39.
Katika ukumbi maarufu wa Gold first ambao upo Kinyapa road, Nyamagana ulikuwa umesheheni warembo mbali mbali ambao walikuwa wakishiriki mashindano ya kumtafuta mlimbwende ambaye ataiwakilisha vyema jiji hili la Mwanza katika kinyang’anyiro kingine cha kumtafuta mrembo wa Tanzania mwaka huu. Takribani ya washiriki ishirini walikuwa wamepanga mstari huku majaji zaidi ya watano wakiwa sambamba na mgeni rasmi ambaye ni mbunge wa Nyamagana jiji la mwanza (Mheshimiwa Ezekiel Wenje). Kati ya majaji hao waliokuwa wameketi mbele huku wamevalia suti nyeusi, alikuwepo John Mapunda. Taarifa juu ya jana yake Alice kushinda taji ndio ilimfurahisha haswa na kumfanya kila muda awe na furaha. Sasa kichwa chake kikawa pamoja na kufikiri ushindani ambao atakutana nao Alice katika mashindano makubwa yafuatayo. Ni Jamila Said peke yake aliokuwepo katika halmashauri ya kichwa cha John mara zote. Jamila alikuwa mzuri sana na alikuwa na kila sifa ya kuwa mshindi katika jiji hili la Mwanza, lakini kwa hilo halikumsababishia yeye kushinda taji hilo la Mwanza mbele ya washiriki wenzake zaidi ya kumi na tisa, Mpaka pale alipolala na John katika hotel ya Savoy siku mbili kabla ya mashindano haya. Muda wote Alipokuwa Jamila akipita, John alikuwa akimpa maksi japo kwa kutetemeka. John alijitahidi kutoa pesa kwa majaji wenzake ili tu Jamila aweze kupita na kumtimizia malengo ya siku nyingi ambayo yalikuwa yakimpa tabu licha ya kusuluhishwa yakaisha.
“..Hapa kinachoangaliwa ni mtoto tu..!, Ndipo nitaridhika na maisha, Ndio mtoto..!!”
John alijikuta akiongea mwenyewe kimoyo moyo huku akichukuwa karatasi yake na kumpitisha Jamila. Baada ya warembo wote kumaliza kupita pale mbele, John aliwaweka majaji wenzake chini kisha wakalipitisha jina la mshindi na kumkabidhi mgeni rasmi. Kamwe John hakulifikiria swala la Alice, alijua fika atamwaga tu Jamila kwa kumpa ushindi wa pili wa mashindano makubwa na pia malengo yake yatakuwa yameshatimia ya kumpa mimba. Punde mgeni rasmi mheshimiwa Ezekiel Wenje akapanda na kisha kumtangaza mshindi wa shindano la kumtafuta mrembo wa jiji la mwanza. Alimtaja yule yule aliyopitishwa na John pamoja na majaji wenzake,Jamila Said. Wapo baadhi waliguna lakini wengi wao waliafiki juu ya ushindi huo. Moyo wa John sasa ukawa umesharidhika huku ukitambua fika sasa malengo yake yatatimia juu ya kumpata mtoto kupitia mrembo huyo Jamila Said. John alitamani kesho yake ifike ili alale naye tena kwa mara ya mwisho na kisha arudi Dar es salaam kupanga mikakati mingine.
Baada ya siku moja kumpata mrembo atakayeliwakilisha jiji la Mwanza Jamila Said. Sasa ikawa ni zamu ya John kwa ahadi walizokuwa wamepeana. John alifurahi kuwa na Jamila kwa mara ya pili. Na kwa usiku ule alifanikiwa kupata Hotel ya Savoy ambayo ilijificha sana, kisha wakaagiza chumba na kulala na Jamila.
“..Baby umenifurahisha sana jana..!!”
“..Ok.., kwangu mie wala usiwe na shaka Jamila, Na kama utashika mimba tu kabla hatujaingia kwenye fainali ya kumtafuta mrembo wa Tanzania nakuhaidi moja kwa moja wewe utakuwa wa kwanza na nitahakikisha siri ya wewe kuwa na mimba yangu yote inafichwa mpaka unajifungua nakuendelea kuhudumia kwa kila kitu..”
“..Kwani umeoa John..??”
“..Kuoa..??, Hapana.., Ila nilishawahi kuishi na mwanamke lakini kama bahati Mungu akanionesha, Hakuwa na uwezo wa kushika mimba hivyo nikamrudisha kwao na kwa sasa naishi na mtoto wa Dada yangu tu, tena ni kabinti kadogo sana na nakasomesha kapo kidato cha pili..”
John alizidisha kumdanganya Jamila. Jamila hakujua lolote hivyo ilimbidi kukubaliana na yote kutokana na wazazi wake kumwachia laana kwa kukataa kuendelea na masomo huku akitanga tanga na wanaume sambamba na kujihusisha na kuigiza filamu za kibongo japo hazikumpa umaarufu sana katika jiji la mwanza. John aliyafurahia mapenzi usiku mzima huku akiamini malengo yake lazima yatimie ya kuitwa Baba, haijalishi mtoto atampata wa kiume ama wa kike.