Mpaka sasa Wizara zilizohamia Rasmi Dodoma

Mpaka sasa Wizara zilizohamia Rasmi Dodoma

Nimesoma thread kuanzia mtoa mada na wachangiaji na kilichonistua ni kuwa mtoa mada hajatoa takwimu lakini kibaya zaidi wachangiaji nao hawana takwimu na wanaunga mkono hoja? Yaani kama stori za kwenye vijiwe vya kahawa. Natoa Pongezi zangu za dhati.
 
Hivi kile kipindi cha TBC kuhusu kuhamia dodoma bado kipo?
Utawala wa Herode huu,kazi ya illuminat ni kutesa binadamu,twendeni pole pole tu mungu atawapiga mapigo saba. watalia meeeee kama mbuzi.
 
Nilikaa tu na kujiuliza mpaka sasa ni wizara ngapi zimehamia rasmi Dodoma? waziri mkuu alisema angeongoza suala hilo la kuhamia Dodoma. Nadhani bado anamalizia kuhamisha vitu vyake pole pole maana huwa ananeda siku moja mbili anarudi tena town.

Tamko lilitolewa pasipo kuwa fikra yakinifu inawezekana ilitokea tu aliyetamka kutokana na hisia akajikuta ametamka. Na kwa bahati mbaya watanzania mambo ya masikhara huchukulia serious na mambo serious huchukulia masikhara. Suala la kuhamia Dodoma wengine walilichukulia ni jambo serious likaandikwa hata kwenye magazeti na kutangazwa sana kwenye vyombo vya habari. Wakajitokeza watu mbalimbali hata kuchangia jambo hilo kana kwamba ni jambo kuuuuubwa sana.

Likatokea jambo serious sana, maafa ya huko Kagera na hata sehemu kadhaa kuwa an njaa hili halijawa issue kubwa sana kwa kuwa, sijui.

Sasa turudi kwenye swali langu la msingi MPAKA SASA NI WIZARA NGAPI ZIMEHAMIA RASMI DODOMA?
Mkuu hawa watu hawako serious katika jambo lolote, waziri mkuu alihadaa watanzania kwamba ndio anahamia rasmi na akaondoka na kupokelewa kwa shangwe na mkuu wa mkoa na raia kibao wakijua neema imewashukia awamu hii..yapo wapi sasa? Hizi ni siasa za kilimbukeni.Taifa linaongozwa kwa kauli za kibabe na kebehi,limekosa dira wala vipaumbele.Hakika huu ndio uongozi ovyo kupata kutokea kutoka taifa lipate uhuru, haina maana waliopita hawakufanya makosa, lahasha, walifanya lakini sio katika kiwango hiki.
 
Urais sio mtu ni taasisi....... Urais sio jeshi la mtu mmoja na taasisi lazima iongozwe kwa misingi ya sheria, tathimini za kweli, ushauri wa kitaalam. Kwa sasa inaonekana haya yote yanakosekana!!!
 
Hii nchi ya "Mzuka" tu... Kile kilikuwa kipaumbele cha mwezi wa nane/ tisa 2016. Baadaye mwezi wa kumi/kumi na mbili 2016 ikaja issue ya "Faru John". Hivi sana tangu Dec 2016- February 2017 issue ni "Njaa na Ukame"....

Chezea Tz wewe, nchi inayoongozwa na "Wataalamu" i.e Madr, Professors na other "elites of the sort"

In short Issue ya kuhamia Dodoma ishasahaulika sasa.
 
Uunaa babuu nna Bibi uupande waaa baba nna mama inabiidi urudi ukaangalie hataaa mashamba huko

Mkuu si kila mtu anahusudu kuwa peasant. Hebu angalia hali za wakulima walivyochoka, si bora kukaa mjini na kubeti tu. Huwa nacheka nikisikia mtu anasema anamiliki heka 30 huko kijijini wakati hata hana nauli ya kuja mjini kusalimia ndugu na jamaa.
 
Sijui ni katiba au ni miongozo...lkn aliyeweka sheria kwamba tamko lolote la Rais ni amri halali huyu hakuvitendea haki vichwa milioni 42 vya waTz...matokeo yake viongozi huwa Maranyingi hukimbizana na vivuli vya wasio ya amini kwa sababu tu yametamkwa na mkuu hata km jambo kalisema kimasihara. Amri halali zote ingekuwa vzr zithibitishwe au kuamliwa na bunge kabla hazijaanza kutekelezwa coz hiki chombo kinavichwa Vingi vinavyowakilisha wtz hivyo uwezo wake wa kuchuja mambo ni mkubwa sana ukitumiwa unavyotakiwa.
 
Rais anadhani nchi inaongozwa na mtu mmoja,kumbe URAIS NI TAASISI ILIYOKAMILIKA, SIO MATAMKO YA BILA WATAALAM.
 
Aliyesema atahamia Dodoma ndani ya wiki ndie huyo anatutangazia kwamba nchi haina njaa.
Tunaanzaje kumuamini?
 
Nilikaa tu na kujiuliza mpaka sasa ni wizara ngapi zimehamia rasmi Dodoma? waziri mkuu alisema angeongoza suala hilo la kuhamia Dodoma. Nadhani bado anamalizia kuhamisha vitu vyake pole pole maana huwa ananeda siku moja mbili anarudi tena town.

Tamko lilitolewa pasipo kuwa fikra yakinifu inawezekana ilitokea tu aliyetamka kutokana na hisia akajikuta ametamka. Na kwa bahati mbaya watanzania mambo ya masikhara huchukulia serious na mambo serious huchukulia masikhara. Suala la kuhamia Dodoma wengine walilichukulia ni jambo serious likaandikwa hata kwenye magazeti na kutangazwa sana kwenye vyombo vya habari. Wakajitokeza watu mbalimbali hata kuchangia jambo hilo kana kwamba ni jambo kuuuuubwa sana.

Likatokea jambo serious sana, maafa ya huko Kagera na hata sehemu kadhaa kuwa an njaa hili halijawa issue kubwa sana kwa kuwa, sijui.

Sasa turudi kwenye swali langu la msingi MPAKA SASA NI WIZARA NGAPI ZIMEHAMIA RASMI DODOMA?
Mtendaji mkuu wa shughuli za serikali ni waziri mkuu, kwa hiyo kama waziri mkuu yupo Dodoma basi serikali ipo tayari kule
 
nakumbuka kairuki alivokua anapaza sauti kama anataka kutafuna mic "waziri mkuu hawezi kwenda sisi tubaki nyuma lazma tutangulie"
ovyo sana
 
Back
Top Bottom