Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #81
65.
“OOhh..!!, Onesmo na Sheray. ….”
Yule mlinzi akawakaribisha kwa lugha ya Kinyarwanda. Wakaongoza pamoja mpaka lango la kuingilia sebuleni na walivyofika tu getini Alice na Mama yake wakashangaa kufunguliwa na kijana mtanashati. Mwenye asili halisi ya kinyarwanda.
“Welcome to my world ”
“Murakoze databuja..!! (Asante bosi)”
Sheray na Onesmo wakaitikia kwa lugha ya kikwao yakinyarwanda. Mtoto wa rais, Aloyce ndiye aliokuwa amewafungulia lango la kuingilia sebuleni. Alikuwa ameshawaandaa wahudumu takribani ishirini. Kila mmoja akiwa ameshikilia kitu chake kuna waliokuwa wakiranda randa sebuleni huku wakizunguka na Aloyce mikononi mwao wakiwa na sahani zilizobeba pombe kali sambamba na glasi. Wengine wakiwa jikoni kwa kuandaa maakuli na baadhi wakimfuata Alice na Mama yake wakiwapepea japokuwa jumba la Aloyce lilizungukwa na viyoyozi vyenye kutoa harufu nzuri na ya kuvutia.
“Welcome miss Tanzania..!!”
Aloyce akaongea kwa tabasamu huku akimtolea macho Alice. Alice kwa uoga akajikuta anashika mapigo yake ya moyo huku akihoji kwa kutokujiamini.
“unaongea na mimi..??”
“Yes, its you mrembo angu. Mrembo nambari moja Tanzania. Na nionavyo you deserve to be the first one and ever in Africa and the whole world. Aboslute honesty wewe ni miss world wangu.. naitwa nani..?”
“Alice Majaliwa.”
Alice akajikuta anatoa tabasamu pana huku macho yake akiyalekeza kwa mama yake wa kufikia,Janet. Zile ndoto za kuishi maisha mazuri zikamteka Alice kwa haraka sana. Akajihisi kusisimka mwili wake mara kwa mara akiyatolea macho mazingira ya sebule. Moja kwa moja akajikuta moyo wake ukiafiki kuwa na Aloyce maishani mwake.
“How about Journey, Sheray..?? Mekuwaje huko..? firstly …..”
Aloyce akawageukia Onesmo na Sheray akawahoji juu ya safari yao.”
“ikuwa mzuri sana. Tumesafiri hakuna shida njjani. Shortly it was good…”
Sheray akamjibu Aloyce kwa ufupii na kiufasaha huku nayeye akichanganya kumjibu kwa lugha ya kiingereza.
“na huyu ni nani..? from Tanzania too..?”
“ni mama wa Alice. Inaitwa Janet. Ni muzuri tu na haina mineno. Tumeichukuwa iwe karibu na itoto yake Alice. Ifarijike..”
Aloyce akafurahi sana. Siku hiyo ikawa kama sherehe kubwa sana kwake. Akatamani sana baba yake angekuwepo lakini ikashindikana kutokana na safari za kikazi za baba yake Aloyce. Wakasherekea peke yao na wahudumu wake. Furaha ikatawala jumba lote. Onesmo na Sheray wakajiona wao ndio wanafuraha mara mbili jumba zima kuliko hata bosi wao Aloyce. Kwanza wakajiona wanafuraha ya kufanikisha zoezi zima la kumpata mrembo nambari moja kwa uzuri Tanzania na pili kitita cha mapesa walichohaidiwa na Aloyce. Wakasherekea kwa muda wa masaa matatu mfululizo huku kila mmoja akibadilishana mawazo kwa kuongea stori mbili tatu na mwenzake. Siri kubwa ya watu wanne juu ya yaliotokea huko Tanzania ikabaki moyoni mwao. Siri ya Alice kuua na pili siri ya Alice kupokwa ushindi na kuhairishwa kwa mashindano. Baada ya kushereke kwa masaa kadhaa, Aloyce akaelekea chumbani kwake na punde akarejea na sanduku dogo mkononi mwake. Akawaita Onesmo na Sheray wakaelekea mpaka nje wakajificha katika kona.
“Hii ni kwa ajili yenu.. nice job ……”
Akawakabidhi lile sanduku. Sanduku ambalo lilijazwa kwa pesa nyingi sana. Ikiwa ni kama sehemu ya makubaliano baada ya Aloyce kufikishiwa kitu ambacho alikitamani maishani mwake. Ndoto ya siku nyingi sana kwake. Akwakabidhi wakatokomea zao kisha Aloyce akarejea peke yake sebuleni. Kabla hajakaa chini akawa kama amekumbuka kitu akatoka tena nje kabisa kuwaita Onesmo na Sheray.
“Mesema hakuna tatizo huko mtokako..? hakuna sumbufu yeyote..??”
“Yes boss..!!”
“OOhh..!!, Onesmo na Sheray. ….”
Yule mlinzi akawakaribisha kwa lugha ya Kinyarwanda. Wakaongoza pamoja mpaka lango la kuingilia sebuleni na walivyofika tu getini Alice na Mama yake wakashangaa kufunguliwa na kijana mtanashati. Mwenye asili halisi ya kinyarwanda.
“Welcome to my world ”
“Murakoze databuja..!! (Asante bosi)”
Sheray na Onesmo wakaitikia kwa lugha ya kikwao yakinyarwanda. Mtoto wa rais, Aloyce ndiye aliokuwa amewafungulia lango la kuingilia sebuleni. Alikuwa ameshawaandaa wahudumu takribani ishirini. Kila mmoja akiwa ameshikilia kitu chake kuna waliokuwa wakiranda randa sebuleni huku wakizunguka na Aloyce mikononi mwao wakiwa na sahani zilizobeba pombe kali sambamba na glasi. Wengine wakiwa jikoni kwa kuandaa maakuli na baadhi wakimfuata Alice na Mama yake wakiwapepea japokuwa jumba la Aloyce lilizungukwa na viyoyozi vyenye kutoa harufu nzuri na ya kuvutia.
“Welcome miss Tanzania..!!”
Aloyce akaongea kwa tabasamu huku akimtolea macho Alice. Alice kwa uoga akajikuta anashika mapigo yake ya moyo huku akihoji kwa kutokujiamini.
“unaongea na mimi..??”
“Yes, its you mrembo angu. Mrembo nambari moja Tanzania. Na nionavyo you deserve to be the first one and ever in Africa and the whole world. Aboslute honesty wewe ni miss world wangu.. naitwa nani..?”
“Alice Majaliwa.”
Alice akajikuta anatoa tabasamu pana huku macho yake akiyalekeza kwa mama yake wa kufikia,Janet. Zile ndoto za kuishi maisha mazuri zikamteka Alice kwa haraka sana. Akajihisi kusisimka mwili wake mara kwa mara akiyatolea macho mazingira ya sebule. Moja kwa moja akajikuta moyo wake ukiafiki kuwa na Aloyce maishani mwake.
“How about Journey, Sheray..?? Mekuwaje huko..? firstly …..”
Aloyce akawageukia Onesmo na Sheray akawahoji juu ya safari yao.”
“ikuwa mzuri sana. Tumesafiri hakuna shida njjani. Shortly it was good…”
Sheray akamjibu Aloyce kwa ufupii na kiufasaha huku nayeye akichanganya kumjibu kwa lugha ya kiingereza.
“na huyu ni nani..? from Tanzania too..?”
“ni mama wa Alice. Inaitwa Janet. Ni muzuri tu na haina mineno. Tumeichukuwa iwe karibu na itoto yake Alice. Ifarijike..”
Aloyce akafurahi sana. Siku hiyo ikawa kama sherehe kubwa sana kwake. Akatamani sana baba yake angekuwepo lakini ikashindikana kutokana na safari za kikazi za baba yake Aloyce. Wakasherekea peke yao na wahudumu wake. Furaha ikatawala jumba lote. Onesmo na Sheray wakajiona wao ndio wanafuraha mara mbili jumba zima kuliko hata bosi wao Aloyce. Kwanza wakajiona wanafuraha ya kufanikisha zoezi zima la kumpata mrembo nambari moja kwa uzuri Tanzania na pili kitita cha mapesa walichohaidiwa na Aloyce. Wakasherekea kwa muda wa masaa matatu mfululizo huku kila mmoja akibadilishana mawazo kwa kuongea stori mbili tatu na mwenzake. Siri kubwa ya watu wanne juu ya yaliotokea huko Tanzania ikabaki moyoni mwao. Siri ya Alice kuua na pili siri ya Alice kupokwa ushindi na kuhairishwa kwa mashindano. Baada ya kushereke kwa masaa kadhaa, Aloyce akaelekea chumbani kwake na punde akarejea na sanduku dogo mkononi mwake. Akawaita Onesmo na Sheray wakaelekea mpaka nje wakajificha katika kona.
“Hii ni kwa ajili yenu.. nice job ……”
Akawakabidhi lile sanduku. Sanduku ambalo lilijazwa kwa pesa nyingi sana. Ikiwa ni kama sehemu ya makubaliano baada ya Aloyce kufikishiwa kitu ambacho alikitamani maishani mwake. Ndoto ya siku nyingi sana kwake. Akwakabidhi wakatokomea zao kisha Aloyce akarejea peke yake sebuleni. Kabla hajakaa chini akawa kama amekumbuka kitu akatoka tena nje kabisa kuwaita Onesmo na Sheray.
“Mesema hakuna tatizo huko mtokako..? hakuna sumbufu yeyote..??”
“Yes boss..!!”