Sasa kama unafahamu kuwa kuna miungu na Mungu na mimi ninaye mmoja, kwanini unapingana na akili yako? Kwenye Sentesi yako ya kwanza umekiri kuwa kuna Mungu na infact umesema kuwa :mimi ninaye mungu wangu: Sasa kama unakri mbele ya JF kuwa mimi nina Mungu wangu, kwanini umeamua kupingana na akili yako inayo kiri kuwa mimi ni Mungu wangu?
Kwa sababu mungu anaweza kuwa hadithi tu, na si halisi.
Kwa mfano, unaweza kumkubali Jehovah au Allah kama mungu aliyeumba dunia, wakati katika hali halisi hajaumba dunia.
Kwa hiyo, nikisema kwamba una mungu nitakuwa sijakosea, kwa sababu huyo ndiye mungu unayemkubali. Lakini ukisema kwamba ndiye muumba wa dunia nitakukosoa, kwa sababu huna uthibitisho kwamba kaumba dunia.
Huwezi kusema nimeshindwa mjadala wakati wewe umeshindwa hata kusaidia "MADAI" na zaidi ya hapo nani aliye kupa Uongozi/wenyekiti wa Mjadala? Unaona tatizo ulilo nalo la kujifuraisha halafu unajipa heko mwenye? Hapo unaonyesha udhaifu katika NAFSI yako.
Umeshindwa mjadala kwa sababu umeshindwa kuanza mjadala.
Mjadala wa kumhusu mungu ni lazima uanze na kum define mungu ni nini, jina lake ni nani, na ana tabia gani.
Wewe hujaweza hata kumtaja jina lake wala sifa zake.
Sasa mimi siwezi kuanza kumvunja vunja mungu wako kwa point za kumvunja Apollo wakati sijui mungu wako ni Marduk au Osiris, Jehovah au Allah.
Umejiweka katika hali mbaya ulipo kiri kuwa mimi nina Mungu Wangu. Rejea katika posti yako "sentensi ya kwanza"
i. Nipe ushaidi kuwa mimi ninaye Mungu kama ulivyo kiri kwenye sentensi yako ya kwanza kwenye annexed quote?
ii. Nipe ushaidi kuwa Mungu ana jina kama ulivyo dai kwenye paragraph yako ya pili?
iii. Nipe ushaidi kuwa Mungu anatabia kama ulivyo dai kwenye paragraph yako ya pili?
Mungu yeyote uliyenaye, unaogopa kumtaja na kutupa sifa zake kwa sababu unaogopa atavunjwavunjwa.
Ukiniomba nikupe ushahidi kwamba una mungu wako, ni sawa na kukana kwamba una jungu wako.
What are you trying to say here?
Unakubali kuwapo kwa mungu au unakataa? Anayekubali kuwapo kwa mungu haombi ushahidi kwamba anakubali kuwepo kwa mungu.
The fact kwamba unaomba ushahidi kwamba unaye mungu inaonyesha hata wewe mwenyewe hujielewi kama unakubali kuwepo kwa mungu au hukubali.
Kama ungekuwa Mahakamani na ndio unatoa ushaidi wako, basi elewa kuwa teyari utakuwa umjifunga mwenyeke kwa kukiri kuwa "Plaintiff" Anaye Mungu na wakati huo huo unajipinga mwenyewe kuwa Mungu hayupo huku UKISHINDWA KUTETEA MADAI YAO zaidi ya KUKUBALI KUWA PLAINTIFF ANAYE MUNGU. Rejea kwenye post yako mwenyewe "quoted"
Mahakamani wewe ndiye ungeshindwa utetezi, kwa maana umeulizwa mungu wako ni yupi na ana tabia gani, hujajibu.
Mahakamani kuna kitu kinaitwa "immanet criticism".
Ambayo huenda kwa kuanza kwa kukubali the opposing side's position, only to dismantle it better from within.
Immanent criticism kutoka kwangu kwenda kwako itaanza kwa kukubali "Kama mungu yupo, ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, imekuwaje kaumba ulimwengu wenye maovu na mabaya kama huu?"
Hapo ukisoma bila kuelewa emanent criticism unaweza usielewe kwamba hii sentensi haisemi kwamba mungu yupo, bali inahoji kama mungu yupo
Kwa kisomo zaidi, kama unapenda kusoma, kuhusu immanent criticism soma wiki hii hapa
Immanent critique - Wikipedia, the free encyclopedia
SASA: Tetea madai yako kuwa Mungu hayupo, Unapo tumia bayana ya "KAMA" ni kuonyesha udhaifu wako kuwa wewe umeshindwa kusaidia unacho kifuata zaidi ya kwa BAYANA na tamthilia.
Nishakueleza kwamba ambacho hakipo hakionyesheki kwamba hakipo, kwa sababu hakipo.
Nimekuuliza unithibitishie kwamba juu ya mlima Kilimanjaro hakuna taa ya dhahabu inayozunguka, hujaweza kunithibitishia kwamba haipo, ingawa haipo. Kwa sababu kisichokuwapo hakithibitishiki kwamba hakipo.
On the other hand, vilivyopo vinathibitishika kwamba vipo.
Kwa sababu vipo.
Sasa unadaiwa na watu wote wenye uwezo wa kufikiri na kufuatilia mambo kwa ukaribu zaidi kuonyesha kwamba mungu yupo.
Kwa uthibitisho.
Mpaka sasa hujaweza.