Ni makosa makubwa Sumatra kufungia Kampuni ambayo mabasi yake yamehusika kwenye ajali bila kufanya uchunguzi wa kina. Kinachotakiwa kufanywa ni kuangalia kama chanzo cha ajali kinatokana na Kampuni kama Kampuni au Dereva kama Dereva. Kuna makosa ya Kampuni na Makosa ya Madereva. Mfano Basi ambalo lime-overtake sehemu ambayo hairusuwi ku-overtake (mfano kwenye kona) na kusababisha ajali huwezi sema chanzo ni Kampuni ya hilo Basi. Hapo chanzo ni Dereva wa Basi personally . Wa kumfungia hapa ni Dereva na siyo Kampuni, unless idhibitike kwamba Dereva aliyekuwa anaendesha (yaani ameajiriwa na Kampuni) hakuwa na Leseni ya Udereva kutoka mamlaka husika.
Aidha inapotokea Basi limepinduka kutokana na kupasuka kwa tairi na uchunguzi ukagundua kwamba tairi za Basi husika zilikuwa zime-expire au zilikuwa zimejazwa upepo kupita kiasi hapo obvious wa Kufungia ni Kampuni. Lakini ikigundulika kwamba tairi hazija-expire na zilikuwa zimejazwa vizuri wakushughulikwa nae ni Mzalishaji wa Tairi kupitia TBS.
Sasa katika mazingira haya ya polisi kugongwa uso kwa uso na Mohamed Trans tusilaumu kwanza Mohamed Trans hadi hapo tutapojua dhahiri chanzo cha ajali ni nini. Na bahati mbaya sana katika hii kesi Injury peoples ambao ni Police ndiyo watakaopima ajali na kufungua kesi Mahakamani. Sijui kama kutakuwa na Justice. Ajali ya kugongwa Nyani anaenda kupima Ngedere na Ngedere huyo huyo anaipeleka kesi Mahakamani.