Mradi wa Gesi Mtwara-Dar ni "White Elephant"?

Mradi wa Gesi Mtwara-Dar ni "White Elephant"?

Manelezu

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2015
Posts
1,906
Reaction score
2,776
Juhudi za kuondoa tatizo la umeme zinaonekana kuwa ngumu kila kukicha, mvua nyingi zinazoendelea kunyesha nchi nzima zimeshindwa kupunguza mgao wa umeme, Mradi wa gesi Mtwara hadi Dar es Salaam ulitoa matumaini ya kumaliza tatizo la umeme nchi surprisingly tatizo linaendelea, mradi uliogharimu taifa ma billioni ya dola, huwa najiuliza hizi pesa za huu mradi zingetumika kujenga na kuzalisha umeme huko huko mtwara then ukaingia kwenye grid ya taifa manufaa yangekuwa makubwa kiasi gani?

Naomba kuwasilisha.
 
Labda mzee mwanakijiji aje atuambie hii serekali anayoisifia na mabadiliko toka ccm ni ipi.
 
Mzee Mwanakijiji atakujia na audio zake kukuambia kuwa tatizo la mgao wa umeme litakuwa historia. Mwisho itajakuwa dhambi
 
Mkuu, naona umeandika tu bila ushahidi. Unaishi Mkoa gani Tanzania ambako kuna mgawo wa umeme?
 
Mzee Mwanakijiji atakujia na audio zake kukuambia kuwa tatizo la mgao wa umeme litakuwa historia. Mwisho itajakuwa dhambi
Tanzania hatuna mgawo wa umeme. Ni wapi kuna huo mgawo? Sisi huku Songea hatuna kabisa ijapokuwa bado tunatumia umeme wa majenereta
 
umeme utanunuliwa kutoka Ethiopia,
mkataba wa gesi ya mtwara ni wa kifamilia zaidi ndiyomaana hata uliletwa bungeni kwa hati ya dharura.
 
Arusha hakuna umeme.Tunasubiria umeme wa Ethiopia haaa haaaa haaaa haaaa.JK Tanzania itauza umeme nchi jirani.Prof Muhongo Tanzania itanunua umeme kutoka Ethiopia duh kweli nimeamini CCM ni ile ile sarakasi haziishi.


Mkuu, naona umeandika tu bila ushahidi. Unaishi Mkoa gani Tanzania ambako kuna mgawo wa umeme?
 
Arusha hakuna umeme.Tunasubiria umeme wa Ethiopia haaa haaaa haaaa haaaa.JK Tanzania itauza umeme nchi jirani.Prof Muhongo Tanzania itanunua umeme kutoka Ethiopia duh kweli nimeamini CCM ni ile ile sarakasi haziishi.

Nchi hii vituko haviishi sasa umeme utoke Ethiopia mpaka uje ufike ni lini?
 
Mkuu, naona umeandika tu bila ushahidi. Unaishi Mkoa gani Tanzania ambako kuna mgawo wa umeme?

Huku Mara,, ni kama tumezoea sasa.. maana umeme kukatika imekuwa kawaida tu.

Kibaya zaidi..wanakata jioni kuanzia sa 12 ahadi usiku wa manane
 
kama hujui kitu ukiza kwanza siyo kukurupuka na mada za upotoshaji
Inaonekana hata hujui kama mradi huo unafanyakazi, we gesi ya kinyerezi unajua inatoka wapi?
 
Siku hizi maswali ya kijinga huwa nayachukia sana. Wenyewe walishaimba "CCM ni ile ile" wale waliowachagua walitarajiaje ifanye tofauti na inavyofanya kila siku! Kila baada ya miaka 10 huwa tunafanya sensa CCM huwa wanadhani wale wahesabuji huwa wanajifunza kuandika tarakimu kwenye makaratasi ya dodoso wanazotumia kufanyia sensa? Hivi huwa wanaoni watu wanaongezeka hivyo na mahitaji yao pia yatongezeka??
 
Mkuu, naona umeandika tu bila ushahidi. Unaishi Mkoa gani Tanzania ambako kuna mgawo wa umeme?

Hata kama una cheo serikalini ndugu ni bora some time ukawa na na mchango utakaosaidia nchi isonge mbele. Mikoa karibu yote Kuna mgao. Nilikua Iringa juzi ni mgao, Leo nipo Tukuyu Mbeya toka asubuhi ya saa 1 hakuna umeme. Tuache maigizo kwenye mambo ya msingi jamani
 
Mkuu, naona umeandika tu bila ushahidi. Unaishi Mkoa gani Tanzania ambako kuna mgawo wa umeme?

Nipo Mwanza, umeme sehemu kubwa ya jiji unakuja usiku na unakatwa asubuhi...Plus wewe upo tanzania nzima kwa wakati mmoja? kuwa na akili kidogo basi. ushahidi wako uko wapi?
 
Mkuu unaposema mradi wa gesi ni white elephant hapo naona huitendei haki Serikali, juzi juzi hapa ndio gesi imefika Kinyerezi na mitambo ya kuzalisha umeme hipo kwenye majaribio muda si mrefu itakuwa run 2 full capacity sasa tatizo liko wapi! Hata kama umeme ungezalishwa Mtwara bado gesi ingesafirishwa kuja Dar kwa ajili ya matumizi viwandani na majumbani,hivo it counts little wapi unaweka kiwanda cha kufua Umeme sehemu zote lazima umeme usafirishwe kwenye grid ya Taifa na losses katika usafirishaji wa nishati ni zile zile,kitu kingine ni lini mvua zimeanza kunyesha si juzi juzi tu,kwa nini unailahumu Serikali kwamba imeshindwa kutumia neema ya mvua kuzalisha umeme wa kutosha kutoka kwenye hydro Power Stations,nani kakwambia mabwawa yanajaa maji instantly hata mvua ikinyesha kwa wiki moja!! Lawama lawama kila kona, as far as you guys are concern Serikali ya CCM haifai - kwa nini mko hivyo lakini?
 
kama hujui kitu ukiza kwanza siyo kukurupuka na mada za upotoshaji
Inaonekana hata hujui kama mradi huo unafanyakazi, we gesi ya kinyerezi unajua inatoka wapi?

Watu hatutaki ngonjera siasa zako pelekesha huko watu tunahoji kwann tumeambiwa umeme utakuwa historia gase tunayo vp tena leo mpk Ethiopia
 
Mkuu, naona umeandika tu bila ushahidi. Unaishi Mkoa gani Tanzania ambako kuna mgawo wa umeme?

Kumbe wewe unapenda porojo na mizaha. Yaani hujui kuwa kuna mgao mkali sana wa umeme?
 
Back
Top Bottom