Mradi wa ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba umeleta ajira na kuchangia chachu ya ukuaji wa uchumi

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,902
945
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama, amesema mradi wa Ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba, pamoja na Miradi mingine ya kimkakati imeleta ajira na kuchangia kasi na chachu ya ukuaji wa uchumi hususan katika Jiji la Dodoma.

Ameyasema hayo mapema leo 3 August 2023, alipokuwa katika ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa Jengo la Mpigachapa Mkuu wa Serikali; Jengo la Kituo cha Taifa cha Usimamizi na Uratibu wa Maafa, Jengo la Wizara Mipango na Uwekezaji, na jengo la Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu).

Waziri Mhagama alisema kuwa, ujenzi wa Mradi hiyo mikubwa ya kimkakati inayoendelea umewezesha vijana wengi kupata ajira katika maeneo hayo, na kujiongezea pato binafsi sambamba na kuchangia ukuajia wa uchumi kutokana na manunuzi ya bidhaa zinazotumika katika mradi hiyo kufanyika katika viwanda vilivyopo nchini.

Alipokuwa katika jengo la Mpigachapa Mkuu wa Serikali, Waziri Mhagama alisema kuwa mradi huo, mkubwa umefikia asilimia tisini na saba (97%) ambapo kiwanda hicho kitakapokamilika kitakuwa na hadhi na sifa ya kuwa ni kiwanda kikubwa kimojawapo cha Serikali,ambapo mashine mpya zimeagizwa na kiwanda hicho kitafanya kazi za ndani ya nje na nchi za Afrika Mashariki (EAC) pamoja na ukanda wa nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

"Sisi tumejipanga kwa matumizi ya ndani na nje pia, nimefarijika kuona ujenzi kwa awamu, hii ya kwanza umefikia hatua kubwa, na ujenzi wa Ofisi umeanza na unaenda kwa kasi." Alisisitiza Waziri Mhagama.

Alipokuwa katika kituo cha Taifa cha Uratibu na Usimamizi wa Maafa Mhe. Mhagama alisema, ujenzi wa awamu ya kwanza ya kituo hicho pia umekamilika kwa Asilimia tisini na nne (94%) na kufafanua kuwa maghala mawili makubwa na Ofisi za Watumishi zimeshakamilika.

"Tunalo jukumu la kuhakikisha kwamba katika kituo hicho nchi inafikia malengo ya kitaifa na Maono na maelekezo ya Mhe. Rais, Dkt, Samia Suluhu Hassan na Serikali kwa Ujumla" Alibainisha Waziri Mhagama.

F2nxxBDXoAAuNqG.jpg
F2nxwZrXoBUJYlI.jpg
F2nzTQCXoAApyaQ.jpg
F2nzSmnXoBgZ4-W.jpg
 
Back
Top Bottom