MOI Wajiunga Tena na MGOMO

MOI Wajiunga Tena na MGOMO

Si ndio maana wamemuachia Muhimbili yake hawana shida na mshahara wake akawaleta hao wa Iran waliomhonga suti watibu wananchi

Well done , ndivyo wanavyotakiwa kufanya na mie nawapongeza kwa hatua yao hiyo, ila mpaka sasa hakuna aliyeandika barua yakuacha kazi , na naomba uwashauri sasa waandike barua ili km kuna mafao yao yaweze kuwa processed , wapewe na waondoke wakatafute maslahi wayatakayo.
 
Oyoo! walimu lin jama tunasubiri? je wafanyakaz? vp kuhusu wanafunz? duu mkulima mbona kimya? na bado bas ziendao mkoan
 
mi nilikua muhimbili mida ya asubuhi kujionea mwenyewe kinacho endelea. nimefanya ukaguzi wangu kama raia mwenye haki hiyo. mbona kazi inaendelea kama kawaida. madaktari waliovaa makoti meue nimewaona wengi. nimehoja baadhi ya wagonjwa wanahudumiwa. labda kama mgomo umeanza mida hii!

jambo lingine ni kwamba wale madaktari ni wasomi. sidhani kama wanaweza kukubali kisha baada ya muda wakagoma tena. tuache kupotosha umma wa watanzania
 
Msimamo mbona JK aliisha utoa kwenye hotuba yake ? alisema hawana haja yakugoma na kumsumbua mwajiri kuwaandikia barua nk, wao waache kazi waende kwenye maslahi bora wayatakayo,.....

Yaani awa madaktari kama wangeitisha mgomo wa kutaka bei za bidhaa na kodi zipunguzwe tungewaelewa ila wamekuwa wabinafsi sana, nadhani sio kosa lao ila kumbukeni hii awamu ya JK imezalisha vichaa wengi nadhani kutokana na ugumu wa maisha.
 
Homa inapanda na kushuka,
Wananchi sasa ndo watagoma barabarani kwa niaba ya madokta

Peleka mawazo ya ndumu na viroba huko.WAGOME wananchi ili iweje na wagome nini usitufanye na sisi mapoyoyo kama nyie CDM
 
7.7 m kwa alietoka direct from school, je mwenye miaka 30 ya uzoefu analipwa shilingi ngapi?

Tafakari chukua hatua

say no to boycott, say no to mob psychology

say yes to humanity, say yes to logical thinking
 
Hayo maslahi wanayoyataka Rais JK aliisha waambia hayawezekani, na akawapa na suluhisho kuwa kama hayawezekani na wao waache kazi, mbona kitu ni rahisi tu na ww kwa nn usitumie muda wako kuwashauri waache kazi tu?

Mbona yeye na mawaziri wake wamekuwa wakitakiwa kujiuzuru hawajiuzuru/hawataki unadhani kwa nini? hebu tafakari hapo?
 
Well done , ndivyo wanavyotakiwa kufanya na mie nawapongeza kwa hatua yao hiyo, ila mpaka sasa hakuna aliyeandika barua yakuacha kazi , na naomba uwashauri sasa waandike barua ili km kuna mafao yao yaweze kuwa processed , wapewe na waondoke wakatafute maslahi wayatakayo.
Waandike barua kwa nani wao siwameondoka Huyo Mbuzi wako Kikwete si awafukuze hana jpya amebaki kutumbua mimacho he has failed the nation poor leader
 
Nadhani sio kujiunga tena na mgomo, la hasha mgomo bado unaendele na hukuwai kwisha toka umeanza!!!! na kwa sasa Lugalo imepewa hadhi ya hospitali ya rufaa....haaaa!!! kuokoa jahazi....!!!!
 
Hayo maslahi wanayoyataka Rais JK aliisha waambia hayawezekani, na akawapa na suluhisho kuwa kama hayawezekani na wao waache kazi, mbona kitu ni rahisi tu na ww kwa nn usitumie muda wako kuwashauri waache kazi tu?

msiongee kwa ushabiki angalieni hali halisi hata hao anajeshi wenyewe wanahali mbaya usifikiri kuwa wanaraha sana. Taaluma za watu ziheshimike sasa wanateua hospitali ya Lugalo kuwa ya Rufaa je inawataalamu wenye sifa za Rufaa? wanavifaa? Kama walishindwa kununua vyombo kuweka muhimbili je wataweza kuweka Lugalo? Ama nini maana ya Hospitali kuitwa ya Rufaa?
 
msiongee kwa ushabiki angalieni hali halisi hata hao anajeshi wenyewe wanahali mbaya usifikiri kuwa wanaraha sana. Taaluma za watu ziheshimike sasa wanateua hospitali ya Lugalo kuwa ya Rufaa je inawataalamu wenye sifa za Rufaa? wanavifaa? Kama walishindwa kununua vyombo kuweka muhimbili je wataweza kuweka Lugalo? Ama nini maana ya Hospitali kuitwa ya Rufaa?

Juzijuzi hapa wajerumani ndio waliiboresha Lugalo hata grade one haizidi vyumba 20
 
MOI hawakujua kuwa kurudi jana kazini ilikuwa ni mbinu ya kukatisha mwendelezo wa kutokuwepo kazini kwa zaidi ya siku tatu kinyume cha sheria mwajiriwa anahesabika kuwa amejifukuza kazi. Wanaanza tena leo na wataaendelea na mgomo mpaka wiki ijayo ambapo watarudi tena siku moja au mbili wanagoma tena

Sheria ni siku 5 hujaonekana kazini unajifukuzisha kazi walishaifanyia marekebisho na imeshaanza kutumika muda mrefu, kuwa usipoonekana kazini siku 5 mfululuzo umejifukuzisha kazi. So walichofanya MOI n kuonekana kazini then wanarudi tena kwenye A kama wameanza mgomo leo unaesabu siku 5 za kazi wanarudi tena mchezo huo wataucheza weee hadi watakapo pata majibu ya matakwa yao

 
Msimamo mbona JK aliisha utoa kwenye hotuba yake ? alisema hawana haja yakugoma na kumsumbua mwajiri kuwaandikia barua nk, wao waache kazi waende kwenye maslahi bora wayatakayo, shida iko wapi ? na kwa nn usiwashauri wafuate ushauri wa Rais wakuacha kazi?
Waache kazi kwasababu ya udhaifu wa mtu ambaye ameshindwa kutawala?
 
Nadhani sio kujiunga tena na mgomo, la hasha mgomo bado unaendele na hukuwai kwisha toka umeanza!!!! na kwa sasa Lugalo imepewa hadhi ya hospitali ya rufaa....haaaa!!! kuokoa jahazi....!!!!

Ni rahisi tu mbona; sekondari nyingi sasa hivi zinaitwa vyuo, shule za msingi nyingi sasa zinaitwa sekondari, vyuo vingi sasa hivi vinaitwa vyuo vikuu ila hawana majengo na hata vifaa vya maabara hii ndo tanzania bhana. Miji mingi sasa hivi inaitwa majiji. Pale Lugalo wameongeza wodi? maaabara ama wameiita tu ya Rufaa? Tatizo letu la kutibu dalili badala ya chanjo
 
7.7 m kwa alietoka direct from school, je mwenye miaka 30 ya uzoefu analipwa shilingi ngapi?

Tafakari chukua hatua

say no to boycott, say no to mob psychology

say yes to humanity, say yes to logical thinking

wewe umesoma na Mwigulu nchemba, nimeambiwa alikuwa anadesa kwako, naamini kwa jinsi mnavyofanana iq.
 

Nasisitiza


Hakuna mgomo muhimbili, after all wagonjwa wa rufaa wanapelekwa LUGALO.
Vip ule Mgomo wenu wa Sensa bado mmeshikilia ule msimamo wenu? Naona lile zoezi lenu la kujihesabu limekuwa gumu mlikuwa mnafikiri zoezi la sensa ni sawa na kuhesabu vikombe vya kahawa na kashata?
 
Ni baada ya mabadiliko ya hali ya Ulimboka.
Wagonjwa waliokwishalipia tu ndo wanaonwa leo.
Emergence yasimama.
Source: Mimi niko ground zero
Mimi na familia yangu tunawaunga mkono, komaeni.....................
 
Back
Top Bottom