domokaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2010
- 3,545
- 1,719
Nimesoma maandishi ya Mohamed Said na nimegundua kama kila mtu angekuwa kama yeye nchi hii isingefika hapa ilipofika. Mohamed Said ni shujaa anayethubutu kusema yale ambayo wengi wetu wanayaogopa kuyasema.
Tungekuwa na ujasiri wa kuyasema leo wabunge wetu wasingedai posho nyingi namna hii, mgomo wa madaktari, Madudu ya TBS, uwongo dhahiri wa viongozi wa juu wa nchi yetu na mengine lukuki hayeshi nikiyaandika hapa. Yote hii imetokana na tabia ya unafiki wa kutaka kujua sisi ni akina nani hasa, tuna silika zipi na tumetoka wapi.
Tunakataa migongano ya mawazo na otofauti wa fikra ambao ndiyo ungetupelekea kupata maarifa mapya na badala yake tunasema huyu anatuvuruga, huyu anavuruga amani, tunataka kila mtu afikiri sawa na mwengine, kila uongo unaosemwa na waloutengeneza tunauamini. Mtu akidai haki yake eti yeye si mzalendo, mzalendo ni yule anayekubali kuonewa.ema hawa walafi na wana upendeleo kwa sababu tu hauko nao imani moja unaitwa wewe mdini.
Miaka itapita iko siku watu wataujua ukweli watamtafuta Mohamed Said awaelekeze watamkosa, watayatafuta majambia.
Tungekuwa na ujasiri wa kuyasema leo wabunge wetu wasingedai posho nyingi namna hii, mgomo wa madaktari, Madudu ya TBS, uwongo dhahiri wa viongozi wa juu wa nchi yetu na mengine lukuki hayeshi nikiyaandika hapa. Yote hii imetokana na tabia ya unafiki wa kutaka kujua sisi ni akina nani hasa, tuna silika zipi na tumetoka wapi.
Tunakataa migongano ya mawazo na otofauti wa fikra ambao ndiyo ungetupelekea kupata maarifa mapya na badala yake tunasema huyu anatuvuruga, huyu anavuruga amani, tunataka kila mtu afikiri sawa na mwengine, kila uongo unaosemwa na waloutengeneza tunauamini. Mtu akidai haki yake eti yeye si mzalendo, mzalendo ni yule anayekubali kuonewa.ema hawa walafi na wana upendeleo kwa sababu tu hauko nao imani moja unaitwa wewe mdini.
Miaka itapita iko siku watu wataujua ukweli watamtafuta Mohamed Said awaelekeze watamkosa, watayatafuta majambia.