Msaada juu ya data network ya hii Galaxy note 9.

teac kapex

JF-Expert Member
Jan 23, 2011
470
136
Kwa kweli simu nilizoamini ni nzuri ni pamoja na Samsung lakini kwangu imekuwa tofauti, mwanzoni simu ilikuwa vizuri lakini sasa hivi natamani kurudi kwenye tecno na infinix, maana nikiwa safarini nawaona wenzangu wakivinjari kwenye mitandao ya kijamii mwanzo mwisho wa safari lakini hili la kwangu limekuwa kimeo halikamati namaanisha netwok hakuna, na siwezi kupiga simu nikiwa safarini, linapoteza mara kwa mara mtandao ingawa ukiangalia pale juu unaona bar zipo zimejaa, lakini kumbe ni emergency calls tu. Hivyo naomba kujua kama kuna mahali pa kurekebisha ili lirudi kama zamani au ndo limekwisha kazi? Natanguliza shukrani
 
Hio simu ni refurb? Kutokana na mtandao na mtandao ilipotokea inawezekana ikamiss 2G/3G/4G bands ikawa mahala fulani unapata mtandao hasa mjini na mahala fulani hupati hasa nje ya jiji.

Unajua kuingia download mode? Ingia kisha angalia model husika.
 
😅😅😅.eby angalia bands zake ni cha ichi gani.
PIA IZO NOTES PHONES UKIWEKA LITE (4G)NA MAHALI ULIPO LITE HAISHIKI BASI INAKATAA KABIXA NA DATA HAIWAKI . CHA KUFANYA UKIONA UMEWESHA DATA THEN ZINAZIMA CHENYEWE NA MTANDAO KUPOTEA NENDA KASHUSHE MTANDAO WEKA WEKA 3G INASOMA FRESH LAKIN BAR INAONESHA 4G
 
yaani urudi tecno kisa mtandao

si ni bora ninunue smart kitochi niwe naunga hotsport???

yaani note 9 ni ya kuidharau hivi!!!aaaaaaah wewe hiyo simu yako itupe tu unajua ulikoitoa
 
Hio simu ni refurb? Kutokana na mtandao na mtandao ilipotokea inawezekana ikamiss 2G/3G/4G bands ikawa mahala fulani unapata mtandao hasa mjini na mahala fulani hupati hasa nje ya jiji.

Unajua kuingia download mode? Ingia kisha angalia model husika.
Ni kweli simu yenyewe ni refurb sasa nifanyeje au ndio safari yake imefika? Naifananisha na tecno L9 ilikuwa hivi na yenyewe ilikuwa ukifika majali network sio nzuri inakata mtandao hadi ufike mjini ndo net irudi. Sasa hii nazidiwa hadi na wenye aitel, kwa simu hii limebaki kama pambo tu, naichukia pale watu wanapoiona na kusifia huku nikjua ni utopolo.
 
Hiyo simu ni mbovu..na nimeamini simu nyingi bongo ni mbovu...nimeagiza samsung note 9 korea, second hand laini moja imekuja kama mpya, betri lake si mchezo linakaa balaa, je ningepata mpya?.
We yako ni mbovu
 
Hiyo unayoisema ni kwa ajili ya samsung s9, nimejaribu kwenye note9 imegoma kila niki press volume down key+bixby+Power inajaribu kuwaka inashindwa, bado nahitaji msaada yaani watu wengine wanafaidi simu zao hadi za itel mimi daaaah.
 
Siku hizi wamebadilika kidogo unapaswa kuchomeka usb tpye c hata headphone ndio itakubali download mode au recovery mode bila hivo haikubali naona kwenye note 9 na note 10 ndio zilivyo kwa sasa
 
Back
Top Bottom