Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
MsemajiUkweli inaonekana hana taarifa kwamba vinara wa ufisadi nchi hii ni HSC. Katika awamu iliyopita waliitia TRA hasara ya karibia TZS trilioni Tisa. Lakini pamoja na hayo, akiwa na jina lake la awali la @mwanadiwani,alikuwa mstari wa mbele kutetea viongozi waliokuwa wanakula na HSC. Leo hii anawatetea katika muktadha wa corporate law, inawezekana ni kwa sababu amewajengea ukumbi wao mpya wa mikutano Dodoma, ukumbi uliotumika kumpitisha mgombea wao mwaka jana. HSC anaendelea kuweka viongozi mfukoni, ana fadhili wateule wa Rais muadilifu, anawanunulia magari, anawapa posho za kujikimu, tukishangaa haya kutokea chini ya awamu hii yenye kuchukia ufisadi, MsemajiUkweli anajibu kwamba hayo hayaihusu serikali, ni suala la corporate law. Pengine anaweza kutuelimisha zaidi kuhusu Corporate Law kwa mapana zaidi.Ahaaaa hapa unatuambia jambo jingine pengine bila kufahamu, au umesahau au unachoma utambi
Hawa GSM si ndio wanaoshirikiana na Mkuu mmoja wa mkoa kujenga Hospitali na si ndio wanaosaidia kujenga jengo la dini moja chini ya mkuu huyo?
Au nitakuwa nimechanganya mambo!!!
MsemajiUkweli, katika muktadha wa corporate law, Kwanini Kitilya yupo ndani wakati liability yake is limited by shares in a company where hes a director? Corporate law inasemaje hapa. Waziri aliyepitisha dili ni marehemu; CEO wa kampuni ya akina Kitilya ambae ndiye aliyehusika moja kwa moja ni marehemu; CEO wa benki iliyotoa hizi Fedha alikamatwa, akabambikiwa kesi ya uraia na kukimbizwa nje ya nchi kwa amri asirudi tena. Baada ya hapo, kesi ndio ikafunguliwa. Mambo ya ajabu kabisa haya.
Lugumi nae, mnazuia mijadala ya bunge isionekane kisha huko ndani mlipojifungia mnampa mhalifu huyu siku tisini amalize kazi aendelee ili Kula maisha. Wahalifu wa escrow wanakingiwa kifua na awamu hii inayochukia ufisadi, wengine wanapewa na vyeo. MsemajiUkweli, nini kinaendelea kama sio ulaghai?