Msaada kiwanja Ku-Date

Msaada kiwanja Ku-Date

H
Unagusa level siyo zako... kama unaanza kusema huna mkwanja basi unakanyaga moto...
Mkuu mtoto wa kiume hatakiwi kukata tamaa, huyu mtoto anaweza kutnitoa kimaisha hapo badae. Mi namjua ila ndo najaribu kuendana na life style lake kwanza.
 
Mtoto natokea majuu, na ni wakishua balaa, Afu natamani maisha anayo ishi ila mi sina uwezo huo. Ila nikimpata nita enjoy sana hela zake na tutashirikiana kimaisha .
Kwao ni hapahapa bongo na nimeshakutana nae mara mbili uso kwa uso ndo nikamuomba contact.

Huu ndo utoto sasa. Kumbe uko after pesa? Hujielewi
 
Hahaha! Sijapata kuona mtu chizi kama wewe.

Usikute walikuwa wanafahamiana kitambo na huyo msichana anarudi zake toka huko India kwa likizo
Kumbe mtoto anatokea India alikua kwenye matibabu Apollo nini?
Itabidi atafute kiwanja chenye kachori, basi aende twoo cc Preta
 
Kama lengo ni kuwa mchumba na baadae umuoe, na huna mkwanja kiivile, nunua nyanya, pilipili hoho, nazi, karoti, vitunguu, mchelele/viazi, matunda, nyama ya ng`ombe/kuku/samaki etc. Pika chakula hapo unapoishi, tengeneza juisi na andaa matunda, umkaribishe mpate chakula. Akipenda anaweza kuja mkapika pamoja huku mkiongea. Mkimaliza kula unaweza kumtembeza mtaani kwenu apajue huku mkiendelea na maongezi. Lakini kama malengo ni kupiga tu mzigo, then nakushauri hata ukakope VIKOBA ili umpeleke sehemu za "kishua". BE REAL, young man!
Wanawake hasa wenye malengo ya kimaisha wanataka mtu awe real sio unamletea maigizo maana maigizo huwa yana mwisho
 
H
Mkuu mtoto wa kiume hatakiwi kukata tamaa, huyu mtoto anaweza kutnitoa kimaisha hapo badae. Mi namjua ila ndo najaribu kuendana na life style lake kwanza.
Nakuelewa...lakini usisahau ndege wafananao ndiyo huruka pamoja... usije ukaumizwa tu mbele ya safari...
 
Mtoto natokea majuu, na ni wakishua balaa, Afu natamani maisha anayo ishi ila mi sina uwezo huo. Ila nikimpata nita enjoy sana hela zake na tutashirikiana kimaisha .
Kwao ni hapahapa bongo na nimeshakutana nae mara mbili uso kwa uso ndo nikamuomba contact.

Ohooooo.......sasa wewe unatafuta shida.........tena sio ndogo......
 
Alikua mamtoni nchi gan na mji gan ?? Alikua akifanya shughuli gan huko ?? Ameishi kule mda gan ??

Na maana yangu kuku uliza hvyo. Tehe
 
Alikua mamtoni nchi gan na mji gan ?? Alikua akifanya shughuli gan huko ?? Ameishi kule mda gan ??

Na maana yangu kuku uliza hvyo. Tehe
Hee we usije ukawa kaka mtu, we sema tu kiwanja, nishachanganyikiwa hapa. maana anasubiri jibu
 
Hivi cape town fish market bado ipo? au wamefunga kwa kodi?

mpeleke ciello

au pale rio gym juu pale golden jubilee plaza ghorofa ya tano wana kiji restaurant cha kishkaji na swimingpool kiaina halafu ukimaliza mnaingia JB bellmonte pale kula mzigo
 
atakua kamtoa badoo af mchumba kamwambia yuko mamtoni kumbe yuko mtoni kwa azizi aly
Mkuu mtoto hadi siku ya kukata ndege kuondoka nilijua na siti aliyokuwa amekaa naijua. Kiufupi amekaa mamtoni miaka minne sasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom