1. Darling
2. Dear
3. Sweet heart
4. Jina lake
5. Jina lake la utotoni
6. Jina la mama yake
7 jina lake la ukoo
8. Kimeo
9. *****
10. Mkosi
Interesting thread, Nimemsave Princess, yeye kanisave mobali na ngai.
Jina la baba yake !1. Darling
2. Dear
3. Sweet heart
4. Jina lake
5. Jina lake la utotoni
6. Jina la mama yake
7 jina lake la ukoo
Kabla sijamuoa nilisave jina lake tu "Jane", sikumoja nikawa naitafuta namba yake kwa jina hilo sikuipata kumbe alikwisha zi hack kimya kimya simu zangu na kujisave "Dear Sweetiee!; kwnye simu ya pili pia akajisave "Honey" na ya tatu "Lovely Wife 2be".......Nilipouliza kwa nini amefanya vile akanijibu eti "nitamtofautishaje yeye na akina Jane wangu wengine wa Tandale Uzuri, kwa Mfuga mbwa huko au wa kwa Mtogole???.. Hakanionya kama nitabadilisha basi atajua simpendi kabisa na sina nia ya kumwona yeye.
Afanaleki, fisrt day tu ya ndoa tupo "honey moon" kakorokocha tena simu zote, ya kwanza kajisave "lovely wife", ya pili "my heart" hii ya tatua akaweka "my darl"....Nikaja nikacheka tu "sikumuuliza akaniambia usibadilishe hivyo nilivyo save" .
Four yrs ya maisha sasa, nakumbuka siku moja tumegombana akachukua simu zangu nikiwa nje akabadilisha " akajisave" (Jane, ya pili "Wife"na ya tatu "Mama Joto (jina la mtoto wetu)
Nilipoingia ndani akamaka "sitaki uniiite tena "dear, darling wala honey,niite jina walilonipa wazazi wangu (Jane) au ukishindwa "mama Joto" na kwenye simu zako zote nimebadili" manake sioni kama una mapenzi ya kweli na mimi, naona kama najipendekeza kwako tu...(hasira kali). Nikacheka tu moyoni.
Baada ya siku kadhaaa, mambo yametulia tunakwenda sawa, naangalia simu nakuta amerejesha vibwagizo vile vile alivyobalisha. Nikamuuliza vipi, akasema "Loooh, wenzangu, unaweza kuweka "darling wako mwingine humo kwenye simu ukipata tatizo au ajali apigiwe yeye na mimi mkeo kipenzi nije kuadhirika bure, niwe wa mwisho kuja kwenye tukio!".....Nikamuuliza kwani mimi umeni save kama nani akajibu "we tena, loh, "karibu kila siku nakubadilishaga "Leo my husband" jana niliweka " my dearest mume wangu" wiki iliyopita ilikuwa "Swetiee mupenzi" .......
Kudadadeki, simu za kiganjani hizi bana!takusave vyovyote utakavyo lakini "mzigo" unatoka kama kawaida kwa wale aliowasave "GS - MABIBO SALOON", MAMA GATI, SHAMILA WA MIKOCHENI, ABUU WA CHAKULA CHA MBWA, SUZY-MSICHANA WA KAZI, DOREN -CBE nk nk