Motsepe Rais wa CAF, ni boss wa Mamelod na rafiki wa Hersi, Mechi na Yanga QF haipo

ubarinolutu

JF-Expert Member
Oct 22, 2012
1,964
3,895
Mimi kama shabiki wa Soka na mfuatiliaji wa Ligi ya NBC, nimefurahi yanga kufuzu lakini na Simba Ina chance ya kufuzu 50/50.
Kwa uwelewa wangu timu sita tayari zimeingia robo fainali, ikiwemo mamelod na Yanga na Al ahly. Ukiangalia Kwa upande wa Yanga timu ambayo inaweza kumsumbua robo fainali ni Mamelod tu kwani Al ahly wapi kundi moja hawawezi kupangwa pamoja.
Kwakuwa mpira wa Africa au Soka duniani Huwa Kuna fugusu za ndani Kwa ndani, hivyo sioni Yanga ikipangwa na Mamelod ya Africa Kusini na sababu zikiwa ni mbili tu

1. Mmiliki wa Mamelod sundown ni Rais wa CAF, tajiri motsepe ambaye ana utajiri mara mbili zaidi ya ule wa MO, Mamelod wamewinda hili kombe muda mrefu hivyo rais wa CAF hatokubali kuipatia timu yake timu ngumu inayoweza kumsumbua. Hivyo naamini Kwa figisu za Africa , Mamelod hatopewa Simba, Wala Yanga, na kwakuwa al ahly ataongoza kundi pia Mamelod hatopewa al ahly, Kwa tafsiri Hiyo Robo fainali ya Simba atacheza na Al ahly.

2. Engineer Hersi kwakuwa amechaguliwa nafasi nyeti sana CAF, na pia ana ukaribu mkubwa na Rais wa CAF motsepe, hivyo engineer Hersi ataendelea kufanya kazi ya kuisaport yanga ndani na nje ya uwanja , na hivyo kuhakikisha robo fainali Yanga hapangwi na Mamelod .

Kwahiyo uwezekano wa timu zetu kuingia nusu fainali ni mkubwa sana. Na tutarajie watu kuzimia zaidi
 
Mimi kama shabiki wa Soka na mfuatiliaji wa Ligi ya NBC, nimefurahi yanga kufuzu lakini na Simba Ina chance ya kufuzu 50/50.
Kwa uwelewa wangu timu sita tayari zimeingia robo fainali, ikiwemo mamelod na Yanga na Al ahly. Ukiangalia Kwa upande wa Yanga timu ambayo inaweza kumsumbua robo fainali ni Mamelod tu kwani Al ahly wapi kundi moja hawawezi kupangwa pamoja.
Kwakuwa mpira wa Africa au Soka duniani Huwa Kuna fugusu za ndani Kwa ndani, hivyo sioni Yanga ikipangwa na Mamelod ya Africa Kusini na sababu zikiwa ni mbili tu

1. Mmiliki wa Mamelod sundown ni Rais wa CAF, tajiri motsepe ambaye ana utajiri mara mbili zaidi ya ule wa MO, Mamelod wamewinda hili kombe muda mrefu hivyo rais wa CAF hatokubali kuipatia timu yake timu ngumu inayoweza kumsumbua. Hivyo naamini Kwa figisu za Africa , Mamelod hatopewa Simba, Wala Yanga, na kwakuwa al ahly ataongoza kundi pia Mamelod hatopewa al ahly, Kwa tafsiri Hiyo Robo fainali ya Simba atacheza na Al ahly.

2. Engineer Hersi kwakuwa amechaguliwa nafasi nyeti sana CAF, na pia ana ukaribu mkubwa na Rais wa CAF motsepe, hivyo engineer Hersi ataendelea kufanya kazi ya kuisaport yanga ndani na nje ya uwanja , na hivyo kuhakikisha robo fainali Yanga hapangwi na Mamelod .

Kwahiyo uwezekano wa timu zetu kuingia nusu fainali ni mkubwa sana. Na tutarajie watu kuzimia zaidi
Uchawi kweli si lazima upande ungo. Si bora tu uweke wazi we shabiki lialia wa simba. Si juzi juzi mlikubwa mnasema Hersi hawamjui anajipendekeza kwao kule S.A sasa leo kawa rafiki mkubwa wa Motsepe tena?
Tena mkasema hicho cheo alichogombea hakina lolote leo kimekuwa kikubwa tena....
Kweli dunia ina mambo
 
Dah,sheria ya shilingi ndio ilitunyima nusu fainali
 

Attachments

  • FB_IMG_17089618746562490.jpg
    FB_IMG_17089618746562490.jpg
    391.5 KB · Views: 6
Nimeishia hapo juu kuwa simba ni timu bora na Mamelodi hawatapewa hiyo. Simba ina ubora gani? Kwanza imeshapita kwenye Robo?
 
Motsepe angekuwa na huo uwezo hao Mamelodi wangeshabeba champs league toka ameingia madarakani. CAF ni taasisi na sio MTU mmoja mwenye nguvu ya kuamua vitu
 
Back
Top Bottom