Mohamed Mpakanjia is no more!

Mohamed Mpakanjia is no more!

Inna Lillahi wa Inna illahi rajiun........ to Him we belong and to Him is our return..


haya basi mwacheni apumnzike leo hatulii?????mmmmmmmmmmmmm
 
kama wanaosema kwamba marehemu alikuwa ameathirika wanauhakika
na wanayoyasema basi hiyo sioni kama ni kuhukumu bali kusema lile
lililopo.

jamii inabidi ikubali kwamba kupata ukimwi si uthibitisho wa
mhusika kubobea katika ngono zembe bali ni hali ambayo inaweza mpata
mtu yeyote. tukifikia hapo kama jamii ninaamini kwamba waathirika hawataendelea kujificha na kuendelea kuishi maisha kana kwamba hawajaathirika bali watajitokeza na kuishi maisha ambayo hayatapelekea
kuwaambukiza wengine.
 
I am a new member to Jamii Forum, naamini nimefanya maamuzi sahihi kujiunga na sitajuta. ninfurahi kubadilishana mawazo na wanajamii wenzangu.
 
I am a new member to Jamii Forum, naamini nimefanya maamuzi sahihi kujiunga na sitajuta. ninfurahi kubadilishana mawazo na wanajamii wenzangu.

Karibu sana Mukani ingawa umeingilia toka juu ya paa. Kuna mlango wa kuingilia kama mgeni. Lakini si mbaya karibu sana hapa tuna msiba. Usishangae uko msibani watu hapa wanaongelea mambo ambayo usingekaa uyasikie kwenye misiba mingine yeyote. Nakuhakikishia hutajuta kujiunga hapa kijiweni bali utajuta kwanini ulichelewa kujiunga.
 
sasa bora uwe na mke mmoja au mpenzi mmoja na muwe waaminifu,Condom inapunguza tu maambukuzi na siyo kinga asilimia Mia.

Kwa si maustadhi mwisho wa ngapi? Mi naweka katika himaya yangu wa 4 ladha tofauti.
 
Kwa si maustadhi mwisho wa ngapi? Mi naweka katika himaya yangu wa 4 ladha tofauti.

AIDS Spread.jpg

Who is Next??

Mungu Ailaze Roho Yake Mahala Pema Peponi.... Amen

Heshima Mbele Great Thinkers
 
Kwa si maustadhi mwisho wa ngapi? Mi naweka katika himaya yangu wa 4 ladha tofauti.

Kuna watu walisema watabakia vichaa wa milembe tu maana gonjwa hili limeshika pabaya!EEH MUNGU TUFUMBUE MACHO.
 
Hakuna mtu anaechekelea kifo hasa kisicho kuhusu unless huyo mtu kuulia mama yako au mtu wa karibu kwa kukusudia ingawa utapata tuu mixed feelings hapo, nasema hivo sbb naona ni vema tukiongelea hivi hizi tabua mbaya za kuambukiza au kutokuwa mtulivu enzi za uhai ili kila mtu ajifunze toka hapo,
tz kuna uchafu wa ngono mwingi sana na usipo kuwa mtu wa ngono unaonekana mshamba sana sasa kama hapa tunapigana vita ya mafisadi kwann tusipigani vita vya UKIMWI na hali unatumaliza???
huku mahospitalini hapafai, huko kinamwananyamala hospt ukienda hutaamini utayayo yaona utanyooka tabis tuu lzm, tuongelee kwa uwazi UKIMWI ili kuokoa maisha, ili kupigana na gonjwa hili

Nawakilisha

Tuandamane,

Nadhani hii vita ya UKIMWI ipo tokea 1986 ilipoingia kutokea mpakani mwa Uganda kwenye kijiji kimoja Kashenye, Kanyigo, Bukoba hapo ndo kulikuwa na gulio la kufa mtu la Waganda/Watanzania huo ugonjwa ukiitwa Slim. Na wafanyabiashara karibia wote au 90% wote walikufa waliokuwa pembezoni.

Baadaye ndo ukaitwa ugonjwa wa UKIMWI hapo ukiwaunaenda kwa kasi ndo dawa za kupunguza makali zikapatikana. Baada ya watu kufa kwelikweli kwa kuhalisha/kukonda mabega/kunyonyoka nywele zote n.k. lakini hapo mikoa yote ikiwa imeshaambukizana hadi kufikia Mbeya tokea huko Uganda.

Sasa hivi huu ugonjwa kasi yake sio kama ile kwani dawa zipo zinasaidia huwezi hata kumtambua mgonjwa wa UKIMWI mpaka uambiwe.

Kinachoumiza sasa hivi mashirika ya misaada mengi sasa hivi yamefunga vilago wamesitisha kutoa misaada. Nasikia yamebaki mashirika mawili tu nayenyewe yakiwa njiani. Sasa hapo ndo kuna kazi maana hali itakuwa mbaya sana kwa hawa ambao walikuwa wanatumia madawa.

Kwa hiyo sitegemei unavyosema kuwa hapa JF hatutoi elimu kuliko ufisadi, huu ufisadi umekuja juzijuzi kama sikosei alikuja nao Dr. Slaa ndo ukajulikana. Lakini Ukimwi upo tokea zamani.

Ila ni vizuri labda MODS akafungua uwanja mpana wa kutolea mawazo hii kitu kwani janga lingine, tutashukuru.
 
Mkuu Ochu zinakwepeka kama utaamua na ukadhamiria. Vinginevyo kama mtu hujafanya maamuzi jua siku moja utaingia ndani ya mduara tu ,it is like a vicious cirle!!! Ni kutafuta kila namna kujizuia kuingia ndani yake. Kama mpaka sasa hujainiga basi apa kuwa hutaingia kwa njia tulizozoea bali kwa bahati mbaya kama ajali ukikuta damu zimeingiliana, sindano, n.k. Vinginevyo stick to your relationship basi!!!! Je hii haiwezekani mkuu?? Tatizo kila bucha unataka ununue nyama, utayamaliza??

Inawezekana, play your part!! Na usisahamu kuzungumzia mambo haya hata ndani ya familia yako au yule mpendaye, iwe is always a sub-topic mnapokutana!!!

Rest in Peace Med wa Mpakanjia.

Maane,

Huu ugonjwa hautabiriki! Nina kitabu cha takwimu kabisa hapa nilipo, takwimu zinaonyesha kuwa Wanandoa (Baba + Mama) ndo wanaoongoza kwa kupata maambukizi haya ya Ukimwi kwa walio wengi! hawa viruka njia wengi wanatumia kondom! hapo upo!
 
wewe margreth,sema gonjwa la ukimwi lipo nchini sio lilingilia tanzania kupitia kashenye,kanyigo hayo yote what for,hili si darasa la historia,for you information mgonjwa wa kwanza wa ukimwi was in 1956,baharia wa kimarekani.
 
Maane,

Huu ugonjwa hautabiriki! Nina kitabu cha takwimu kabisa hapa nilipo, takwimu zinaonyesha kuwa Wanandoa (Baba + Mama) ndo wanaoongoza kwa kupata maambukizi haya ya Ukimwi kwa walio wengi! hawa viruka njia wengi wanatumia kondom! hapo upo!
Wanandoa wanaongoza nadhani kwa sasa wamezoea peku na wenza wao hivyo wakitoka nje condom hawaziwezi.
 
wewe margreth,sema gonjwa la ukimwi lipo nchini sio lilingilia tanzania kupitia kashenye,kanyigo hayo yote what for,hili si darasa la historia,for you information mgonjwa wa kwanza wa ukimwi was in 1956,baharia wa kimarekani.

wewe mhaya kabisa jamani penye ukweli usemwe hata kama unauma
 
for you information mgonjwa wa kwanza wa ukimwi was in 1956,baharia wa kimarekani.

Habari za kwenye vijiwe vya kahawa...naomba source mkuu....unajua lini wewe HIV virus was isolated?

HIV was first isolated in 1983 separately by the Robert Gallo lab at the
U.S. National Institutes of Health and Luc Montagnier lab at France's
Pasteur Institute

Hiyo 1956 ni habari za kwenye mabao na draft
 
Habari za kwenye vijiwe vya kahawa...naomba source mkuu....unajua lini wewe HIV virus was isolated?



Hiyo 1956 ni habari za kwenye mabao na draft
kuna maiti ilikuwa exhumed for other checks,not long ago na hey presto wakagundua huyu mtu unknown to them at that time had succumbed to aids
 
Back
Top Bottom