Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #101
84.
Nguvu ya mwili ikaendelea kumuisha Alice. Akajihisi mwili wote kumtetemeka haswa sehemu ya magotini kukosa ushirikiano. Macho yake yote yakawa bado yanawaangalia wale mapolisi kwa upande wa chini yake. Wale mapolisi wakawa hawamwangalii tena zaidi ya kuwashuhudia wakiendelea kumuhoji yule mhudumu wa mapokezi.
“Mungu baba weza kunisaidia kutoka katika hii sehemu”
.
Alice akajikuta akiomba sala taratibu. Mwili wake ukawa bado hauna uwezo wa kutembea. Akainama chini kabisa kwa kukosa nguvu nakuanza kujiburuza huku akitafuta chumba kile alichofikia. Aliendelea kujikokota kwa utaratibu mithili ya mnyama aliyekosa ama kuumizwa miguu. Hakukuwa na msaada wowote kutokana na kila mmoja aliyepangisha hapo hotelini kujifungia ili kupisha uchunguzi uliokuwa ukifanywa hapo chini na mapolisi. Hatua chache alizotumia kujiburuta Alice zikamfanya akaribie maeneo ya mlango wa hoteli lakini hakikuwa chumba alichokuwa amepanga Aloyce hapo awali.
“What are you doing here ?” (Unafanya nini hapa?)
“Please help me?” (Nisaidie tafadhari?)
Alikuwa ni mmoja wa wapangaji pale hotelini. Alikuwa amefungua mlango kwa uwoga baada ya kuhisi kama kuna mtu anaugusa mlango wa chumbani mwake.
“Means you did’nt hear the command of the police?” (Inamaana amri ya polisi hujaisikia?)
Yule dada akaendelea kumhoji Alice na safari hii akaongeza sauti zaidi na kuongea kwa sauti ya juu kidogo hali iliomfanya Alice kuendelea kutetemeka kwa uwoga.
“I heard “ (Nilisikia)
Alice akajitahidi kujitetea kwa yule dada huku akifungua pochi yake nakutoa ufunguo wa chumba chake hali iliomfanya yule dada aamini kama Alice naye ni mpangaj kama yeye katika hotel ya Darlington. Kwa huruma ambayo ilikuwa imemuingia yule dada kwa muda mfupi akajikuta akichukuwa mikono yake nakuigusanisha na ya Alice kisha akamvuta nakumuingiza ndani ya chumba chake moja kwa moja nakumkalisha katika kochi la chumbani kwake.
“Tell me where are you from?” (haya niambie watokea wapi wewe?)
“M’ from Uganda” (Natokea Uganda)
Alice akadanganya kwa makusudi ili tu asiweze kujulikana.
“I’m from Kenya and we are neighbors because we all live in one East Africa zone. So you know Swahili?” ( Mimi natokea Kenya na ni jirani yako kwa sababu wote tunaishi ukanda mmoja wa afrika mashariki. Kwahiyo unajua Kiswahili?”
“Ndio najua!!”
Alice akamjibu kwa kutumia lugha ya Kiswahili nakumfanya yule dada aamini kama Alice anatokea afrika mashariki tena nchi ya Uganda.
“Nafurahi kukusikia hivyo. Naitwa Achieng, Sijui mwenzangu waitwaga nani vile?”
“Naitwa Jacky”
Alice ikambidi kuongopa jina lake. Hakutaka kabisa Achieng ajue anaitwa nani na hata anapoishi. Alice akajikuta yale maumivu aliokuwa nayo muda mfupi uliopita katika miguu yake kama yakimuisha taratibu. Furaha ya moyo ikaanza kumtawala hata lile tumbo ambalo lilikuwa kama linamkata likaanza kutulia kwa maumivu.
“Mie nalikuja hapa kwa harusi ya my brother aitwa Alongise Mangaliwa na ilikuwa yafanyika Darlington 1, sijui kwa wewe mwenzangu au tulikuwa kwa wote Darlington 1?”
Nguvu ya mwili ikaendelea kumuisha Alice. Akajihisi mwili wote kumtetemeka haswa sehemu ya magotini kukosa ushirikiano. Macho yake yote yakawa bado yanawaangalia wale mapolisi kwa upande wa chini yake. Wale mapolisi wakawa hawamwangalii tena zaidi ya kuwashuhudia wakiendelea kumuhoji yule mhudumu wa mapokezi.
“Mungu baba weza kunisaidia kutoka katika hii sehemu”
.
Alice akajikuta akiomba sala taratibu. Mwili wake ukawa bado hauna uwezo wa kutembea. Akainama chini kabisa kwa kukosa nguvu nakuanza kujiburuza huku akitafuta chumba kile alichofikia. Aliendelea kujikokota kwa utaratibu mithili ya mnyama aliyekosa ama kuumizwa miguu. Hakukuwa na msaada wowote kutokana na kila mmoja aliyepangisha hapo hotelini kujifungia ili kupisha uchunguzi uliokuwa ukifanywa hapo chini na mapolisi. Hatua chache alizotumia kujiburuta Alice zikamfanya akaribie maeneo ya mlango wa hoteli lakini hakikuwa chumba alichokuwa amepanga Aloyce hapo awali.
“What are you doing here ?” (Unafanya nini hapa?)
“Please help me?” (Nisaidie tafadhari?)
Alikuwa ni mmoja wa wapangaji pale hotelini. Alikuwa amefungua mlango kwa uwoga baada ya kuhisi kama kuna mtu anaugusa mlango wa chumbani mwake.
“Means you did’nt hear the command of the police?” (Inamaana amri ya polisi hujaisikia?)
Yule dada akaendelea kumhoji Alice na safari hii akaongeza sauti zaidi na kuongea kwa sauti ya juu kidogo hali iliomfanya Alice kuendelea kutetemeka kwa uwoga.
“I heard “ (Nilisikia)
Alice akajitahidi kujitetea kwa yule dada huku akifungua pochi yake nakutoa ufunguo wa chumba chake hali iliomfanya yule dada aamini kama Alice naye ni mpangaj kama yeye katika hotel ya Darlington. Kwa huruma ambayo ilikuwa imemuingia yule dada kwa muda mfupi akajikuta akichukuwa mikono yake nakuigusanisha na ya Alice kisha akamvuta nakumuingiza ndani ya chumba chake moja kwa moja nakumkalisha katika kochi la chumbani kwake.
“Tell me where are you from?” (haya niambie watokea wapi wewe?)
“M’ from Uganda” (Natokea Uganda)
Alice akadanganya kwa makusudi ili tu asiweze kujulikana.
“I’m from Kenya and we are neighbors because we all live in one East Africa zone. So you know Swahili?” ( Mimi natokea Kenya na ni jirani yako kwa sababu wote tunaishi ukanda mmoja wa afrika mashariki. Kwahiyo unajua Kiswahili?”
“Ndio najua!!”
Alice akamjibu kwa kutumia lugha ya Kiswahili nakumfanya yule dada aamini kama Alice anatokea afrika mashariki tena nchi ya Uganda.
“Nafurahi kukusikia hivyo. Naitwa Achieng, Sijui mwenzangu waitwaga nani vile?”
“Naitwa Jacky”
Alice ikambidi kuongopa jina lake. Hakutaka kabisa Achieng ajue anaitwa nani na hata anapoishi. Alice akajikuta yale maumivu aliokuwa nayo muda mfupi uliopita katika miguu yake kama yakimuisha taratibu. Furaha ya moyo ikaanza kumtawala hata lile tumbo ambalo lilikuwa kama linamkata likaanza kutulia kwa maumivu.
“Mie nalikuja hapa kwa harusi ya my brother aitwa Alongise Mangaliwa na ilikuwa yafanyika Darlington 1, sijui kwa wewe mwenzangu au tulikuwa kwa wote Darlington 1?”