TANZIA Sheikh Hassan Mohamed Said Kinyozi Mpigania Uhuru na Mmoja wa Waasisi wa TANU Lindi amefariki Dunia

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,912
30,253
Jioni hii imenifikia taarifa kutoka Lindi kuwa Hassan Mohamed Said Kinyozi mmoja katika vijana waliowasha moto wa kupigania uhuru wa Tanganyika Southern Province, yaani Jimbo la Kusini amefariki dunia akiwa na umri wa kiasi cha miaka 90.

Nakumbuka kama jana siku nilipofika Lindi kwa basi dogo nikitokea Mtwara.

Barabara ya Lindi Mtwara ilikuwa mbovu sana miaka ile basi likiendeshwa kwa tahadhari kubwa.

Nakumbuka tulipoingia Lindi tunaelekea stendi natazama yale mandhari ya mji nageuza shingo huku na huku zile nyumba naziona mfano wa nyumba za Mtaa wa Swahili Dar es Salaam miaka ya 1950.

Nami nimo katika basi la Dar es Salaam Motor Transport (DMT) natokea Moshi shule nakuja likizo Dar es Salaam.

Nakumbuka nilikuwa nakabidhiwa kwa dereva Kapesa Johari kijana wa Gerezani kwani nilikuwa bado mdogo niko shule ya msingi hata uhuru bado.

Niko Lindi ndani ya basi naangalia minazi na nyumba zilizoezekwa kwa makuti.

Hii Lindi machoni kwangu ilikuwa sawasawa na Dar es Salaam ya udogoni kwangu.

Nilikuwa katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes na mwaka ulikuwa wa 1993.

Hassan Mohamed Said Kinyozi amefariki.

Nimemtaja shujaa mzalendo huyu Maalim Hassan Mohamed Kinyozi, mtoto wa Sheikh Kinyozi aliyekuwa anaendesha moja ya madrasa maarufu mjini Lindi iliyofahamika kama Madrasa ya Sheikh Kinyozi.

Madrasa hii bado ipo hadi leo na baada ya kifo cha baba yake marehemu Hassan Kinyozi alisimamia chuo hiki na kuendelea kusomesha hadi kifo kilipomchukua hii leo.

Kuna mtu alinikumbuka wakati nilipokwenda Lindi kufanya utafiti na mahojiano na Rashid Salum Mpunga na Yusuf Mohamed Chembera.

Huyu ndiye aliyenitafuta na kunipa taarifa ingawa hatukupata kuonana tena toka mwaka ule wa 1993.

Ukisoma kitabu cha Abdul Sykes nikieleza historia ya TANU ni nani walioasisi chama cha TANU hapo Lindi utasoma maneno haya:

''...hawa wawili Ahmed Seif na Hassan Mohamed Kinyozi walikuwa ndiyo wafanyakazi wa kwanza wa TANU waliokuwa wakilipwa mshahara Southern Province.

Kwa ajili hii wakawa miongoni mwa wafanyakazi wachache sana walioajiriwa na TANU kwa wakati ule.

Suleiman Masudi Mnonji alitoa nyumba yake katika mtaa wa Makonde kuwa ofisi ya kwanza ya TANU kusini yote.

Baada tu ya kuanzishwa kwa TANU, Athumani Mussa Lukundu, kiongozi wa Lindi Dockworker's Union, aliunganisha chama chake na TANU.

Jambo hili kwa TANU lilikuwa la kuitia moyo sana kwa sababu Dockworker's Union ilikuwa na wanachama wengi na hatua ile iliongezea TANU nguvu.''

Bahati mbaya sana kuwa majina haya niliyoyataja hapo juu hayamo katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Naamini si wengi hata hapo Lindi kwenyewe wanaifahamu historia hii ya mzee wetu Hassan Mohamed Said Kinyozi.

Waasisi wakuu wa TANU ukimtoa Suleiman Masudi Mnonji walikuwa vijana wawili - Rashid Salum Mpunga na Yusuf Mohamed Chembera.
Baada ya kupokea taarifa ya msiba huu nikaanza kupiga simu huku na huku kutafuta picha ya marehemu.

Mmoja katika marafiki zangu wazawa wa Lindi akanitumia picha ya marehemu ya mwaka wa 1954 wakati huo akiwa kijana mdogo sana aliyopiga na wazee wa mjini wengi wao walikuja si muda mrefu kuwa mstari wa mbele katika TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Angalia picha ya pili hapo chini:

1.Aliyeketi chini mbele kushoto ni Hassan Mohamed Saidi Kinyozi
2. Aliyekaa kwenye kiti nyuma ya Hassan Kinyozi ni Rashid Salum Mpunga.
3. Aliyefunga tai ameketi ni Yusuf Mohamed Chembera.
4 Picha ilipigwa Ghana Restaurant 1954 na hii ilikuwa vilevile ni ofisi ya Lindi Seamens Club mahali walipokuwa wanakutana wanamji kwa mazungumzo na kituo cha harakati za TANU.
Picha ya tatu ni Hassan Mohamed Said Kinyozi katika ujana wake.

Sheikh Hassan Kinyozi ni mtu maarufu hata kwa wale ambao leo hawaijui historia yake kama mpigania uhuru.

Mtoto wa dada yake Bi. Salma bint Rashid ni mke wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.

Marehemu anategemewa kuzikwa leo Jumatano hapo Lindi.
Tunamwomba Allah amsamehe makosa yake na amweke Pepo ya Fidaus.

Amin.
1668546812882.png
1668546840660.png
1668568054620.png
1668568171694.png
 
Kila muislamu mzee alianzisha tanu na kupigania uhuru.
Execute,
Siyo kila Muislam ni hao Waislam ambao walioanzisha na nimeandika kitabu hicho hapo chini.

Waliotafiti historia ya TANU kabla yangu waliliona hili na liliwatia hofu hawakutaka kulieleza.

Imetoka kwa Dar es Salaam waliounda African Association na TANU mimi ni wazee wangu na ndiyo nikapata ghera ya kuandika historia hii.

1668568441462.jpeg
 
Huo ndio ukweli au wewe ulitaka aseme wakristo wa kwenu chunya
Kuna mambo huwa yanashangaza sana tena sana kuhusu huyu mtoa mada huwa muda mwingine namfanananisha na sheikh Rogo, mfano mji wa Dar-es-Salaam wakati ule kabla haujawa na muingiliano mkubwa nikweli jamii kubwa walikuwa ni waislamu ambacho ni kitu cha kawaida kwa mikoa ya pwani,

Mimi binafsi natokea mkoa wa Mtwara ndiko kwetu na mwaka 2012 watu wa Mtwara walileta mgomo wa kuwa gesi haitoki hali ambayo ilileta machafuko makubwa mno hususani mkoa wa Mtwara wote,

Hamasa zilitoka kwenye mimbari za misikiti tofauti hapa mjini na kwenye majukwaa ya kisiasa kuwa gesi isitoke na kama unavyojua Mtwara asilimia 93% ni waislamu na pia nakumbuka mimi na ndugu zangu tulijihimu kabisa uwanja wa mashujaa kwenye kisomo cha albadir na hiyo siku uwanja ulifurika mno utadhani siku ya iddi vile,

Sasa je ni sahihi kuhusisha lile vuguvugu la kudai gesi na uislamu kisa eti wengi wao walikuwa waislamu?
 
Upuuzi mtupu wa hawa watu.
Execute,
Kwako inaweza historia hii ikawa ni upuuzi lakini baada ya kifo cha mzalendo huyu nimepokea simu na picha kutoka ndiugu zake zinisaidie katika kuandika taazia ya marehemu Hassan Mohamed Said Kinyozi.

Hakuna haja ya kutukana si ustaarabu kuiita taazia ni upuuzi.
Fikiria wewe angekufa ndugu yako na taazia yake ikaitwa upuuzi ungejisikiaje?

Kipi kilichokughadhibisha ndugu yangu?
Angalia Mtaa huo hapo chini.

Sheikh Mohamed Yusuf Badi alikuwa mmoja wa waasisi wa TANU na alipigania uhuru wa Tanganyika.

Mji wa Lindi umempa mtaa.
Angalia na picha ya Rashid Salum Mpunga shujaa mwingine aliyepigania uhuru wa Tanganyika na nimemwandikia kitabu yeye na Yusuf Mohamed Chemebera:



1668569145200.jpeg
1668569752203.jpeg
1668569783505.jpeg
 

Attachments

  • 1668569684544.jpeg
    1668569684544.jpeg
    7.6 KB · Views: 10
SHEIKH HASSAN MOHAMED SAID KINYOZI MPIGANIA UHURU NA MMOJA WA WAASISI WA TANU LINDI KAFARIKI DUNIA

Jioni hii imenifikia taarifa kutoka Lindi kuwa Hassan Mohamed Said Kinyozi mmoja katika vijana waliowasha moto wa kupigania uhuru wa Tanganyika Southern Province, yaani Jimbo la Kusini amefariki dunia akiwa na umri wa kiasi cha miaka 90.

Nakumbuka kama jana siku nilipofika Lindi kwa basi dogo nikitokea Mtwara.

Barabara ya Lindi Mtwara ilikuwa mbovu sana miaka ile basi likiendeshwa kwa tahadhari kubwa.

Nakumbuka tulipoingia Lindi tunaelekea stendi natazama yale mandhari ya mji nageuza shingo huku na huku zile nyumba naziona mfano wa nyumba za Mtaa wa Swahili Dar es Salaam miaka ya 1950.

Nami nimo katika basi la Dar es Salaam Motor Transport (DMT) natokea Moshi shule nakuja likizo Dar es Salaam.

Nakumbuka nilikuwa nakabidhiwa kwa dereva Kapesa Johari kijana wa Gerezani kwani nilikuwa bado mdogo niko shule ya msingi hata uhuru bado.

Niko Lindi ndani ya basi naangalia minazi na nyumba zilizoezekwa kwa makuti.

Hii Lindi machoni kwangu ilikuwa sawasawa na Dar es Salaam ya udogoni kwangu.

Nilikuwa katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes na mwaka ulikuwa wa 1993.

Hassan Mohamed Said Kinyozi amefariki.

Nimemtaja shujaa mzalendo huyu Maalim Hassan Mohamed Kinyozi, mtoto wa Sheikh Kinyozi aliyekuwa anaendesha moja ya madrasa maarufu mjini Lindi iliyofahamika kama Madrasa ya Sheikh Kinyozi.

Madrasa hii bado ipo hadi leo na baada ya kifo cha baba yake marehemu Hassan Kinyozi alisimamia chuo hiki na kuendelea kusomesha hadi kifo kilipomchukua hii leo.

Kuna mtu alinikumbuka wakati nilipokwenda Lindi kufanya utafiti na mahojiano na Rashid Salum Mpunga na Yusuf Mohamed Chembera.

Huyu ndiye aliyenitafuta na kunipa taarifa ingawa hatukupata kuonana tena toka mwaka ule wa 1993.

Ukisoma kitabu cha Abdul Sykes nikieleza historia ya TANU ni nani walioasisi chama cha TANU hapo Lindi utasoma maneno haya:

''...hawa wawili Ahmed Seif na Hassan Mohamed Kinyozi walikuwa ndiyo wafanyakazi wa kwanza wa TANU waliokuwa wakilipwa mshahara Southern Province.

Kwa ajili hii wakawa miongoni mwa wafanyakazi wachache sana walioajiriwa na TANU kwa wakati ule.

Suleiman Masudi Mnonji alitoa nyumba yake katika mtaa wa Makonde kuwa ofisi ya kwanza ya TANU kusini yote.

Baada tu ya kuanzishwa kwa TANU, Athumani Mussa Lukundu, kiongozi wa Lindi Dockworker's Union, aliunganisha chama chake na TANU.

Jambo hili kwa TANU lilikuwa la kuitia moyo sana kwa sababu Dockworker's Union ilikuwa na wanachama wengi na hatua ile iliongezea TANU nguvu.''

Bahati mbaya sana kuwa majina haya niliyoyataja hapo juu hayamo katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Naamini si wengi hata hapo Lindi kwenyewe wanaifahamu historia hii ya mzee wetu Hassan Mohamed Said Kinyozi.

Waasisi wakuu wa TANU ukimtoa Suleiman Masudi Mnonji walikuwa vijana wawili - Rashid Salum Mpunga na Yusuf Mohamed Chembera.
Baada ya kupokea taarifa ya msiba huu nikaanza kupiga simu huku na huku kutafuta picha ya marehemu.

Mmoja katika marafiki zangu wazawa wa Lindi akanitumia picha ya marehemu ya mwaka wa 1954 wakati huo akiwa kijana mdogo sana aliyopiga na wazee wa mjini wengi wao walikuja si muda mrefu kuwa mstari wa mbele katika TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Angalia picha ya pili hapo chini:

1.Aliyeketi chini mbele kushoto ni Hassan Mohamed Saidi Kinyozi
2. Aliyekaa kwenye kiti nyuma ya Hassan Kinyozi ni Rashid Salum Mpunga.
3. Aliyefunga tai ameketi ni Yusuf Mohamed Chembera.
4 Picha ilipigwa Ghana Restaurant 1954 na hii ilikuwa vilevile ni ofisi ya Lindi Seamens Club mahali walipokuwa wanakutana wanamji kwa mazungumzo na kituo cha harakati za TANU.
Picha ya tatu ni Hassan Mohamed Said Kinyozi katika ujana wake.

Sheikh Hassan Kinyozi ni mtu maarufu hata kwa wale ambao leo hawaijui historia yake kama mpigania uhuru.

Mtoto wa dada yake Bi. Salma bint Rashid ni mke wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.

Marehemu anategemewa kuzikwa leo Jumatano hapo Lindi.
Tunamwomba Allah amsamehe makosa yake na amweke Pepo ya Fidaus.

Amin.View attachment 2418084View attachment 2418085View attachment 2418131View attachment 2418132
Islamist
 
SHEIKH HASSAN MOHAMED SAID KINYOZI MPIGANIA UHURU NA MMOJA WA WAASISI WA TANU LINDI KAFARIKI DUNIA

Jioni hii imenifikia taarifa kutoka Lindi kuwa Hassan Mohamed Said Kinyozi mmoja katika vijana waliowasha moto wa kupigania uhuru wa Tanganyika Southern Province, yaani Jimbo la Kusini amefariki dunia akiwa na umri wa kiasi cha miaka 90.

Nakumbuka kama jana siku nilipofika Lindi kwa basi dogo nikitokea Mtwara.

Barabara ya Lindi Mtwara ilikuwa mbovu sana miaka ile basi likiendeshwa kwa tahadhari kubwa.

Nakumbuka tulipoingia Lindi tunaelekea stendi natazama yale mandhari ya mji nageuza shingo huku na huku zile nyumba naziona mfano wa nyumba za Mtaa wa Swahili Dar es Salaam miaka ya 1950.

Nami nimo katika basi la Dar es Salaam Motor Transport (DMT) natokea Moshi shule nakuja likizo Dar es Salaam.

Nakumbuka nilikuwa nakabidhiwa kwa dereva Kapesa Johari kijana wa Gerezani kwani nilikuwa bado mdogo niko shule ya msingi hata uhuru bado.

Niko Lindi ndani ya basi naangalia minazi na nyumba zilizoezekwa kwa makuti.

Hii Lindi machoni kwangu ilikuwa sawasawa na Dar es Salaam ya udogoni kwangu.

Nilikuwa katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes na mwaka ulikuwa wa 1993.

Hassan Mohamed Said Kinyozi amefariki.

Nimemtaja shujaa mzalendo huyu Maalim Hassan Mohamed Kinyozi, mtoto wa Sheikh Kinyozi aliyekuwa anaendesha moja ya madrasa maarufu mjini Lindi iliyofahamika kama Madrasa ya Sheikh Kinyozi.

Madrasa hii bado ipo hadi leo na baada ya kifo cha baba yake marehemu Hassan Kinyozi alisimamia chuo hiki na kuendelea kusomesha hadi kifo kilipomchukua hii leo.

Kuna mtu alinikumbuka wakati nilipokwenda Lindi kufanya utafiti na mahojiano na Rashid Salum Mpunga na Yusuf Mohamed Chembera.

Huyu ndiye aliyenitafuta na kunipa taarifa ingawa hatukupata kuonana tena toka mwaka ule wa 1993.

Ukisoma kitabu cha Abdul Sykes nikieleza historia ya TANU ni nani walioasisi chama cha TANU hapo Lindi utasoma maneno haya:

''...hawa wawili Ahmed Seif na Hassan Mohamed Kinyozi walikuwa ndiyo wafanyakazi wa kwanza wa TANU waliokuwa wakilipwa mshahara Southern Province.

Kwa ajili hii wakawa miongoni mwa wafanyakazi wachache sana walioajiriwa na TANU kwa wakati ule.

Suleiman Masudi Mnonji alitoa nyumba yake katika mtaa wa Makonde kuwa ofisi ya kwanza ya TANU kusini yote.

Baada tu ya kuanzishwa kwa TANU, Athumani Mussa Lukundu, kiongozi wa Lindi Dockworker's Union, aliunganisha chama chake na TANU.

Jambo hili kwa TANU lilikuwa la kuitia moyo sana kwa sababu Dockworker's Union ilikuwa na wanachama wengi na hatua ile iliongezea TANU nguvu.''

Bahati mbaya sana kuwa majina haya niliyoyataja hapo juu hayamo katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Naamini si wengi hata hapo Lindi kwenyewe wanaifahamu historia hii ya mzee wetu Hassan Mohamed Said Kinyozi.

Waasisi wakuu wa TANU ukimtoa Suleiman Masudi Mnonji walikuwa vijana wawili - Rashid Salum Mpunga na Yusuf Mohamed Chembera.
Baada ya kupokea taarifa ya msiba huu nikaanza kupiga simu huku na huku kutafuta picha ya marehemu.

Mmoja katika marafiki zangu wazawa wa Lindi akanitumia picha ya marehemu ya mwaka wa 1954 wakati huo akiwa kijana mdogo sana aliyopiga na wazee wa mjini wengi wao walikuja si muda mrefu kuwa mstari wa mbele katika TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Angalia picha ya pili hapo chini:

1.Aliyeketi chini mbele kushoto ni Hassan Mohamed Saidi Kinyozi
2. Aliyekaa kwenye kiti nyuma ya Hassan Kinyozi ni Rashid Salum Mpunga.
3. Aliyefunga tai ameketi ni Yusuf Mohamed Chembera.
4 Picha ilipigwa Ghana Restaurant 1954 na hii ilikuwa vilevile ni ofisi ya Lindi Seamens Club mahali walipokuwa wanakutana wanamji kwa mazungumzo na kituo cha harakati za TANU.
Picha ya tatu ni Hassan Mohamed Said Kinyozi katika ujana wake.

Sheikh Hassan Kinyozi ni mtu maarufu hata kwa wale ambao leo hawaijui historia yake kama mpigania uhuru.

Mtoto wa dada yake Bi. Salma bint Rashid ni mke wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.

Marehemu anategemewa kuzikwa leo Jumatano hapo Lindi.
Tunamwomba Allah amsamehe makosa yake na amweke Pepo ya Fidaus.

Amin.View attachment 2418084View attachment 2418085View attachment 2418131View attachment 2418132
Mungu ampokee mja wake
Hakika binafsi namshukuru kwa ushiriki wake kwenye harakati za uhuru.

Cha kushangaza ni kwamba Historia ya Uhuru imeandikwa kuanzia katikati kwenda juu. Na wenye clues wanaishia kuandika makala ambazo wapindisha historia wanapata nafasi ya kuzipinga na kuendeleza makosa ya kuwanyima haki walioshiriki mbio za uhuru.

Mungu akawafariji wafiwa, ndugu na jamaa wa marehemu
 
Back
Top Bottom