JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,462
Watu wengi wanaoishi katika nyumba hii ya upangaji wameshindwa kutoa mali zao ndani ya nyumba, baadhi yao wapo pembeni wanalia hasa kina mama.
Chanzo inadaiwa ni shoti ya umeme, mpaka naandika hapa bado moto unaendelea na nyumba hiyo ya ghorofa moja inazidi kuteketea, kuna hatari moto unaweza kusababisha madhara mengine pia katika nyumba za jirani.
============
Gari la zima moto ndio limefika muda huu linapambana kuzima moto lakini tayari sehemu ya juu ya nyumba hiyo imeshaungua yote na imeanguka, sasa moto unaelekea sehemu ya nyumba ya chini.