Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,843
- Thread starter
- #61
49.
“..Hapana..!!, nyumbani kwao walikuwa na uwezo hivyo akawa anapewa hela nyumbani kwao na zinanisaidia kujkimu. Siku baada ya siku Nick wangu akaanza kubadilika nakujikuta anajiingiza katika madawa ya kulevya. Nilijitahidi kumrudisha Nick katika hali yake ya zamani lakini sikuwa na ujanja kwa kuwa hela alikuwa akipewa kwao na kukimbilia kwenye madawa. Ile hali ya Nick nikajikuta sina hela hata kidogo. Sina mtegemezi tena hivyo nikaanza na mimi kutafuta pesa huku nikiendelea mahusiano ya kimapenzi na Nick wangu japo si sana. Nilitanga huku na kule huku mpaka baadhi ya rafiki zangu waliponishauri nijiingize katika kuigiza filamu za kibongo. Napo nikaambulia kutambulika tu pale Mwanza lakini nikawa natembea na wanaume tofauti kisiri siri wanaoigiza na hata wengine watengenezaji na wasambazaiji wa hizi Cd za bongo muvi huku nikijilinda kwa kutumia kinga nakumtelekeza Nick wangu.
“Mmmh..!!, pole mwaya kwa matatizo.., sasa ikawaje Jamila rafiki..?”
“..Basi mpaka akatokea ndugu yangu mmoja akanishauri kwakuwa nina mwili mzuri tu naweza kujiingiza katika urembo na nikashinda. Nikaanza kutafuta fomu nakuingia rasmi katika mashindano haya ya urembo. Taarifa zikamfikia mpaka Nick wangu. Nikarudiana naye japokuwa alikuwa ameshaathirika na madawa sana ila niliapa nitakuja kufunga naye ndoa siku moja kwakuwa ndio mwanaume wangu wa maisha aliyenitoa usichana wangu. Nilipokuwa bado kambini kule Mwanza kabla hatujaingia katika mashindano alinifuata Jaji mmoja kisha akaniambia kuwa endaapo nitatembea nae yuko tayari kuniweka kuwa mshindi wa kwanza na hivyo kuja huku Dar. Na pia kama nitakuwa mshindi atanipa tena na mtihani mwingine wa kumzalia mtoto. Hapa ninapokwambia zoezi la kwanza nimefanikiwa kwani nililala naye nakumpa mapenzi nayeye akanitekelezea kama nilichokitaka hivyo nikawa mshindi wa kwanza.. Tatizo kubwa nilionalo Alice.., si unakumbuka jana usiku tulipishana bafuni..??”
“..Ndio nakumbuka Jamila..!!”
“..Basi nilienda kutapika na hapa najisikia kichefu chefu sana na hii yote ni dalili ya mimba Alice..”
“..Kwahiyo inamaana tayari umeshika mimba Jamila..??”
“..Ndio tena nahisi hivyo lakini kama ni mimba basi itakuwa ni ya mpenzi wangu Nick siyo yule Jaji..!!”
Alice alikuwa akiifuatilia story hiyo kwa masikitiko makubwa huku akionesha kutikisa kichwa kwa kumsikitikia Jamila kwa yaliomkuta na kumpa pongezi kwa hapa alipofika.
“..Kwa huyo huyo mtu aliokupitisha ukawa mshindi alikuwa akiishi huko huko Mwanza au..?”
“..Hapana Alice, huyu mtu anaitwa John aliniambia anaishi na kufanya kazi huku huku Dar..”
“..nani Jamila..??”
Alice alioneshwa kushtushwa sana na jina la John. Akili yake moja kwa moja ilimpeleka mpaka kwa Baba yake wa kufikia, John. Hakutaka kuamini kabisa kama Baba yake angeweza kuwa na tabia hizo. Mapigo yake ya moyo sasa yakawa yanaanza safari kama vile gari lililokuwa likishuka kwenye mteremko mkali. Alijihisi jasho jembamba kumtoka, huku ile hali ya usingizi ikimuishia kabisa. Muda wote alikuwa akimkodolea jicho Jamila.
“Mhh..!!, Alice mbona umebadilika ghafla my Dear..?”
“Hapana Jamila, embu niambie kweli wala hata usinifiche. Umesema huyo mtu anatwa nani tena..??”
“..Hapana..!!, nyumbani kwao walikuwa na uwezo hivyo akawa anapewa hela nyumbani kwao na zinanisaidia kujkimu. Siku baada ya siku Nick wangu akaanza kubadilika nakujikuta anajiingiza katika madawa ya kulevya. Nilijitahidi kumrudisha Nick katika hali yake ya zamani lakini sikuwa na ujanja kwa kuwa hela alikuwa akipewa kwao na kukimbilia kwenye madawa. Ile hali ya Nick nikajikuta sina hela hata kidogo. Sina mtegemezi tena hivyo nikaanza na mimi kutafuta pesa huku nikiendelea mahusiano ya kimapenzi na Nick wangu japo si sana. Nilitanga huku na kule huku mpaka baadhi ya rafiki zangu waliponishauri nijiingize katika kuigiza filamu za kibongo. Napo nikaambulia kutambulika tu pale Mwanza lakini nikawa natembea na wanaume tofauti kisiri siri wanaoigiza na hata wengine watengenezaji na wasambazaiji wa hizi Cd za bongo muvi huku nikijilinda kwa kutumia kinga nakumtelekeza Nick wangu.
“Mmmh..!!, pole mwaya kwa matatizo.., sasa ikawaje Jamila rafiki..?”
“..Basi mpaka akatokea ndugu yangu mmoja akanishauri kwakuwa nina mwili mzuri tu naweza kujiingiza katika urembo na nikashinda. Nikaanza kutafuta fomu nakuingia rasmi katika mashindano haya ya urembo. Taarifa zikamfikia mpaka Nick wangu. Nikarudiana naye japokuwa alikuwa ameshaathirika na madawa sana ila niliapa nitakuja kufunga naye ndoa siku moja kwakuwa ndio mwanaume wangu wa maisha aliyenitoa usichana wangu. Nilipokuwa bado kambini kule Mwanza kabla hatujaingia katika mashindano alinifuata Jaji mmoja kisha akaniambia kuwa endaapo nitatembea nae yuko tayari kuniweka kuwa mshindi wa kwanza na hivyo kuja huku Dar. Na pia kama nitakuwa mshindi atanipa tena na mtihani mwingine wa kumzalia mtoto. Hapa ninapokwambia zoezi la kwanza nimefanikiwa kwani nililala naye nakumpa mapenzi nayeye akanitekelezea kama nilichokitaka hivyo nikawa mshindi wa kwanza.. Tatizo kubwa nilionalo Alice.., si unakumbuka jana usiku tulipishana bafuni..??”
“..Ndio nakumbuka Jamila..!!”
“..Basi nilienda kutapika na hapa najisikia kichefu chefu sana na hii yote ni dalili ya mimba Alice..”
“..Kwahiyo inamaana tayari umeshika mimba Jamila..??”
“..Ndio tena nahisi hivyo lakini kama ni mimba basi itakuwa ni ya mpenzi wangu Nick siyo yule Jaji..!!”
Alice alikuwa akiifuatilia story hiyo kwa masikitiko makubwa huku akionesha kutikisa kichwa kwa kumsikitikia Jamila kwa yaliomkuta na kumpa pongezi kwa hapa alipofika.
“..Kwa huyo huyo mtu aliokupitisha ukawa mshindi alikuwa akiishi huko huko Mwanza au..?”
“..Hapana Alice, huyu mtu anaitwa John aliniambia anaishi na kufanya kazi huku huku Dar..”
“..nani Jamila..??”
Alice alioneshwa kushtushwa sana na jina la John. Akili yake moja kwa moja ilimpeleka mpaka kwa Baba yake wa kufikia, John. Hakutaka kuamini kabisa kama Baba yake angeweza kuwa na tabia hizo. Mapigo yake ya moyo sasa yakawa yanaanza safari kama vile gari lililokuwa likishuka kwenye mteremko mkali. Alijihisi jasho jembamba kumtoka, huku ile hali ya usingizi ikimuishia kabisa. Muda wote alikuwa akimkodolea jicho Jamila.
“Mhh..!!, Alice mbona umebadilika ghafla my Dear..?”
“Hapana Jamila, embu niambie kweli wala hata usinifiche. Umesema huyo mtu anatwa nani tena..??”