‘’Mpemba’’ amponza DCI, Diwani Athumani

Hili halihusiani na hayo. Kwanza amembiwa atapangiwa kazi nyengine hivyo hayahusu mambo ya hasnoo ambaye kesi yake ipo miaka mingi sasa.
Hapa kaondolewa sababu anajua alomuweka na kumuondoa mengine ni speculation
 
MsemajiUkweli Mwambie mkuu wa mkoa kuwa GSM ni wale walikuwa na biashara ya HSC ambao wewe umesema walinusa hatari wakabadili ngozi.

Mkuu wa Mkoa aliwaongoza GSM kwenda kujaenga jengo la dini akijua pesa zinazotumika si safi
Mkuu wa mkoa kamuongoza makamu wa Rais kushiriki shughuli iliyoandaliwa na Homeshopping a.k.a GSM

Ni wakati sasa mkuu wa mkoa atoke na kuwaeleza waumini wanaojengewa lile jengo uhalali wa msaada alioongoza, ni wakati amtake radhi makamu wa Rais kwa kumshirikisha na watu wasio na ithbati ya uadilifu

Ni wakati Ole Sendeka aagize kama alivyosema kwa Zitto, kwamba account na mali za mkuu wa mkoa zikaguliwe

Mkuu wa mkoa kuna harufu isiyo nzuri, msemajiukweli katusaidia. Mkuu wa mkoa anashiriki na watu wenye mashaka, tuna kila sababu ya kumtilia mashaka na kutilia mashaka uteuzi wake !
 
Mimi bado nipo na hoja ya MsemajiUkweli kuhusu Home shopping ambayo ni GSM

GSM inafanya kazi bega kwa bega na mkuu wa mkoa katika miradi kadhaa

Kuna ujenzi wa jengo la dini ambalo mkuu wa mkoa kwa kushirikiana na kampuni ya GSM ambayo msemajiukweli amesema in 'uchafu' kwa jina la zamani, wanauendeleza.

Ikumbukwe hili ni Jengo la waumini na linatakiwa lisiwe na shaka juu yake.
Leo Mkuu wa Mkoa kaongoza kampeni kwa kutumia GSM.

Pili, kuna ujenzi wa wodi za hospitali ambapo GSM wanashirikiana na mkuu wa mkoa . Makamu wa Rais naye akajikuta anashirikiana na GSM na hatimaye serikali nzima

Kuna kila sababu za kuhoji mahusiano ya mkuu wa mkoa na GSM ! hawa GSM wana interst gani na serikali?
Tunajua awamu iliyopita HSC waliiweka'mikononi' kwa kila hali, je, hili ndilo linataka kutokea tena?

Mkuu wa Mkoa ana la kueleza umma na safari hii hatudhani anapaswa kuachwa kama lile aliloagiza wananchi watwangwe na Polisi yeye atajibu

Hili linaenda mbali na kugusu uadilifu wa serikali hii! Mkuu wa mkoa ameweka uadilifu wa serikali katika kupambana na maovu katika mashaka makubwa!

Tunapaswa tuelezwe uhusiano wa Serikali ya Magufuli na GSM kupitia mkuu wa mkoa
 
Mimi bado nipo na hoja ya MsemajiUkweli kuhusu Home shopping ambayo ni GSM

GSM inafanya kazi bega kwa bega na mkuu wa mkoa katika miradi kadhaa

Kuna ujenzi wa jengo la dini ambalo mkuu wa mkoa kwa kushirikiana na kampuni ya GSM ambayo msemajiukweli amesema in 'uchafu' kwa jina la zamani, wanuendeleza.

Ikumbukwe hili ni Jengo la waumini na linatakiwa lisiwe na shaka juu yake.
Leo Mkuu wa Mkoa kaongoza kampeni kwa kutumia GSM.

Pili, kuna ujenzi wa wodi za hospitali ambapo GSM wanashirikiana na mkuu wa mkoa . Makamu wa Rais naye akajikuta anashirikiana na GSM na hatimaye serikali nzima

Kuna kila sababu za kuhoji mahusiano ya mkuu wa mkoa na GSM ! hawa GSM wana interst gani na serikali?
Tunajua awamu iliyopita HSC waliiweka'mikononi' kwa kila hali, je, hili ndilo linataka kutokea tena?

Mkuu wa Mkoa ana la kueleza umma na safari hii hatudhani anapaswa kuachwa kama lile aliloagiza wananchi watwangwe na Polisi yeye atajibu

Hili linaenda mbali na kugusu uadilifu wa serikali hii! Mkuu wa mkoa ameweka uadilifu wa serikali katika kupambana na maovu katika mashaka makubwa!

Tunapaswa tuelezwe uhusiano wa Serikali ya Magufuli na GSM kupitia mkuu wa mkoa

Sasa HSC itakuwaje GSM?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Sasa HSC itakuwaje GSM?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
Siyo maneno yangu, msemajiukweli kasema Homeshopping ndio wamebadili jina na sasa wanaitwa GSM.

Hao GSM ndio wanaoshughulika na ujenzi wa nyumba za waumini, lakini ni wale wale homeshopping

Ni hivi bibie, muuza viungo vya binadamu akipata pesa akaanzisha kampuni ya mabasi, halafu akaja kukujenga kanisa au msikiti, ile pesa bado ni haramu.
 
Sasa ulitaka niweke maoni yako?

Kwani wewe umebadilika?

Hii ni thread yangu na nina haki ya kuandika chochote kama sivunji taratibu na sheria za Jamiiforums.

Kama unadhani hakuna lolote unaloweza kuchagia katika maoni yangu, ungesoma na kuondoka tu.

Jamiiforums has no room for dictatorial mentality.
unachokiandika huku nikwaajili ya watu na watu wenyewe ndosisi!! Andika vizuri heading ibebe kilichomo ndani sio unaandika kama magazeti ya makorokocho...kubali kukosolewa jamaa
 
Mbongo ukishaweka kitu kwenye maandishi baasi umewaua. Juzi kuna chief accountant nimemtumia instructions zimeandikwa kila kitu in a simple way. Kasoma lkn bado kapiga simu anaulizia yaleyale yaliyoandikwa.
Huwajui wabongo...akikuuliza usidhani hajakuelewa hapo ndiyo anakupoteza...anajua yote
 
Huyu jamaa si ameshakamatwa tayari? Mbona mnakanyagana...nendeni hapo Keko mtamtambua
 
Kama humfahamu mtu anayejulikana kama ''mpemba'', ingia kwenye mtandao ya NGO zinazopambana na vita vya ujangili wa nyara za serikali au subiri kesi ya ''Malkia wa pembe za ndovu''.

Ukitaka kumfahamu ''mpemba'' pitia hii thread;
Katibu wa zamani wa Simba Hasonoo kortini kwa wizi wa pembe za ndovu

Watanzania wengi ni wagumu sana kubadilika!

Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan kila siku anawambia wabadilike kwa sababu zama zimebadilika lakini wameziba masikio na hawataki kubadilika.

Ndugu yangu Diwani Athumani alikuwa anadhani ni zama zileee ambazo unaweza kuweka uzio katika uchunguzi kwa sababu ya cheo chako au ukaribu wako na Ikulu na hakuna wa kuhoji kwa nini unaweka uzio .

Huu sio muda wa kukumbatia mitandao ya kijangili na kifisadi. Zama zimebadilika sana.

Kwa nini baadhi ya watu hawajifunzi kwa Home Shopping Center ambayo baada ya kunusa hatari iliyoko mbele wakaamua kujifilisi kisheria na kuibuka huku wamevaa ngozi nyingine kibiashara inayoitwa GSM Foundation.

Rais Magufuli kila mara anawaambia kama unafahamu ulikuwa unatenda dhambi za kisiasa na kiuchumi. Huu ni muda wa kutubu na kuachana na dhambi hizo.

Vita vya nyara za serikali imemuondoa Diwani Athumani.

Kuna wengine bado wako mbioni kusombwa na mafuriko.
 
Back
Top Bottom