Mradi wa Gesi Mtwara-Dar ni "White Elephant"?

Mradi wa Gesi Mtwara-Dar ni "White Elephant"?

Siyo kweli. Muhongo mbio Ethiopia kununua umeme baada ya kukiri gesi haitoshelezi mahitaji.
...Kama ni kununua umeme toka nje, hata Kongo inafaa, tena ni karibu zaidi. By the way, nani ana gharamia ujenzi wa njia. Itabidi tuelewane na waKenya pia. Complicated! ...Tunahitaji kujitegemea kiumeme, tunao uwezo huo!
 
Tanzania hatuna mgawo wa umeme. Ni wapi kuna huo mgawo? Sisi huku Songea hatuna kabisa ijapokuwa bado tunatumia umeme wa majenereta

SONGEA Isio Na Mgao Wa Umeme Unamaanisha SONGEA Hii Niishiyo Mimi Au Nyingine??
 
Hapa NJOMBE mjini umeme wenyewe ni shida,mgao kila mara
 
Hata kama una cheo serikalini ndugu ni bora some time ukawa na na mchango utakaosaidia nchi isonge mbele. Mikoa karibu yote Kuna mgao. Nilikua Iringa juzi ni mgao, Leo nipo Tukuyu Mbeya toka asubuhi ya saa 1 hakuna umeme. Tuache maigizo kwenye mambo ya msingi jamani


Mkuu huyu tumeshamzoea. Unajua siasa za kipuuzi zikizidi zinaharibu akili ya mtu kama mihadarati. Huku Urambo Tbr kila siku umeme unakatwa kwa masaa kati ya 5 - 12 halafu anatokea mtu anaendeleza siasa kwenye vitu vya maendeleo ya watu.
 
Tanzania hatuna mgawo wa umeme. Ni wapi kuna huo mgawo? Sisi huku Songea hatuna kabisa ijapokuwa bado tunatumia umeme wa majenereta
mkoa wa pwani kila siku hauna umeme kuanzia saa nee asubuhi mpaka saa moja usiku, ni wiki ya pili sasa
 
Mkuu unaposema mradi wa gesi ni white elephant hapo naona huitendei haki Serikali, juzi juzi hapa ndio gesi imefika Kinyerezi na mitambo ya kuzalisha umeme hipo kwenye majaribio muda si mrefu itakuwa run 2 full capacity sasa tatizo liko wapi! Hata kama umeme ungezalishwa Mtwara bado gesi ingesafirishwa kuja Dar kwa ajili ya matumizi viwandani na majumbani,hivo it counts little wapi unaweka kiwanda cha kufua Umeme sehemu zote lazima umeme usafirishwe kwenye grid ya Taifa na losses katika usafirishaji wa nishati ni zile zile,kitu kingine ni lini mvua zimeanza kunyesha si juzi juzi tu,kwa nini unailahumu Serikali kwamba imeshindwa kutumia neema ya mvua kuzalisha umeme wa kutosha kutoka kwenye hydro Power Stations,nani kakwambia mabwawa yanajaa maji instantly hata mvua ikinyesha kwa wiki moja!! Lawama lawama kila kona, as far as you guys are concern Serikali ya CCM haifai - kwa nini mko hivyo lakini?
Kweli unaipenda CCM ile ile loooh.
 
tutolee unafiki wako hapa. hakuna sehemu ambayo haina mgao wa umeme sasa hivi hapa nchini.

Mkuu, naona umeandika tu bila ushahidi. Unaishi Mkoa gani Tanzania ambako kuna mgawo wa umeme?
 
Juhudi za kuondoa tatizo la umeme zinaonekana kuwa ngumu kila kukicha, mvua nyingi zinazoendelea kunyesha nchi nzima zimeshindwa kupunguza mgao wa umeme, Mradi wa gesi Mtwara hadi Dar es Salaam ulitoa matumaini ya kumaliza tatizo la umeme nchi surprisingly tatizo linaendelea, mradi uliogharimu taifa ma billioni ya dola, huwa najiuliza hizi pesa za huu mradi zingetumika kujenga na kuzalisha umeme huko huko mtwara then ukaingia kwenye grid ya taifa manufaa yangekuwa makubwa kiasi gani?

Naomba kuwasilisha.


Nadhani kiwango chako cha Elimu ni kidogo sana
Gesi na umeme ni vitu viwili tofauti, kuleta Dar gesi ni lazima ujenge tena mitambo ya kuzalisha umeme.
mradi wa Kinyerezi una phases nne , sasa wamekamilisha phase one , wakija kumaliza nyingine tatu , upungufu wa umeme itakuwa historia
 
Eeh kwa kweli kua uyaone yan mtu macho yanamtoka kutetea umeme ambao watu tumeaminishwa na muda mrefu kuwa ungekuwa ni historia, walianza na wiki wakasema wanakamilisha kufunga mitambo tutumie gesi, na isingechukua wiki tatu, tatizo lingeisha,wapi, wakaja ooh kuna hitilafu, yan upumbavu mtupu sijui tulikoseaga wap maskin ya Mungu sie, watu kama ni kura wanapiga mambo ni yale yale watu wale wale, wapuuzi wengine humu wanakuja kutetea ujinga.
 
Nchi hii vituko haviishi sasa umeme utoke Ethiopia mpaka uje ufike ni lini?

Mkubwa Mzima hujui Mwendo kasi wa Umeme...! inaelekea hata Kuoga unaoga Uchi wewe...!
 
Asante mkuu kwa maelezo hayo, lakini swali a mdau lipo pale pale, kwa nini mitambo ya kinyerezi haikujengwa mtwara ili kupunguza gharama na losses ya gasi wakati wa usafirishaji? KUulikuwa na ulazima? au ndo white elephant?
 
Nadhani kiwango chako cha Elimu ni kidogo sana
Gesi na umeme ni vitu viwili tofauti, kuleta Dar gesi ni lazima ujenge tena mitambo ya kuzalisha umeme.
mradi wa Kinyerezi una phases nne , sasa wamekamilisha phase one , wakija kumaliza nyingine tatu , upungufu wa umeme itakuwa historia
Mwafrika utamjua. .sasa ulichoandika hapo kinaonyesha una PhD? Ningekupa ufafanuzi ila kwa kuwa u najiona msomi zaidi sina cha ziada
 
Niliposikia kauli ya prof muhongo nilitamani kujinyonga nife kabisa juzi tulikuwa tunaambiwa tutauza sisi leo tunaambiwa tutanunuwa sisi dah kweli gas imepewa wachina kwa miaka saba kwa majaribio ccm ccm mungu awalaani!
 
Wanabakia kusema hapakazi tu# wakati kuna gizaaaaa la mgao wa umeme
 
Trillions za cubic feet of CH4 are absolutely meaning less. JK ujinga au ujanja mshikaji?
 
Labda mzee mwanakijiji aje atuambie hii serekali anayoisifia na mabadiliko toka ccm ni ipi.

Punguza mahaba kwa wanaume wenzako mtoto wa kiume .
Nani kakwambia serikali ya magufuli ndiyo iliidhinisha na kusimamia huo mradi wa gesi? Mradi ukisainiwa na ngeleja na rais alikua kikwete na pm pinda. ww ungesubiri hadi kamati za bunge ziundwe na kuchambua huu mradi ili sisi wananchi tupate majibu na walafi wafike kwa magufuli akishindwa hapo una haki ya kutoa hizi dhihaka zako
 
Umeme utanunuliwa Ethiopia, umeme utauzwa nchi za nje... sijui sasa tumwamini nani.... katika kutii amri, wa kwanza akikuambia simama, baadae wapili akakuambia kaa! Akija mtu mwegine atakukuta umekaa.... hivyo amri ya mwisho ndio inayo exist..
UMEME UNANUNULIWA ETHIOPIA, ina maana hatuna umeme.. white elephant
 
ghana walikubwa na ishu kama hii,walikopa fedha nyingi wakawekeza kwenye gas at the end gas iliyokuja kupatikana ilikuwa ndogo sana, wamebaki na madeni makubwa yakulipa, tunaomba mungu yasitutokee hayo.
 
Back
Top Bottom