Kumekuwapo wimbi la vijana kupeana motisha za ajabu; mara siku hizi hatari kubwa kwa vijana Tanzania si kukosa ajira bali ni kukosa skills, mara AI ndiyo future na vijana wawekeze katika kujifunza teknolojia ya AI, mara dini ndiyo sababu kuu ya umasikini Tanzania; mara wasomi (shule) haina umuhimu wowote; kasumba ya kuwaaminisha vijana (hasa kupitia mitandao ya kijamii) kwamba hela ipo mtaani, ni kwamba vijana hawataki kufanya kazi, na bla bla nyingi.
Lakini Tanzania hii inayoongozwa na Serikali ya CCM kwa zaidi ya miaka 60 bado inahangaika kupata mahitaji ya msingi: chakula, maji, makazi, mavazi na umeme. Unawezaje kuwekeza katika skills za teknolojia ya juu sana wakati Serikali yako imefeli vibaya kutatua mahitaji ya msingi ambayo asilimia kubwa ya Watanzania hawana? Tunahitaji kutatua matatizo ya kweli hapa kabla ya kuanza kulaumu wasomi, au kuwekeza katika AI skills ndogo ndogo (ingawa ni muhimu).
Kati ya watu milioni 68, watu milioni 47 hawana upatikanaji wa maji safi; takribani watu milioni 36 bado hawana umeme wa uhakika mwaka 2024; takribani asilimia 59 ya kaya haziwezi kumudu lishe yenye virutubisho.
CCM, acheni kujificha nyuma ya kichaka cha kauli kwamba vijana wajifunze skills, AI, na propaganda za mitandaoni kwamba hela ipo mtaani, ilhali mamilioni ya Watanzania wanashindwa kupata mahitaji ya msingi: chakula, maji, makazi, mavazi na umeme.
Wajibikeni.
Lakini Tanzania hii inayoongozwa na Serikali ya CCM kwa zaidi ya miaka 60 bado inahangaika kupata mahitaji ya msingi: chakula, maji, makazi, mavazi na umeme. Unawezaje kuwekeza katika skills za teknolojia ya juu sana wakati Serikali yako imefeli vibaya kutatua mahitaji ya msingi ambayo asilimia kubwa ya Watanzania hawana? Tunahitaji kutatua matatizo ya kweli hapa kabla ya kuanza kulaumu wasomi, au kuwekeza katika AI skills ndogo ndogo (ingawa ni muhimu).
Kati ya watu milioni 68, watu milioni 47 hawana upatikanaji wa maji safi; takribani watu milioni 36 bado hawana umeme wa uhakika mwaka 2024; takribani asilimia 59 ya kaya haziwezi kumudu lishe yenye virutubisho.
CCM, acheni kujificha nyuma ya kichaka cha kauli kwamba vijana wajifunze skills, AI, na propaganda za mitandaoni kwamba hela ipo mtaani, ilhali mamilioni ya Watanzania wanashindwa kupata mahitaji ya msingi: chakula, maji, makazi, mavazi na umeme.
Wajibikeni.