Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Mussa Kaswahili amesema eneo hilo la Mizani barabara Kuu ya Morogoro kuelekea Iringa, awali lilikuwa na mzani mmoja, lakini Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kuboresha na kuongeza mzani husika.
Amesema: “Awali ilikuwa lazima magari yote yapimwe, lakini maboresho mapya yatachuja magari yanayotakiwa kupimwa na mengine yatakayoonesha yanatakiwa kupimwa yataingia katika mzani.”