Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,843
- Thread starter
- #21
20.
“..Hapana dokta na kiumbe changu..”
“..Ni kwamba mimba inaonesha ilikuwa ndogo sana hivyo imesharibika na hii harufu kali unayoendelea kuisikia ambayo hii damu iliobadilika rangi na kuwa ya kijani na manjano imetokana na hii mimba iliyoharibika, Na huenda mimba ikawa imechangia kifo cha huyu japo sijapima vipimo vingine vilivyompelekea kifo chake. Cha muhimu ni kumshukuru Mungu kwa kazi yake aliyoitenda..”
“..Noo, Noo, Nooo Dokta siwezi kuvumilia..!!, Dokta nashindwa kujizuia..!!, ni nani ataliziba pengo hili.., nani atanizalia Doktaaaa….”
Daktari akabaki na mshangao, Mshango wa kile anachoendelea kukishuhudia kwa John, Alijitahidi sana kumbembeleza lakini ndio kwanza alikuwa akizizidisha hasira za John ambazo sasa zilikuwa zinamshinda nguvu na kusababisha mdomo wake kuanza kuropoka ovyo na kwa sauti ya ukali. John na yule daktari Wakiwa bado wodi ya wagonjwa mahututi mara Nesi akatokea huku akionesha anahema sana na amekuja kwa taarifa.
“..Dokta..??, Dokta…??, Dokta..?? Yyyuuu uule mgonjwa uliyetuambiaa tut u tuumpeleke kule wooddini.., tumemuwekea ile oksijeni ili apate hewa lakini oksijeni yote imejaa damu na sasa yupo anafurukuta kama anataka ku..”
“..Unasemaje..??, Alice anakufaa..?”
John alishikwa na butwaa nakuropoka.., hakuamini maneno ya yiule Nesi, wakaondoka wote na Yule Dokta mpaka kwenye wodi alipokuwa amelazwa Alice napo walipofika walishuhudia kitanda chote kikifurika bahari ya damu huku Alice akijikunja kunja mithili ya mtu anayetaka kukata roho..
******************************
ITAENDELEA
“..Hapana dokta na kiumbe changu..”
“..Ni kwamba mimba inaonesha ilikuwa ndogo sana hivyo imesharibika na hii harufu kali unayoendelea kuisikia ambayo hii damu iliobadilika rangi na kuwa ya kijani na manjano imetokana na hii mimba iliyoharibika, Na huenda mimba ikawa imechangia kifo cha huyu japo sijapima vipimo vingine vilivyompelekea kifo chake. Cha muhimu ni kumshukuru Mungu kwa kazi yake aliyoitenda..”
“..Noo, Noo, Nooo Dokta siwezi kuvumilia..!!, Dokta nashindwa kujizuia..!!, ni nani ataliziba pengo hili.., nani atanizalia Doktaaaa….”
Daktari akabaki na mshangao, Mshango wa kile anachoendelea kukishuhudia kwa John, Alijitahidi sana kumbembeleza lakini ndio kwanza alikuwa akizizidisha hasira za John ambazo sasa zilikuwa zinamshinda nguvu na kusababisha mdomo wake kuanza kuropoka ovyo na kwa sauti ya ukali. John na yule daktari Wakiwa bado wodi ya wagonjwa mahututi mara Nesi akatokea huku akionesha anahema sana na amekuja kwa taarifa.
“..Dokta..??, Dokta…??, Dokta..?? Yyyuuu uule mgonjwa uliyetuambiaa tut u tuumpeleke kule wooddini.., tumemuwekea ile oksijeni ili apate hewa lakini oksijeni yote imejaa damu na sasa yupo anafurukuta kama anataka ku..”
“..Unasemaje..??, Alice anakufaa..?”
John alishikwa na butwaa nakuropoka.., hakuamini maneno ya yiule Nesi, wakaondoka wote na Yule Dokta mpaka kwenye wodi alipokuwa amelazwa Alice napo walipofika walishuhudia kitanda chote kikifurika bahari ya damu huku Alice akijikunja kunja mithili ya mtu anayetaka kukata roho..
******************************
ITAENDELEA
