo yasikie tu kwa watu. Yanaweza kuwavuruga hadi mkasambaratika. Muhimu ni msikubali kutenganishwa hata kidogo. Mtatajwa wachawi mmoja baada ya mwingine hapo. Endeleeni kuongea na mama kwa upendo na mumsaidie majukumu. Muambie dingi, sasa ndo wamefikia stage ya kuchukuliana mizigo kwa upendo. Aendelee kusali na kumuombea mkewe pia kuwa Mungu azidi kumuonyesha upendo wake.

Acheni jamani! Kuna mtu anaenda kulala church 3 days anaacha familia ati!
Yaani inahuzunisha sana kuna mama mmoja alikua anaacha mtotto wa miaka 3 na kwenda kwenye maombi kuanzia asubui mpaka usiku. Na anaporudi anakua hana muda na familia, maana anaingia tena kwenye sala binafsi hapo humtoi. Yaani taratibu nyumba inaanza kufanya ufa . Ni ngumu sana kudeal na watu wa namna hii lkn kama ulivyosema king'asti huu ndio muda wa kuchukuliana mizigo sasa kama familia inabidi wamsaidie kwa upendo.
 
mLETA UZI WEWE NI MUONGO TENA MUONGO MKUBWA, ETI ANATOKA SAA 11 ALFAJIRI NA KURUDI USIKU????!!!! PIA ILI TUWEZE KUKUSAIDIA TAJA NA HILO KANISA MF.KWA MAMA RWAKATARE, GWAJIMA, LUSEKELO, KAKOBE,MTUME NYAGA, GAMANYWA, KATUNZI, NABII FLORA etc.
 
eTI BABA YAKO HAWEZI KUWA MCHAWI KWA KUWA NI MFANYABIASHARA MKUBWA SANA????!!!! ANAFANYA BIASHARA ULAYA, MIDLE EAST NA MAREKANI SO HAWEZI KUWA MCHAWI!!!.
 
bABA YAKO ALIACHA KAZI JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI MIAKA YA 8O, FOR YOUR INFORMATION JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKA ILIVUNJIKA MIAKA YA 7O ENZI NA KENYATA, NYERERE NA NDULI IDD AMINI.
 
sEMA TU HUUPENDI ULOKOLE KWA SABABU HUJUI CHOCHOTE KUHUSU WOKOVU A.K.A KUMPOKEA BWANA YESU KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKO. WE UNGEULIZA TU NN MAANA YA ULOKOLE, UNGEPATA MAJIBU KWA KIREFU!!
 

Falsafa mbaya kabisa!


Mie sijasema kama ni mchawi babake yaliyosema ni mapepo kuwa yametumwa na babake kama nimeelewa vzuri. Mama ndo mana hajamwambia baba direct mpaka saiz kuhusu ilo ila kunavita ya kiroho hapo inaendelea kat ya hao wanandoa.

Narudia tena: TULIZA UFAHAMU WAKO

Kanisa la Kiroho halina kazi ya kuongea na mapepo na kuyauliza yametoka wapi. Pepo anapotolewa hapewi nafasi ya kufungua mdomo kwani atakachofanya ni kufarakanisha watu. Ni kwa mganga ndio pepo huambiwa aongee na sio kwa Yesu.

Labda nikuulize swali: Wewe unaamini maneno yatakayosemwa na pepo?

Ikiwa jibu lako ni NDIO, basi hujui unachoongea. Kama pepo ni msema kweli, ugomvi wetu na yeye wa nini? Ikiwa jibu lako ni HAPANA, kuna haja ya kumsikiliza?

Ninachokiona kwako ni aina ile ile ya Walokole wa Ajabu Ajabu kiimani. Hawa watu wamefarakana wewe unasema vita ya kiroho? Unaijua vita ya kiroho?

Mimi naona kuna vita ya UFAHAMU na wala si vita ya kiroho. Mchungaji mwenye akili timamu, haongei na mapepo. Huyaamuru yatoke na yasirudi tena. Experience zenu na waganga wa kienyeji mnazihamishia kanisani jamani, tunaenda wapi? Pepo ukiongea nalo litawafarakanisha tu.
 
Mama yangu Ana miaka 58, inawezekana Ana frustration kwenye ndoa yake siwezi kataa japo sina ushaidi , ila ktk maisha yangu yote sijawahi kuona wazazi wangu wakigombana kwa kweli, sijawahi kuona baba yangu akirudi nyumbani usiku wa manane, amechelewa ni saa 2 usiku na Sio mlevi, ni mtu anayesaidia sana wenye shida na ni mwepesi kusamehe, japokuwa naishi mbali na nyumbani sidhani Kama amebadilika na amekuwa akinisisitiza sana nirudi nyumbani Ili niweze kumsaidia biashara zake kwani amechoka kusafiri.
Ni kweli mkuu una kazi kubwa, maana unaweza ukawa unadili na moshi na kuuacha moto kwingine. Kitendo cha mama kudiriki kumhusisha baba na "mapepo" ya "mwanae" kinaongea mengi sana kuhusu mahusiano yao. Kwa watu ambao wangekuwa wanaishi kwa amani na upendo, mama angekuwa mtu wa mwisho kumshuku baba kwa mambo ya kushetani. Wewe kama mtoto itakuwia vigumu sana kuchunguza na kujua ukweli ingawa ukitulia ukatumia mbinu 'Sophisticated' kidogo utaupata ukweli. Nina wasiwasi amani uliyokuwa unaiona ilikuwa kwa nje, but kwa ndani kulikuwa na "kansa" ilikuwa inawatafuna kimya kimya, na sasa imefika mahali where mother can't hold it any more!!!
 
Pole na matatizo ukirudi kaa na mama yako usimuogope muulize kiini cha tatizo kilianza lini

Imani zingini ni za kutaka mali ya baba yako

Mwisho ulokole mwingine hamna tofauti na uganga wa jadi
 
mm sina cha kuongeza hapo kwani best umeongea mambo muhimu sana kuhusu huyu ndugu yetu sokwe anachotakiwa akae karibu mama yake, na amhoji lakini kabla hajamhoji afanye uchunguzi kwanza kuwa mama yake ameingia dhehebu la namna gani usijejua kuwa anaabudu mashetani au kajiingiza freemason ikiaina pasipo kujua yeye, kwa sababu wengi wa manabii, mitume wa siku hizi wanatafuta pesa na sio kulisha kondoo wa Bwana, na weingi wao hawana wito wowote wamekaa kimaslahi zaidi hivyo awe makini kwa suala hili kisha ndo aanze mazungumzo na mama yake kwa upendo, natumaini atafanikiwa kama atafuata haya. pole
Lol pole sana huyo mama anahitajia ushaui nasaha aisee. Kuna makanisa kadhaa huwa yanahubiri upotofu kabisa na hii inatokea kwenye familia nyingi zinazoamua kujiingiza kwenye imani hizo. Maana alitakiwa awe na mabadiliko mazuri hasa baada ya kuokoka sasa kama inakua mbaya basi hiyo haitokani na Mungu. Wengi wanautata sana maana wanakua brainwashed na hao wachungaji mara mikesha, mara semina na hasa wakiona huyo ni mambo safi hapo kazi ipo kumng'oa ndugu yangu. Cha msingi Muombe Mungu akupe nafasi na hekima ya kuongea nae na jaribu kufuatilia je anaenda kwenye kanisa gani na mchungaji wake ana historia gani. Fuatiia waumini wanaosali kwenye kanisa hilo wakoje. Maana kuna baadhi ya makanisa waumini wao wamekua kama wamelishwa dawa hivi.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom