Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,904
Moto umeshamaliza kazi yake, umeteketeza majengo ya ghorofa yasiyopungua manne na hasara mbalimbali, pengine vifo na majeruhi pia! Bila kusahau usumbufu mkubwa kwa wapita njia.
Kikosi cha zimamoto kiko chini ya kilometre moja toka eneo la ajali lakini kuna magari ya zimamoto ya makampuni binafsi ndani ya kariakoo na maeneo ya jirani.
Mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio wanasema moto ulianzia chini kwenye mirunda iliyoshikilia zege la ghorofa ya kwanza lililokuwa linaendelea kujengwa
Kwakuwa haukuwa mlipuko ina maana moto ulishika kasi na kuenea maeneo mengine kwa kasi inayodhibitika..! Magari ya zimamoto moto yalifika kwa wakati pamoja na kikosi kizima.. Lakini upungufu wa maji ukawa tatizo..mabomba ya maji ya dharura yalikuwa kama mapambo hayakuwa na maji.. Moto ukasambaa kwa raha zake toka jengo moja hadi lingine huku kikosi cha uokoaji kikifanya juhudi za kuuzima bila mafanikio tarajiwa
Minong'ono eneo la tukio ilikuwa mingi.. Wengine wakisema ni hujuma wengine wakisema ni mchongo.. Maana kikosi cha zimamoto kisingeshindwa kuuzima moto kama ule wakati unaanza
Tutarajie kuundwa tume na pengine ripoti ya polisi vitakavyoacha maswali mengi kuliko majibu ama jawabu la mioto isiyoisha!
Umafia, ubabe na ujasusi wa biashara za Kariakoo | Page 2 Umafia, ubabe na ujasusi wa biashara za Kariakoo
Pia soma: Soko la Kariakoo lateketea kwa moto
Sent using Jamii Forums mobile app
Kikosi cha zimamoto kiko chini ya kilometre moja toka eneo la ajali lakini kuna magari ya zimamoto ya makampuni binafsi ndani ya kariakoo na maeneo ya jirani.
Mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio wanasema moto ulianzia chini kwenye mirunda iliyoshikilia zege la ghorofa ya kwanza lililokuwa linaendelea kujengwa
Kwakuwa haukuwa mlipuko ina maana moto ulishika kasi na kuenea maeneo mengine kwa kasi inayodhibitika..! Magari ya zimamoto moto yalifika kwa wakati pamoja na kikosi kizima.. Lakini upungufu wa maji ukawa tatizo..mabomba ya maji ya dharura yalikuwa kama mapambo hayakuwa na maji.. Moto ukasambaa kwa raha zake toka jengo moja hadi lingine huku kikosi cha uokoaji kikifanya juhudi za kuuzima bila mafanikio tarajiwa
Minong'ono eneo la tukio ilikuwa mingi.. Wengine wakisema ni hujuma wengine wakisema ni mchongo.. Maana kikosi cha zimamoto kisingeshindwa kuuzima moto kama ule wakati unaanza
Tutarajie kuundwa tume na pengine ripoti ya polisi vitakavyoacha maswali mengi kuliko majibu ama jawabu la mioto isiyoisha!
Umafia, ubabe na ujasusi wa biashara za Kariakoo | Page 2 Umafia, ubabe na ujasusi wa biashara za Kariakoo
Pia soma: Soko la Kariakoo lateketea kwa moto
Sent using Jamii Forums mobile app