Mwl.RCT
JF-Expert Member
- Jul 23, 2013
- 13,580
- 18,615
WATU wawili wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha basi la Kampuni ya Abood na Noah zilizogongana uso kwa uso asubuhi ya leo Septemba 11, 2023 eneo la Kitungu Manispaa ya Morogoro.
Ajali hiyo imehusisha basi lenye namba za usajili T904 DKY mali ya Kampuni ya Abood iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Morogoro na gari ndogo aina ya Noah yenye namba za usajili T828 DNB iliyokuwa ikitokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam.
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro umethibitisha kupokea miili ya watu wawili pamoja na majeruhi wawili.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, ACP Alex Mkama amezungumzia kutokea kwa ajali hiyo huku chanzo kikitajwa kuwa uzembe wa dereva wa basi la Abood.
Ajali hiyo imehusisha basi lenye namba za usajili T904 DKY mali ya Kampuni ya Abood iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Morogoro na gari ndogo aina ya Noah yenye namba za usajili T828 DNB iliyokuwa ikitokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam.
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro umethibitisha kupokea miili ya watu wawili pamoja na majeruhi wawili.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, ACP Alex Mkama amezungumzia kutokea kwa ajali hiyo huku chanzo kikitajwa kuwa uzembe wa dereva wa basi la Abood.